tag:blogger.com,1999:blog-38223885923816691892024-03-04T23:20:24.452-08:00Karugendo BlogNews and Writing from Privatus Karugendopkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.comBlogger364125tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-57713280625598931992013-12-10T00:30:00.000-08:002013-12-10T00:30:09.108-08:00SAFINA MARIA MAGDALENA JESUS<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59199" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59198" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">MWANA MAMA MCHUNGAJI SAFINA MARIA MAGDALENA JESUS.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59196" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59122" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59121" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Leo katika safu yetu ya Mwana Mama, tunawaletea Mchungaji Safina Jesus. Yeye
mwenyewe, anapenda ajulikane kwa jina lake kamili ambalo ni: Mchungaji Safina
Maria Magdalena Victoria Jesus. Waliomfahamu siku za nyuma na hata alipokuwa
akiishi na kufanya kazi nchini Uingereza, walimfahamu kwa jina la Safina
Yussaph Haruna. Ni mwana mama aliyekulia kwenye imani ya Ukatoliki, akaingia
kwenye imani ya <span> </span>Uislamu na hatimaye
kupokea wito wa kuwa mchungaji na kupokea kipaji cha uponyaji mwaka 2011, akiwa
nchini Uingereza. Kwa ufupi ni kwamba ni mama aliyeonja imani zote, Ukristu wa
dhehebu mbali mbali na Uislamu.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59202" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59201" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Hapana shaka kwamba uzoefu wake wa imani hizi zote ndo unamsukuma kuwa na
hamu na shauku la kuanzisha nyumba ya ibada, kanisa la watu wote; wenye imani
tofauti, maoni tofauti lakini wenye nia na lengo la kujenga jumuiya yenye
mshikamano na upendo. Jumuiya yenye maendeleo na heshima kwa binadamu wote bila
ubaguzi wa aina yoyote ile.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59205" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59204" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Mbali na mvuto wa mama huyu kwenye huduma ya uchungaji na uponyaji, ni
mapenzi yake kwa watoto yatima. Amejipanga kufungua kituo cha watoto yatima
kule Kigamboni, ili watoto hawa wapate elimu ya kuwasaidia kuacha kuzurura
mitaani na kuomba omba. Yeye ana imani kwamba haitoshi kumsaidia mtoto Yatima
chakula na nguo, maana mahitaji ya kila siku ni lazima yaendelee maisha yake
yote; hivyo ni lazima kumsaidia mtoto yatima ili aweze kujisaidia mwenyewe.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59208" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59207" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">KITUO cha watoto yatima kinatarajiwa kujengwa jijini Dar es Salaam
ambacho kitachukua watoto zaidi ya 1000 na kwamba watoto hao watapewa elimu ya
ufundi kwa ajili ya kujiandaa na maisha ya kujitegemea na kuachana na
kuombaomba</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59212" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;"><span> </span></span><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59211" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;"> “Watoto
watajifunza kupitia walimu waliobobea ili kuweza kuwa chachu ya kujiajiri
baada ya umri wa kujitegemea na kuongeza nguvu kazi ya taifa. Hatuwezi
kuendelea kuhubiri injili wakati watoto wako mitaani, hivyo lazima tuwe na njia
mbadala za kuweza kusaidia taifa hili ikiwa ni pamoja na kujenga vituo vya
watoto yatima ambao watapata elimu ya kiroho na elimu ya kujitegemea kwa kuwa
na ujuzi,” alisema Safina . </span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59215" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59214" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Pia anasema alipokuwa nchini Uingereza kiu yake ilikuwa inamtuma
kufanya jambo linalohusiana na watoto akiwa nchini Tanzania kwa kujenga kituo
ambacho kitakuwa sehemu ya chuo kwa ajili ya watoto yatima na mitaani kupata
elimu ya ujuzi mbalimbali.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59218" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59217" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Mwana mama huyu alizaliwa Iringa mnamo
mwaka 1979, Baba yake anatokea Iringa, wakati mama yake anatokea Bukoba. Baada
ya masomo yake, alifanya kazi kwenye jiji la Dar-es-Salaam na hasa kwenye sekta
ya mahoteli. Baadaye alihamia nchini Uingereza na kuishi kwenye bonde la Bevois
na kufanya kazi Bexhill,East Sussex kwenye kanisa la Mtakatifu Barnabas. Ni
wakati huo alipoitwa kumtumika Bwana Yesu.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59221" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59220" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Mama huyu, alipata daraja la uchungaji
kutoka kwa Mheshimiwa sana Askofu Mkuu Richard Palmer, wa Episcopal Free Church
ya Southampton. Na baada ya kumpatia daraja hilo Askofu Mkuu huyo alisema hivi
juu ya Mama huyu: “ Nafurahi sana kuwa na mchungaji huyu kama mtumishi,
nafikiri atakuwa mzuri sana, ni mtu aliyejitoa kwa moyo wake wote kwa huduma
hii”.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59224" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59223" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Lengo la mama huyu hapa Tanzania, ni
kujenga uhusiano kati ya Kanisa la Mtakatifu Barnabas na Tanzania; kuamusha
imani ya kumpenda na kumtumikia bwana Yesu Kristu kwa matendo. Pia ana ndoto za
kupanua huduma hii kwenye nchi mbali mbali za Afrika na popote pale ambapo roho
mtakatifu atamwelekeza.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Wakati anajiandaa kupata sehemu ya
kujenga nyumba ya Ibada, anaendelea kusali na kuhubiri kwenye nyumba yake
maeneo ya Kimara. Anawakaribisha watu wa imani zote, maana lengo lake kubwa ni
kuijenga jumuiya ya watoto wa Mungu, wanaokutana kusali pamoja na kushirikiana
kujenga jumuiya yenye amani na maendeleo.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59227" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59226" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Mama huyu anapinga mwenendo wa Mashoga
