YU WAPI DESMOND TUTU WETU TANZANIA?

MAKALA HII ILITOKA KWENYE GAZETI LA RAI 2005

YU WAPI 'DESMOND TUTU' WETU TANZANIA?


RAI toleo Na 587,Paulo Mapunda, aliandika makala yenyekichwa cha habari: Yu wapi Desmond Tutu wetu Tanzania.Makala hii ilifanana kwa karibu na makala ya PrinceBagenda, kwenye toleo hilo hilo yenye kichwa chahabari: Ushirikina wa ushindi wa kishindo. PauloMapunda, anahoji:" Najaribu kutumia rejea mbalimbali kuwashtua kutokausingizini viongozi wetu wa dini ili tuweze kuwapatakina Desmond Tutu wa Tanzania...... Yu wapi DesmondTutu wetu, mtu anayeweza kuzinduka toka usingiziniakafumbua macho kuangalia, kutazama na kusikilizasauti za watu walio nyikani watesekao kwanjaa, magonjwa yanayotibika na yasiyotibika uporaji wamamilioni ya walipa kodi, ujambazi, ukosefu wa ajira,akakemea juu ya ongezeko la ufa kati ya matajiri(watawala) na masikini (watawaliwa)" (RAI 587).Kwa Mtanzania aliye makini, kilio cha Paulo Mapunda,hakitofautiani na cha Prince Bagenda, pale anaposemahivi: "Kama mtu akitamka kwamba Chama Cha Mapinduzikimeshinda kwa haki katika chaguzi hizi, basi kwa ninitusiamini kwamba hayo ni matayarisho ya vurugu kubwazitakazojitokeza mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu 2005? Nayote haya yanatokea wakati viongozi wetu wa diniwanabuni wakorofi na wenye kutaka kuleta vurugu kwenyeuchaguzi Mkuu, wakati tayari kuna chama kinajulikanana kimekwisha kuanzisha vurugu, lakini viongozi wetuwa dini wanakionea haya?" (RAI 587).Kabla ya kuwaangalia Paulo Mapunda na Prince Bagenda,kwa jicho moja, kuna machache ya kuweka sawa. Nikianzana Mapunda, badala ya kuhoji: Yu wapi Desmond Tutuwetu Tanzania, angelihoji: Yu wapi Askofu wetu waAnglikana Tanzania. Kwa haraka inaweza kuonekanahakuna tofauti. Desmond Tutu, ni Askofu, hivyo inatoshakusema yuko wapi Desmond Tutu, kila mtu akafahamu nijuu ya maaskofu wote! Labda wengine wangependaMapunda, anahoji hivi: Yu wapi Askofu wetu wa Tanzania?Au mbona maaskofu wetu hawajitokezi kukemea maovukatika taifa letu? Kwa mchambuzi makini kuna tofautikubwa. Kanisa la Anglikana, lina historia ya kutoaviongozi shupavu, jasiri na wanaojisimamia, viongoziwanaotanguliza taifa lao na kuyaweka mbele maslahi yaraia katika taifa husika. Maaskofu wasiotangulizamaslahi yao binafsi ambao wako tayari kutoa maisha yaokwa manufaa ya wengine. Askofu Desmond Tutu, ni kutokakatika kanisa la Anglikana. Aliyoyafanya na ambayoanayafanya Afrika ya Kusini, tuliyasikia na badotunayasikia. Askofu wa Uganda, aliyesimama na kupingautawala wa Iddi Amin, alikuwa ni wa kanisa laAnglikana. Wakati maaskofu wa makanisa menginewaliendelea kumkumbatia Iddi Amin, na kumtukuza iliayapendelee makanisa yao, Askofu wa Anglikana,alikataa kuendelea kukumbatia uovu, alisimama bilawoga na kumpinga Iddi Amin, alimwambia aache kuuawatu, atawale kwa kufuata katiba na sheria, alipotezamaisha yake mikononi mwa Iddi Amin, wakati akiteteahaki za raia wa nchi yake ya Uganda. Tumesikia jinsimaaskofu Waanglikana wa Amerika, walivyompatiaUaskofu, mchungaji Shoga. Hili ni tukio liliopigiwakelele na dunia