na wasagaji; anapinga kwa nguvu zote watu wanaokubali na kukumbatia utamaduni
huu, pia anapinga kwa nguvu zote wanaowalaani na kuwatenga mashoga na
wasagaji.<span> </span>Msimamo wake ni kwamba watu
hawa pia wanahitaji huruma ya mwenyezi Mungu. Kazi ya jamii si kuwatenga watu
hawa na kuwalaani, bali ni kwasikiliza, kusali nao na kutafuta njia ya kuwasaidia
na kuwabadilisha. Anatoa ushuhuda wa kuwasaidia baadhi ya watu hawa na sasa
wameachana na tabia hiyo. Hivyo nyumba yake ya ibada inawakaribisha wa watu wa
aina zote.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59230" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59229" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Pia Mama huyu ni miongoni mwa
wanaoamini kwamba Bwana Yesu, aliliacha kanisa lake mikononi mwa Mwanamke,
yaani Maria Magdalena. Biblia inaeleza vizuri kwamba Maria Magdalena, ndiye
aliyesifiwa na Bwana Yesu, kuyafahamu mafundisho yake na kuyashika. Ingawa
baadaye mfumo dume, uliingia kanisani mnamo mwaka 321 ukiongozwa na Mfalme
Constatine wa himaya ya Warumi, na kubadilisha ukweli wote wa kanisa kuachwa
mikononi mwa mwanamke. Hivyo anawahimiza wanawake popote walipo kujitokeza
kuliongoza kanisa. Wanawake kujitokeza kupokea huduma ya uchungaji na utumishi.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59233" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59232" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Mambo manne yanamtofautisha mama huyu
na wachungaji wengi tuliowazoea: Kwanza ni mtizamo wake juu ya watoto Yatima;
lengo lake la kuwasaidia watoto yatima ili baadaye wajisaidie wenyewe ni
tofauti na nyumba za watoto yatima tulizozizoea za kuwapatia chakula, malazi,
matibabu na wakati mwingine masomo, bila mpango mzima wa kuwaandalia maisha ya
baadaye.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Pili, msimamo wake juu ya mashoga na
wasagaji ni tofauti kabisa na kauli nyingine ambazo tumezizoea na kuzisikia.
Hili la kuwapokea, kuwasikiliza na kuwasaidia kubadilika ni jipya kabisa na ni
jambo zuri na la kuungwa mkono na wanaharakati wote wa kutetea haki za
binadamu.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Tatu; mpango wake wa kuwashirikisha
watu wote wa imani mbali mbali, kusali pamoja na kufanya kazi pamoja, ni muhimu
sana hasa wakati huu ambapo dalili za kutoelewana miongoni mwa imani mbali
mbali hapa chini linaanza kujitokeza.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59236" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59235" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Nne, imani yake kwamba Kanisa liliachwa
kwenye Uongozi wa mwanamke, ni jambo linalomtofautisha Mwana mama huyu na
wachungaji wengine tuliowazoea. Hivyo huyu ni Mwana mama wa mfano kwetu sote.
Huyo ndiye Mchungaji Safina Maria Magdalena Victoria Jesus.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59254" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59252" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59251" lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv2418849405MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_59249" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-85224921792493212052013-12-10T00:28:00.003-08:002013-12-10T00:28:17.195-08:00TGNP<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58223" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58222" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">TGNP NA MPANGO WA UTAFITI SHIRIKISHI WA URAGHABISHI.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58225" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58228" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58227" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Katika jitihada zake za kupambana na mfumo dume, uliberali mamboleo na
mifumo yote kandamizi na kupambana ili rasilmali ziwanufaishe wanawake walioko
Pembezoni, TGNP imeanzisha mpango wa utafiti shirikishi wa uraghabishi. TGNP,
imeamua kuukumbatia mpango huu kwa vile unatoa nafasi pana ya ushirikishwaji
hadi ngazi ya vijijini na kuchochea kuibua kero na changamoto nyingi ambazo
zinahitaji majibu ya jamii nzima.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58231" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58230" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mpango huu unatumika kama mbinu muhimu ya kujifunza, kutafakari, kuchambua
na kutekeleza mikakati mbali mbali ya ujenzi wa Tapo la ukombozi wa wanawake
kimapinduzi lililokita katika ngazi za msingi ya kijamii na lenye uwezo kwa
kudai uwajibikaji katika kutoa huduma bora, kusimamia rasilimali za taifa ili
ziwanufaishe makundi yaliyoko pembezoni hususani wanawake.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58234" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58233" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Lengo kuu na mpango huu wa utafiti shirikishi wa uraghabishi ni kuwezesha
ushiriki wa wanawake, wanaume, makundi na mitandao katika ngazi ya jamii
kufanya uchambuzi wa hali halisi kwa mrengo wa ukombozi wa wanawake
kimapinduzi; kuibua kero na changamoto zinazokabili makundi husika<span> </span>na za pamoja. Mpango huu pia unalenga katika
kukuza uwezo na uelewa wa<span> </span>uchambuzi wa
kero zinazoikabili jamii.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58238" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58237" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tamko la TGNP kwa vyombo vya habari lilitolewa tarehe 9.6.2013 ni la mpango
huu ulioendeshwa kwenye wilaya tatu za Mbeya vijijini, kata ya Mshewe, Morogoro
vijijini Kisaki na Kishapu – Shinyanga. Katika makala hii tutajadili mrejesho
wa utafiti huu ambao ni wa aina yake.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58241" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58240" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Changamoto za uwekezaji na mgawanyo mbaya wa ardhi kwa wananchi,
ilijitokeza katika utafiti huu na mfano mzuri ni Kata ya Mshewe Mbeya vijijini.
Katika kata hii utafiti ulibaini mgawanyo mbaya wa ardhi kwa wawekezaji; ardhi
nzuri na yenye rutuba imetolewa kwa wawekezaji kiasi kwamba wenyeji hawana
mashamba na wanalazimika kuwa vibarua kwenye mashamba ya wawekezaji. Mbaya zaidi
ni kwamba wawekezaji wenyewe wanawalipa kidogo. Mfano wanawake wanalipwa kati
ya shilingi 2,500 hadi elfu3 kwa siku. Pamoja na kulikwa kidogo, wanakumbana na
rushwa ya ngono na manyanyaso mengine hali inayosababisha ongezeko la magonjwa
ambukikizi yakiwemo VVU na Ukimwi.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58244" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58243" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Changamoto hii ya mgawanyo mbaya wa ardhi imejitokeza pia katika kata ya
Kisaki, Morogoro mjini, ambapo wakulima wadogo wadogo wanapambana na wafugaji.
Kwa vile wafugaji hawana maeneo ya kutosha kwa mifugo yao, wanaingiza mifugo
kwenye mashamba ya wakulima na kuleta vita mbaya. Kwa upande mwingine wafugaji
wanatumia fedha kuwahonga viongozi ili wasisumbuliwe wanapoingiza mifugo kwenye
mashamba ya wakulima. Matumizi ya fedha ni kupokonya wanyonge haki zao ni
tatizo sugu kwa wananchi waishio pembezoni.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Suala jingine muhimu lililojitokeza kwenye utafiti huu wa TGNP kwenye
wilaya tatu, ni upatikanaji wa maji safi na salama. Pamoja na sera ya taifa
kwamba maji yawe umbali wa mita 400 kutoka kwa makazi ya watu, bado maeneo
mengi hapa Tanzania yana tatizo kubwa la kupata maji safi na salama. Watu wa
Kishapu na<span> </span>Mshewe, ni miongoni mwa
wananchi wa Tanzania ambao bado wana tatizo hili kubwa. Kijiji cha<span> </span>Ilota- Mshewe, wananchi wanalazimika
kuchangia maji machafu na mifugo. Tatizo hili la maji sai na salama ni kubwa
sana katika vijiji vya Isoso na Lubaga katika kata ya Kishappu, wanawake
wanatembea mwemdo mrefu na katika mazingira hatarishi kutafuta maji; mazingira
haya yanasababisha mimba za utotoni, ubakaji na vipigo kwa wanawake wakichelewa
kutoka kuchota maji. Na nyongeza ni kwamba muda mwingi na rasilmali vinatumika
kusaka maji kitu kinachoongeza hali ya umasikini katika jamii ya watu hawa
Kishapu.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ukosefu wa huduma bora za afya ni suala jingine lililoibuliwa na mpango wa
utafiti shirikishi wa uraghabishi. Mfano kati<span>
</span>ya wanawake 20 walihojiwa katika kijiji cha Ilota, Mbeya vijijini ni
mwanamke mmoja tu ndiye aliyetaja kujifungulia hospitali. Umbali wa hospitali
na vituo vya afya unawalazimisha wanawake wengi kuzalia nyumbani kwa wakunga wa
jadi. Hii ni hatari kwa mama na mtoto na kuna ukweli wa wanawake wengi kupoteza
maisha wakati wa kujifungua na watoto kutopata huduma muhimu za chanjo wakiwa
na umri chini ya miaka 5.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kata ya Kisaki Morogoro vijijini, tatizo si hospitali wala kituo cha afya,
tatizo ni dawa na wahudumu wa afya katika vijijini vya Gomero, Station na
Nyarutanga. Vijiji hivi vina majengo mazuri, lakini hakuna dawa na wahudumu.
Mbali na tatizo hilo, pia inapobidi wananchi wanachangia gari la wagonjwa
silingi 70,000, ili kumpeleka mama mja mzito kwenye hospitali ya Mkoa Morogoro
mjini. Hali hii ni hatari, maana wanawake wengi wanaweza kupoteza maisha yao
kwa kushindwa kulipia hizo shilingi elfu 70,000.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ukiachia masuala hayo yaliyotajwa hapo juu, utafiti huu wa TGNP, ulibaini
kwamba tatizo la msingi ni uongozi mbovu na rushwa. Hili lilitajwa kila sehemu
iliyofanyiwa utafiti. Kwamba uongozi mbovu na rushwa vinasababisha ukosefu wa
huduma za msingi kwa wanawake na wanaume walioko pembezoni. Na kwamba kuna
usiri wa taarifa za mapato na matumizi, viongozi kutowashirikisha wananchi
katika masuala ya maendeleo, viongozi ngazi za vijiji kuruhusu video za ngono
na viongozi kutotekeleza ahadi zao kwa wananchi.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ni mengi yaliyojitokeza kwenye utafiti huu, ila yametajwa machache ili
kufikisha ujumbe kwa wahusika, ili wajaribu kutafuta majibu ya kuondoa unyanyasaji
wa wanawake na wasichana katika wilaya hizi zilizotembelewa na watafiti wa TGNP
pamoja na maeneo mengine ndani ya taifa letu. Mfano tatizo la maji
linasababisha vipigo kwa wanawake, ubakaji, elimu duni kwa wasichana, mimba za
utotoni na ukosefu wa kipato.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58247" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58246" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Serikali kuu na serikali za mitaa zinaweza kuyatumia matokeo ya utafiti huu
kurekebisha matatizo yaliyoorodheshwa hapo juu: Mfano serikali kuirejesha ardhi
ya Kata ya Mshewe inayomilikiwa na wawekezaji wa n nje na ndani ya nchi, kwa manufaa
ya wananchi sasa na vizazi vijavyo. Pia serikali itenge maeneo ya wafugaji
katika kata ya Kisaki, ili kuepesha mapigano kati ya wakulima na wafugaji.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58250" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58249" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Huduma ya kupatikana maji safi na salama ishughulikiwe katika vijiji
vilivyotajwa na ambavyo havikutajwa. Utafiti huu umeonyesha wazi kwamba maji
safi na salama ni muhimu kwa watanzania wote. Huduma ya hospitali pia nayo
iboreshwe. Pia ni muhimu kuwepo na mfumo wa kuwawajibisha viongozi wote
wanaokiuka maadili ya kazi zao ili kuondokana na aina zote za rusha na ukatili
wa kijinsia hasa ukatili kwa wanawake na wasichana.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58253" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58252" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Lakini pia viongozi wawakilishi hususan madiwani na wabunge wanaweza
kutumia matokeo ya utafiti kudai uwajibikaji wa serikali kwa wananchi katika
ngazi zote kupita bajeti, ripoti ya mkaguzi wa serikali, kudai sera ya haki ya
uhuru wa wananchi na mikakati mbali mbali ya maendeleo.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58256" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58255" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Vyombo vya habari, taasisi za utafiti na makundi ya kiraia yanaweza pia
kuutumia mpango huu wa utafiti shirikishi wa uraghabishi kuibua masuala ya