nzima. Lakini, maaskofu waKianglikana, hawakuyumba kwa vile walikuwa wanaangaliaumuhimu wa Askofu Shoga, katika kutoa huduma kwa raiawa nchi yake. Ipo mifano mingi inayoonyesha msimamousio yumba wa viongozi wa kanisa la Anglikana. Kwaninisisi Tanzania, hatuna Askofu wa Anglikana, aliyeshupavu ka wenzake? Baadaye tutaona ni kwa niniviongozi hawa wa kanisa la Anglikana wanakuwa namsimamo imara.Kwa upande wa Prince Bagenda, jambo la kuweka sawakabla ya kuendelea na mjadala ni pale anaposema:" Nakumbuka maneno ya Mhashamu Kilaini aliyotoa baadaya mauaji ya waandamanaji Pemba, Januari 27 2001.Askofu Kilaini alisema kwamba polisi wasiwaue raialakini vilevile raia wasiwachokoze polisi. Hivyokatika mantiki ya Askofu Kilaini, suala la polisikuwaua raia waliokuwa wakiandamana linalinganishwa namatatizo ya raia kuwachokoza polisi. Na pale raiawanapowachokoza polisi adhabu yao yaweza kuwa kifokutokana na mashambulizi ya polisi....).Sina hakika Prince Bagenda, anamfahamu Askofu Kilaini,kwa kiasi gani. Kama ni kweli aliyatamka hayoyaliyonukuliwa na Bagenda, basi hayakuwa maoni yaAskofu Kilaini, bali kivuli chake. Askofu Kilaini nimsomi wa hali ya juu, ni mtu anayeheshimu haki zabinadamu, utawala wa katiba na sheria, ni mtu mwema namzalendo. Wale wanaomfahamu kwa karibu wanajua jinsianavyokuwa akipigana na nafsi yake wakati akiendeshamajadiliano ya mambo mbalimbali katika luninga. Aminiusiamini anayeonekana kwenye luninga, anakuwa siAskofu Kilaini, bali kivuli chake. Mfano paleanapolinganisha ugonjwa wa UKIMWI, na ugonjwa wakisukari. Kwamba kama mgonjwa wa kisukari anakatazwakutumia sukari, basi na mgonjwa wa UKIMWI, akatazwetendo la ngono. Huyo si Askofu Kilaini, bali kivulicha Askofu Kilaini. Askofu Kilaini, ni kati yamaaskofu wachache wanaofahamu kwamba kazi ya Serikalisi kuwaua raia wake ambao wakati huohuo ni waumini wadini na madhehebu mbalimbali, anajua jinsi ilivyomuhimu kwa viongozi wa dini kulinda na kutetea uhai.Yeye Askofu Kilaini, kama Kilaini, hawezi kutoamatamshi yanayopingana na uhai. Ni mtu makini, mtu wawatu na mtu wa Mungu! Kivuli chake kinawezakuteteleka, lakini si Kilaini! Hoja hapa ni kutakakumfahamisha Bagenda, kwamba hatuwezi kupambana navivuli! Mapambano ni lazima yaelekezwe kwa kituchenyewe kinachozalisha kivuli! Ni kitu gani hicho?Tutakigusia wakati tukiwajadili na kuwaangalia Bagendana Mapunda, kwa jicho moja.Bagenda na Mapunda, wanapiga vita ukimya wa viongoziwetu wa dini hapa Tanzania. Mapunda anasema: "Viongozi wetu wa vikundi vya kijamii na hasa hasadini mara zote wamekuwa kimya dhidi ya maamuzi mabaya,yasiyo na visheni yafanywayo na Serikali hii ya awamuya tatu...". Kwa maneno mengine lakini kwa kutaka kuelezea kitukilekile Bagenda, anasema: "Kuna unafiki mkubwa unafanywa na wakuu wa dini namadhehebu ambao wana nafasi ya kujua lakini wanatumiahisia na mazoea. wanaona fahari kuwa upande wa wenyemadaraka na kuwaombea, bila kutaka kujua waumini waowako katika hali gani?".Unaweza kuuitaunafiki, ukimya, woga, ufahari, kujipendekeza, utumwa, ulemavuwa fikra nk. lakini hali hii ya viongozi