wanajamii na kujenga uwezo wa wanajamii kuhoji na kudai uwajibikaji. Hapana
shaka kwamba mpango huu wa utafiti shirikishi na uraghabishi ndio unafaa kabisa
kubainisha chanzo cha vurugu za Mtwara. Mpango huu unamruhusu kila mshiriki kuzungumza
bila kuogopa na kwa njia hii ya uraghabishi, watu wanajifunua na kujiweka wazi.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58258" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58268" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58267" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58260" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
<div class="yiv2907073951MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58262" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_58265" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">www.karugendo.net</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-65675431635959529792013-12-10T00:27:00.001-08:002013-12-10T00:27:10.198-08:00Nani anajali?<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57323" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57322" lang="SW" style="font-size: 16.0pt;">MTOTO WA AFRIKA, NI NANI
ANAJALI?</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57325" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57328" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57327" lang="SW" style="font-size: 16.0pt;">Kauri mbi ya siku ya
mtoto wa Afrika mwaka huu inasema: “Kuondoa Mila zenye kuleta madhara kwa
watoto: Ni jukumu letu sote”. </span><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57335" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tarehe 16.6.2013, kama kawaida ilikuwa ni siku ya Mtoto
wa Afrika .Baadhi ya watu wameikumbuka, lakini inaelekea moto wake unaendelea
kupunguka na kubakia ni siku ya watoto wa shule, kukutana na kuimba nyimbo,
kucheza ngoma na maigizo. Watu wazima wanaanza kuikwepa siku hii. Jana kwenye
taarifa za habari ilionekana asilimia kubwa ya watoto na asilimia ndogo sana ya
watu wazima. Pamoja na jitihada za kuikwepa siku hii ukweli unabaki pale pale
kwamba yaliyotokea Soweto miaka hiyo yanaweza kutokea tena popote kwenye nchi
hizi za Kiafrika na Tanzania ikiwemo. Matendo ya ukiukwaji wa haki za watoto
ikiwemo na uporaji wa ardhi yamekuwa mengi. Binafsi nimejenga utamaduni wa
kuandika makala kila tunapoikumbuka siku hii ya mtoto wa Afrika. Ninaamini
mchago wangu huu unaweza usiwanufaishe watanzania wa leo, lakini kama wasemavyo
kwama “Kilichoandikwa kimeandikwa” ni imani yangu kwamba mchango wangu
utawanufaisha hata watanzania wa kesho. Na ndiyo maana nimeamua kuuliza katika
makala haya: Mtoto wa Afrika, ni nani anajali?</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57341" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57340" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kauri mbiu ya mwaka huu ni mwiba mkubwa kwetu
sote. Tuna mfumo gani wa kuondoa mila zenye kuleta madhara kwa watoto wetu?
Tuna mfumo gani wa kutokomeza uporaji wa ardhi, tuna mfumo gani wa kuwaambukiza
watoto wetu moyo wa uwajibikaji na uzalendo? Tuna mfumo gani wa kujenga mila
zenye ustaarabu na kuachana na mila za kishenzi kama zile zinazoanza kujitokeza
katika jamii yetu: Watu wanapigwa wanaumizwa na wengine wanauwa, watu wanasingiziwa
na kubambikiziwa kesi; wanaotenda matendo haya ya kinyama bado wanaendelea
kudunda na kupandishwa vyeo. Tuna mfumo gani wa kuwafundisha watoto wetu kusema
ukweli? Kuwa waaminifu, kuacha uchakachuaji, kuacha tabia ya kuuza bidhaa
bandia. Tuna mfumo gani wa kufundisha uadilifu? Elimu mbovu ni kujenga mila
zenye kuleta maafa! Tumeshuhudia watoto wetu wakishindwa vibaya, tumeshuhudia
watoto wetu wakifundishwa kwa kutumia vitabu bandia ambavyo havina viwango:
Alimu mbovu ni maafa matupu!</span><span lang="SW" style="font-size: 16.0pt;"></span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57343" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57346" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57345" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mnamo mwaka 1976, Kule Soweto, Afrika ya kusini,
maelfu ya watoto weusi wa shule waliingia mitaani na kufanya maandamano ya
zaidi ya nusu kilomita, wakipinga elimu duni waliyokuwa wakiipata na kudai kufundishwa
kwa lugha yao. Walifanya maandamano ya amani kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa
serikali ya makaburu. Ujumbe huu ulikuwa mchungu kwa wakubwa na hawakuwa tayari
kuusikiliza. Kama kichaa anavyoweza kutumia bunduki kuua mbu, ndivyo makaburu
walivyofanya kwa wanafunzi hao. Mamia ya wasichana na wavulana walipigwa risasi
na kupoteza maisha yao.<span> </span>Kwa vile bunduki
inaua mwili, lakini fikra na roho vinaendelea kuishi, maandamano hayo
hayakuzimwa kwa risasi! Machafuko yaliyofuatia tukio hili yalipoteza maisha ya
mamia ya watu na kuacha majeruhi kadhaa.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57349" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57352" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57351" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoshuhudia
matatizo mengi ya watoto. Tunashuhudia watoto wetu wanavyosukumwa kila siku
kwenye daladala, watoto wanavyosoma kwa shida, shule za msingi wengine wanakaa
chini, sekondari wanasoma bila kuwa na walimu wa kutosha, matokeo yake<span> </span>wanafanya vibaya na kushindwa kuendelea na
masomo ya juu. Lakini pia na wale wanaofanikiwa kuendelea na masomo ya juu,
tunashuhudia wanavyonyanyaswa na Bodi ya mikopo. Tunashuhudia watoto wetu wakikoswa
ajira, tunashuhudia watoto wetu wakibugia dawa ya kulevya, wakilewa pombe,
wavulana wakisuka nywele na kujifananisha na wasichana, wasichana wakitembea
nusu uchi na baadhi ya watoto wetu wakiikimbia nchi kwenda kuishi
ughaibuni.<span> </span>Kwa asilimia kubwa maisha ya
mtoto wa Kitanzania, yanakuwa ni ya shida.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 16.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57356" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57355" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Binafsi, nimeamua mwaka huu niandike juu ya Mtoto wa
Afrika<span> </span>na uporaji wa ardhi na mtoto wa
na elimu mbovu. Kwanini, nimeamua kuandika hivyo: chanzo cha siku ya mtoto wa
Afrika, ni maasi yaliyofanywa na watoto wa Soweto, kwa kukataa kunyanyaswa.
Walikuwa wakipata elimu duni ukilinganisha na ile ya Wazungu. Pia, walitaka
elimu inayotolewa kwa lugha yao. Kule Soweto, watoto walianza kutambua kwamba
wale waliokuwa wakifundishwa katika shule nzuri ndio waliokuwa wakipata kazi nzuri
na vyeo vya juu katika serikali. Hali ya kutamani hali bora ya maisha kwa siku
za mbele, hali ya kutaka kuwa na vyeo na nafasi nzuri za kazi, iliwafanya
wanafunzi kukataa elimu duni waliyokuwa wakiipata. Hawakuogopa nguvu za jeshi
la Makaburu. Walikuwa tayari kupambana bila silaha – na kweli wengi wao
walipoteza maisha. Watoto wa Soweto, walitambua kwamba kujifunza kwa lugha za
kigeni wasingepata maarifa yenyewe. Walitaka wafundishwe kwa lugha ya kwao,
lugha inayofanana mazingira yao, lugha inayogusa maisha halisi, lugha inayoweza
kuharakisha maendeleo. Hoja yangu ni kwamba Bila kuwa waangalifu, inawezekana
na sisi hapa Tanzania, tunaandaa Tanzania ya kesho yenye maasi kama ya Soweto.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57360" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57359" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Bila kuwa na elimu nzuri na bora, watoto wetu
wakasoma na kupevuka kifikra6/15/2013, tutakuwa tunajiandalia majanga ya Soweto;
bila kuwa na ardhi ya kuwarithisha watoto wetu tunakuwa tunaliandalia taifa
letu migogoro na majanga ya Soweto.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57363" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57362" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kumetokea wimbi la uporaji wa ardhi. Watu wenye
fedha wananunua ardhi kubwa kwa kisingizio cha kuwekeza. Matokeo yake vijana
wengi watajikuta hawana ardhi na wataikataa hali hii. Na tunavyosikia kwenye
vyombo vya habari sehemu nyingine hali hii imekataliwa mapema. Tunasikia kule
Manyara jinsi watu wanavyovamia mashamba, kukata mazao na kuwashambulia wanao
miliki mashamba. Tukio la Tegeta, la kukatana mapanga katika harakati za vijana
kufukuzia mbali waporaji wa ardhi, ni la kusikitisha na kutafakarisha; na ni
fundisho pia kwamba vijana wakiamua kudai ardhi yao, patachimbika.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57365" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57368" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57367" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mgogoro wa ardhi wa Loliondo, tumeshuhudia jinsi
ulivyovuruga amani kwenye maeneo hayo na kupanda mbegu ya maasi na chuki kwa
vizazi vijavyo. Mashirika mbali mbali yasiyokuwa kiserikali yamepiga kelele juu
ya suala hili la uporaji wa ardhi, lakini kelele hizi zimekuwa kama ile sauti
iliayo nyikani. Mashirika haya yamekuwa yakijitahidi kutengeneza majukwaa ya
majadiliano, ili watanzania tukae pamoja na kujadiliana juu ya uhai wa taifa
letu. </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57371" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57370" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ardhi ni muhimu sana kwa maisha yetu ya leo na
vizazi vijavyo; uchumi wetu unategemea kilimo; bila ardhi hatuwezi kulima,
hatuwezi kupata chakula na mazao ya kuuza na kujipatia fedha za kigeni. Hivyo
ni muhimu sote kusimama pamoja kupinga wimbi hili kubwa la kupora ardhi yetu.