wa dini zetuinaelezeka. Dini kubwa tulizonazo hapa Tanzania,Uislamu na Ukristu ni dini za kigeni. Zililetwa nakupandikizwa. Kwa bahati mbaya mizizi yake haikushikavizuri! Zilibaki kuwa dini za kigeni hadi leohii Zinatawaliwa na kupokea maelekezo kutoka nje.Zinaendeshwa kwa misaada na pesa za kutokanje. Viongozi kama maaskofu wanateuliwa kutoka nje nasi kwa kuzingatia matakwa na mahitaji ya nchi husika,bali kwa kuzingatia maslahi ya dini husika yenye makaomakuu nje ya nchi Uzalendo wa mtu na mapenzi yake kwawatu wake na nchi yake si kitu kinachotiliwa maanani.Kwa kutaka au kutotaka viongozi hawa wanakuwavibaraka. Hali hii inawafanya kuonekana kama vivuli.Wanasema na kusimamia yale wanayotumwa. Ukiliwekakanisa la Kianglikana pembeni, Ukristu na Uislamuzimebaki ni dini za kigeni. Anglikana, walifanikiwakujizingarisha. Ndio maana tunasikia the church ofUganda,The province of Tanganyika, The Church ofKenya, the church of England, nk. Kanisa la Anglikana,linakuwa na uhuru wa kuamua mambo yake katika nchi.Viongozi wake wanachaguliwa kulingana na mazingira yanchi. Hii inatoa mwanya kwa watu wenye uzalendo nauchungu wa nchi kujipenyeza na kufikia madarakamakubwa katika kanisa hilo na kuweza kuitumia nafasihiyo kutetea maslahi ya raia. Kwa njia hii alipatikanaAskofu Mkuu Desmond Tutu na yule Askofu wa Uganda,aliyepoteza maisha yake mikononi mwa Iddi Amin. Ndeomaana inashangaza Tanzania, kushindwa kumpata DesmondTutu, wetu, Askofu shupavu wa kanisa la Anglikana laTanzania.Ili hoja yangu ilieleweke vizuri, nitoe mfano wakanisa katoliki ambalo ninalifahamu vizuri. Kwa Askofuwa kanisa katoliki, kanisa ni kubwa kuliko Tanzania.Analiangalia kanisa lote kabla ya kuiangaliaTanzania. Hawezi kujiingiza kwenye kitu chochote chenyekuleta matata bila kusikiliza kwanza viongozi wakekule ROMA, wanasema nini. Mfano mzuri ni nchi za LatinAmerika, ambazo karibu wakazi wake wote ni Wakatoliki.Nchi hizi zimekuwa zikitawaliwa kwa mabavu, uchumiwote wa nchi uko mikononi mwa watawala, ardhi nzuriiko mikononi mwa watawala na washirika wao, wakatiraia wanaongelea kwenye umasikini unaonuka! Kanisalimekuwa upande wa hawa watawala wa mabavu, maanaMaaskofu wanachaguliwa kutoka ROMA, Vatican, imekuwana uhusiano wa karibu na wakati mwingine kuwa na hisa katikamakampuni makubwa ambayo mara nyingi yanaunga mkonoutawala wa mabavu katika nchi za dunia ya tatuinayozijumuisha nchi za Latin Amerika. Mapadre namaaskofu, walioamua kuwa upande wa wanyonge,walitengwa na kanisa na kupachikwa jina la waasi.Baadhi yao wamejiunga na makundi ya wapiganaji wamsituni.Askofu wa Kanisa Katoliki, anaweza akahamishwa kutokaTanzania na kwenda kufanya kazi nchini Ghana, India auRoma, na kufa na kuzikwa huko. Kanisa, ni kubwa kulikonchi zao. Uzalendo wao ni wa kanisa zima! Maaskofuwetu hawajui adha ya umasikini, wana majumba mazuri,wana magari mazuri, wanakula chakula cha kila aina,wakiugua wanapelekwa Ulaya. Hawaguswi na adha yarushwa. Kwa vile kanisa ni kubwa kuliko nchi kama vileTanzania, matatizo ya nchi moja yanafunikwa na neemakutoka nchi nyingine na mara