Tuhakikishe kila Mtanzania ana ardhi yake ya kutosha na kupiga vita kwa nguvu
zote ardhi kuwa mikononi mwa watu wachache.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57373" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57376" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57375" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tunapoikumbuka siku mtoto wa Afrika, ni bora
tukazingatia umuhimu wa ardhi kuwa ustawi wa mtoto wa Afrika. Tukiilinda ardhi
yetu leo, tunaepusha machafuko ya ardhi kesho na keshokutwa. <span> </span>Pia tunapoikumbuka siku ya<span> </span>mtoto wa Afrika ni muhimu sana kutambua elimu<span> </span>bora kwa watoto wetu italiepusha taifa letu
na wimbi kubwa la machafuko. Hivyo basi, Mtoto wa Afrika, ni nani anajali? Ni
mimi? Ni wewe, ni yeye? Ni wao au ni sisi sote! Mungu ibariki Tanzania, Mungu
wabariki watoto wote wa Afrika.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57395" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57379" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri<span>
</span>Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57381" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
<div class="yiv5558166607MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_57393" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><a href="http://www.karugendo.net/" rel="nofollow" target="_blank">www.karugendo.net</a></span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-69476504723858039312013-12-10T00:24:00.003-08:002013-12-10T00:24:21.976-08:00Tujifunze kutoka kwa Mandela<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:WordDocument>
<w:View>Normal</w:View>
<w:Zoom>0</w:Zoom>
<w:TrackMoves/>
<w:TrackFormatting/>
<w:PunctuationKerning/>
<w:ValidateAgainstSchemas/>
<w:SaveIfXMLInvalid>false</w:SaveIfXMLInvalid>
<w:IgnoreMixedContent>false</w:IgnoreMixedContent>
<w:AlwaysShowPlaceholderText>false</w:AlwaysShowPlaceholderText>
<w:DoNotPromoteQF/>
<w:LidThemeOther>EN-US</w:LidThemeOther>
<w:LidThemeAsian>X-NONE</w:LidThemeAsian>
<w:LidThemeComplexScript>X-NONE</w:LidThemeComplexScript>
<w:Compatibility>
<w:BreakWrappedTables/>
<w:SnapToGridInCell/>
<w:WrapTextWithPunct/>
<w:UseAsianBreakRules/>
<w:DontGrowAutofit/>
<w:SplitPgBreakAndParaMark/>
<w:DontVertAlignCellWithSp/>
<w:DontBreakConstrainedForcedTables/>
<w:DontVertAlignInTxbx/>
<w:Word11KerningPairs/>
<w:CachedColBalance/>
</w:Compatibility>
<m:mathPr>
<m:mathFont m:val="Cambria Math"/>
<m:brkBin m:val="before"/>
<m:brkBinSub m:val="--"/>
<m:smallFrac m:val="off"/>
<m:dispDef/>
<m:lMargin m:val="0"/>
<m:rMargin m:val="0"/>
<m:defJc m:val="centerGroup"/>
<m:wrapIndent m:val="1440"/>
<m:intLim m:val="subSup"/>
<m:naryLim m:val="undOvr"/>
</m:mathPr></w:WordDocument>
</xml><![endif]--><br />
<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:LatentStyles DefLockedState="false" DefUnhideWhenUsed="true"
DefSemiHidden="true" DefQFormat="false" DefPriority="99"
LatentStyleCount="267">
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Normal"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="heading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="35" QFormat="true" Name="caption"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="10" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" Name="Default Paragraph Font"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="11" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtitle"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="22" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Strong"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="20" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="59" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Table Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Placeholder Text"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="No Spacing"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Revision"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="34" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="List Paragraph"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="29" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="30" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="19" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="21" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="31" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="32" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="33" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Book Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="37" Name="Bibliography"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" QFormat="true" Name="TOC Heading"/>
</w:LatentStyles>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 10]>
<style>
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:"Table Normal";
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:"";
mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;
mso-para-margin-top:0in;
mso-para-margin-right:0in;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0in;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:"Calibri","sans-serif";
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-font-family:"Times New Roman";
mso-fareast-theme-font:minor-fareast;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-bidi-font-family:"Times New Roman";
mso-bidi-theme-font:minor-bidi;}
</style>
<![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapedefaults v:ext="edit" spidmax="1026"/>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapelayout v:ext="edit">
<o:idmap v:ext="edit" data="1"/>
</o:shapelayout></xml><![endif]-->
<br />
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<b style="mso-bidi-font-weight: normal;"><u><span style="font-size: 14.0pt;">TUJIFUNZE KUTOKA KWA MZEE MANDELA</span></u></b></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Wakati
dunia nzima inaendelea kumwombea Mzee Mandela, apate afya njema na kupona
ugonjwa uliomlaza kitandani zaidi ya majuma mawili sasa, ni lazima watanzania tujifunze
kutoka kwake. Mzee Nelson Mandela, ni kati ya watu wachache waliofanikiwa
kuyaishi na kuyashika mafundisho magumu. Mafundisho ambayo waliowengi tunayaita
ndoto, lakini tunayafundisha na kuwahimiza watu wengine wayashike na
kuyafuata.Alipohukumiwa kifungo cha maisha,Mzee Mandela, alipokea hukumu hiyo
bila ya woga, ni kitu alichokifahamu hata kabla ya kuanza mapambano na serikali
ya makaburu. Alifahamu nguvu na uwezo wa serikali ya makaburu. Alijua
walivyokuwa wameshikilia vyombo vya dola na silaha nzito nzito, alijua
angekamatwa na kufungwa au kuuawa.Pamoja na kuyajua yote hayo aliamua kuendelea
kupambana na makaburu kwa vile alitanguliza uhai wa taifa lake na wala si uhai
wa maisha yake binafsi. Lakini pia alijua jinsi nguvu na uwezo wa makaburu vilivyokuwa
vinaishia kwenye kuutesa mwili wake bila ya kuwa na uwezo wa kuigusa roho yake
hata hivyo mafundisho magumu ambayo roho yake haikuwa na uwezo wa kuyakwepa
yalikuwa mbele ya macho yake:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span><b style="mso-bidi-font-weight: normal;"><i style="mso-bidi-font-style: normal;">“ Msiwaogope wale wauao mwili lakini
hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili
pamoja na roho..”</i></b> (Matayo 5:28).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Makaburu
waliutesa mwili wa mzee Mandela, alifanyishwa kazi za
suluba,alidhalilishwa,alipokonywa uhuru wake,alinyimwa uhuru wa kuwa na familia
yake,alinyimwa uhuru wa mawasiliano, alipofiwa na mtoto wake wa kiume,
alinyimwa ruhusa ya kuhudhuria mazishi yake. Unyama wote aliofanyiwa akiwa
gerezani uliugusa na kuutesa kwa kiasi kikubwa mwili wake tu,lakini roho yake
ilibaki madhubuti. Alipochaguliwa kuwa Rais wa kwanza mwafrika wa Afrika ya
kusini huru, Mandela, alimshangaza kila mtu pale alipowakumbatia adui zake na
kukaa nao meza moja ya chakula. Hakulipiza kisasi! Unyama aliotendewa
gerezani,haukuigusa roho yake! Mzee Mandela, amekuwa mwalimu wa kuwafundisha
watu kuishi na kuyashika mafundisho magumu, mambo ambayo tumezoea kuyaita
ndoto.Watanzania tuna utamaduni wa kuogopa mwenye nguvu na uwezo wa kuua
mwili.Pia tuna utamaduni wa kulipa kisasi, wawe ni viongozi wa dini au viongozi
wa serikali,tabia hii ipo. Tujifunze kwa Mzee Mandela: Mwili unateswa,
unanyanyaswa na kudhalilishwa na mwanadamu, lakini roho ya ukweli, amani na
wema viko juu ya uwezo wa mwandamu! Hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kuiua roho
ya wema, hata kama mtu huyo angekuwa na nguvu za kidunia kama za Amerika!Pia
tujifunze kwamba ukipambana na mtu, ukimshinda, mnashikana mikono na
kukumbatiana – si kujenga chuki wala uhasama!</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Watu wanaouona mwanga huu wameanza kugundua
kwamba yale tunayoita mafundisho magumu na ndoto yanawezekana, Mzee Mandela,
ametuonyesha mfano: </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">“ <b style="mso-bidi-font-weight: normal;"><i style="mso-bidi-font-style: normal;">Mmesikia
kwamba ilisemwa: ‘Jicho kwa jicho, jino kwa jino’. Lakini mimi nawaambieni,
usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia
shavu la pili..”</i></b> (Matayo 5:38-39).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Haya ni mafundisho magumu ambayo yamewashinda
watu wengi hata na wale walioyafundisha na kuyaeneza. Hadi leo hii hata
viongozi wa dini bado mafundisho haya yanawapatia shida. Bado wanashikilia
‘Jicho kwa jicho, na jino kwa jino’. Migogoro inayowakumba viongozi<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>wa dini inasababishwa na kutokubali kupigwa
shavu la kulia, na kugeuza la kushoto. Wakipigwa kofi, wanarudisha. Hii
inavuruga amani na kuleta magomvi yasiyoisha. Mandela, hakurudisha kofi!
Alisamehe! Mafundisho magumu yalikuwa mbele ya macho yake na roho yake
iliyoandaliwa kwa umakini na kwa miaka mingi haikuwa na uwezo wa kuyakwepa: </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">“<b style="mso-bidi-font-weight: normal;"><i style="mso-bidi-font-style: normal;">Mmesikia
kwama ilisemwa:<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>‘Utampenda jirani yako,
lakini utamchukukia adui yako.’ Lakini mimi nawaambieni,wapendeni maadui wenu
na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi…”</i></b> ( Matayo<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>5:43-44).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Tunakumbuka
jinsi Mzee Mandela, alivyowashauri wamarekani:<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>“Tumejifunza jinsi ya kuishi na maadui zetu, nanyinyi mjifunze kuishi na
maadui zenu..”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Tume
ya maridhiano ya Afrika ya Kusini, ilifanya kazi kwa uhuru na kumsikiliza kila
mtu. Haikuwa na upendeleo wala kukikumbatia chama tawala. Haki ilitendeka kwa
kila mwanachi na watu wote walifurahia kazi yake.Hizo zilikuwa mbinu za Mzee
Mandela, za kukumbatia mafundisho magumu ya kumpenda adui.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Mzee Mandela, alipompoteza mtoto wake wa kiume
kwa ugonjwa wa UKIMWI, kwa masikitiko makubwa(maana huyu ndo mtoto pekee wa
kiume aliyekuwa amebakia) alitangaza wazi mbele ya vyombo vya habari bila aibu
kwamba mtoto wake alikufa kutokana na ugonjwa wa UKIMWI. Hapa pia mafundisho
magumu ambayo roho yake haikuwa na uwezo wa kuyakwepa yalikuwa mbele ya macho
yake: </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">“ <b style="mso-bidi-font-weight: normal;"><i style="mso-bidi-font-style: normal;">Jihadharini
na chachu ya Wafarisayo, yaani <u>unafiki</u>. Kila kilichofunikwa
kitafunuliwa, na kila <u>siri </u>itajulikana. Kwa hiyo, kila mlichosema
gizani, watu watakisikia katika mwanga, na kila mlichonong’ona,
faraghani,milango imefungwa,kitatangazwa juu ya nyumba.”</i></b> (Luka 12:1-3).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Hili
limekuwa fundisho jingine kutoka kwa Mzee Mandela, la mafundisho magumu ambayo
wengi wetu na hasa Barani Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara, tumekuwa
tukidhani ni ndoto. Tumezoea kusikia watu mashuhuri wakifa kutokana na
shinikizo la damu,kisukari, ugonjwa wa muda mrefu na ugonjwa wa ghafla nk. Ni
nadra kusikia mtu mashuhuri amekufa kwa UKIMWI. Ugonjwa huu, umezungukwa na
unafiki mkubwa.Ndo maana ugonjwa huu umekuwa wa hatari katika nchi zetu hizi
masikini. Ugonjwa unafichwa na unafiki unaendelea kutawala.Hawa watu mashuhuri
wanaokufa kwa shinikizo la damu wanatoa mwanya wa wenzi wao kuendelea kusambaza
virusi vya UKIMWI, hakuna anayeshughulika kuchukua tahadhari maana shinikizo la
damu si ugonjwa wa kutisha kama UKIMWI!! Matokeo yake ni janga kama
tunavyoendelea kushuhudia. Ni lazima tumpongeze Mzee Mandela, kwa ujasiri wake
na tuendee kujifunza kutoka kwake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Mzee
Mandela, alipougua ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo, alitangaza wazi.
Hakuficha ugonjwa wake.Alipatiwa matibabu, na sasa anaendelea kuishi! Hapa
Tanzania, tumewapoteza watu wengi kwa ugonjwa huu kwasababu ya aibu na unafiki!