nyingi kutoka nchi zadunia ya kwanza. Mazingira wanamoishi ni vigumukuamsha moyo wa uzalendo kiasi cha kusimama nakutetea haki za raia. Mazingira wanamoishi hayawezikuwaruhusu kuangalia, kutazama na kusikiliza sauti zawatu walio nyikani watesekao kwa njaa magonjwayanayotibika na yasiyotibika, uporaji wa mamilioni yawalipa kodi, ujambazi ukosefu wa ajira, na kukemea juuya ongezeko la ufa kati ya matajiri na masikini kamaambavyo Mapunda, anapendekeza. Ndio maana viongozi wetuwa dini wanafanya yale anayoyalalamikia Bagenda: "Mara nyingi tumeona viongozi wakuu waliomo ndani yaSerikali na chama tawala, wengine ambao wanadaiwa kuwawala rushwa, ndio wanaoongoza harambee za kuchangishamamilioni kwa ajili ya shughuli za kanisani namisikiti". Haya yanatokea kwa sababu viongozi wa dini hawaguswina maisha ya hapa Tanzania. Wanaishi kwenye mfumomkubwa zaidi ya Tanzania. wanaishi kwenye mfumounaoweza kuwaruhusu kupata kitu chochote au hudumayoyote kutoka nje.Ni vigumu kumtegemea mtu asiyeishi maisha ya watuasimame na kuwatetea! Viongozi wetu wa dini ni wagenikatika nchi yao. Hawana uchungu, kwa vile hawaguswi nakitu! Wanaweza kuvumilia serikali zote ilimradiwaruhusiwe kufanya mambo yao bila kuingiliwa.Waruhusiwe kuingiza magari bila kutozwa ushuru,wafanye biashara bila kulipa kodi, wamiliki ardhi kubwana wakati mwingine wawe juu ya sheria!Nimetoa mfano wa kanisa katoliki. Lakini hataukiangalia yale yanayoendelea kule KKKT utasemayanafanywa na watu wenye uchungu na nchi? Ni naniasiyeona kwamba maaskofu wa KKKT, wanatangulizamaslahi binafsi? Wanavunja amani na kuivuruga imani yawatu wanaowaongoza. Wanataka kila Tarafa iwe naDiosisi, kila kabila liwe na Diosisi yake. Wanatakakuigawa Tanzania, katika kanda. Mambo yakienda vibayatukianza kuchinjana wengi wao watakimbilia Amerika naGermany. Utapeli ulioufanya na Askofu Mgwamba, wa KKKTDar, angelikuwa mtu wa kawaida angekuwa anasota kuleKeko. Sasa yeye Bwana Askofu anapeta kule Marekani!Kama tunataka dini zetu zisaidie kuchangia katikamaendeleo na ustawi wa taifa letu ni lazima tufanyejitihada za kuzilazimisha kujizingarisha. Tuwe naviongozi wetu wa dini wanaoweza kufanya maamuzi kwakujitegemea bila kusikiliza maamuzi kutoka nje ya nchi.Tuwe na viongozi wanaoishi na kuguswa na maisha yawatu wa kawaida, wanaoguswa na maendeleo ya Taifa lao.Bila hivyo ni ndoto kumpata Desmond Tutu wetu waTanzania na ni upuuzi kutegemea mchango wa maanakutoka kwa viongozi wetu wa dini katika siasa za Taifaletu.Dini zetu kubwa Uislamu na Ukristu, zikiendelea kuwani dini za kigeni, tutaendelea kushuhudia vivuli. Kamanilivyodokeza hapo juu, ni vigumu kupambana na vivulina ni makosa kuvilaumu vivuli, maana kivuli si kituhalisi! Ingawa pia kivuli si kitu cha kupuuzia, kwavile kinatoa picha ya kitu halisi, kwa vile kinawezakuchangia kuwadumaza watu na kuwaletea ulemavu wafikra, kuna ulazima wa kufuatilia chanzo chake. Nilazima kupambana na kitu halisi kinachozalisha kivuli!Tukifika hatua hii tutakuwa tumepiga hatua ya kuelekeamwanzo mpya!

Na,

Padri Privatus Karugendo.

0 comments:

Post a Comment