Pia watu wanakufa kwa kuficha magonjwa ya zinaa yanayotibika kwasababu ya aibu
na unafiki. Magonjwa yakigusa sehemu za siri, watu wanakuwa na aibu.Aibu hii
inatokana na mawazo ya kulichukulia tendo la ngono kama la aibu. Ingawa kuna
ukweli kwamba si magonjwa yote yanayozishambulia sehemu za siri yanasababishwa
na tendo la ngono. Baadhi ya watu wakiugua sehemu za siri, wanataja
kichwa,tumbo na mgongo. Madaktari wanatibu kichwa,tumbo na mgongo, kumbe mgojwa
ana saratani ya kibofu cha mkojo au magonjwa mengine ya zinaa. Inapotokea
bahati ya kuugundua ugonjwa,mgonjwa anakuwa amezidiwa na kufa! Aibu na unafiki
vinasababisha vifo visivyokuwa vya lazima katika taifa letu na katika nchi
nyingine za Kiafrika.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="tab-stops: 307.5pt; text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;"><span style="mso-tab-count: 1;"> </span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Lengo
la makala hii ni kuonyesha jinsi tulivyo na mambo mengi ya kujifunza kutoka kwa
Mzee Mandela. Bahati mbaya viongozi wetu wa dini na serikali ni woga.
Hatujapata viongozi wa kuyashika na kuyaiishi mafundisho magumu kama
alivyofanya Mzee Mandela. Hatujapata viongozi wasiogopa macho na masikio ya
watu, viongozi wasiojali kudhalilishwa na ikibidi kuupoteza uhai wao katika
harakati za kutetea ukweli na kupingana na unafiki.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Tunapojifunza
kutoka kwa Mzee Mandela, ni lazima tumwangalie yeye na historia yake. Si kwamba
misimamo yake hii ya kuishi na kuyashika mafundisho magumu, ilimnyeshea kama
mvua. Ni mtu aliyefanya<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>maandalizi, ni
mtu aliyeitafuta elimu akiwa na malengo katika maisha yake – hakusoma tu kwa
vile kusoma ni lazima – hakusoma kuishinda maitihani, bali alisoma kwa vile
alikuwa na lengo la kuikomboa nchi yake. Lengo hili lilijaa kwenye roho </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">yake.
Hata ungeupiga na kuumiza mwili wake, usingeliligusa lengo lililokuwa kwenye
roho yake.Alijiandaa kwa maamuzi magumu –alijua jinsi njia ya kulifikia lengo
lake ni kupitia kwenye maamuzi magumu. Alijifunza na kujiandaa kulitanguliza
taifa lake kwa kila kitu. Hakuaangalia tumbo lake,cheo chake au biashara yake
(mambo ya mwili) aliangalia uhai wa taifa zima(mambo ya kiroho) . Mungu
amsaidie, hata uhai wake ukiondoka, tutaendelea kuishi na roho yake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-88965168466194986342013-12-10T00:22:00.002-08:002013-12-10T00:22:24.064-08:00GAIDI NI NANI?
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53325" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53327" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53325" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53327" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">SWALI LANGU KWA RAIS OBAMA: GAIDI NI NANI?</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53330" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53329" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53330" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53329" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Juzi nilikutana na mtu wa kawaida kwenye mitaa, akaniambia yeye
hafurahishwi na ujio wa Baraka Obama, maana rais huyu anakuja Tanzania
kufuatilia maslahi ya Amerika. Na mwingine akaniambia Raisi Obama, anafuatilia
nyendo za China, na kasi kubwa ya China kushirikiana na nchi zinazoendelea. Kuna
wengine walioniambia kwamba Obama, ataleta neema kubwa Tanzania. Kila mtu ana
mawazo yake juu ya ujio wa Obama Tanzania. Kule Afrika ya kusini, tumeshuhudia
wanafunzi wakiandamana kwa mabango kupinga ujio wa Rais Baraka Obama, kwenye
nchi yao. Tunaweza kusema ujio wa Obama katika nchi za Afrika, utapokelewa kwa
hisia tofauti. Pamoja na ukweli kwamba Obama ni mwana wa Afrika, bado kuna
ukweli kwamba yeye kama Rais Amerika, ujio wake ni nguvu za Amerika na sera za
Amerika. Na tujuavyo Amerika iko mstari wa mbele kupambana na ugaidi
unaofafanuliwa kwa misamiati ya kimarekani.</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53336" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53335" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ningepata bahati ya kukutana Rais Obama, bahati ambayo ni ndoto za mchana, ningemuuliza
swali langu moja: Gaidi ni nani? Sina lengo la kuutetea ugaidi kwenye makala
hii, ninajua ugaidi ni mbaya, unawagusa waliomo na wasiokuwemo; usumbufu wa
kusafiri nchi za nje unatugusa sote, mtu ukipanda ndege unakuwa na wasi wasi,
ukiwa kwenye majengo makubwa na kwenye mkusanyiko wa watu roho haitulii! –
hakuna aliye salama mbele ya ugaidi na hasa ugaidi huu wa kulipua ndege na
majengo. Ninachofanya kwenye makala hii ni kuwataka wasomaji wangu
tutafakari juu ya Ugaidi. Ukienda Afghanistan na Iraq, watu watakwambia gaidi
ni Osama au ni Wamarekani? Wakati Afrika ya Kusini ikipigania uhuru wake,
Mandela, alikuwa ni gaidi namba moja. Hata kule Kenya wakati wa huru,
wapiganaji wa Mau Mau, walijulikana kama Magaidi. Hivyo kila mtu anaweza kuwa
gaidi kutegemeana na nyakati na mapambano yaliyopo. Ndo maana ningetamani sana
kusikia Mheshimiwa rais Obama, ana jibu gani kuhusu gaidi! Yeye kwa maoni yake
gaidi ni nani?</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53340" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53339" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kuiingilia nchi huru kijeshi kama Amerika ilivyofanya kule Pakistan katika
harakati za kumwangamiza Osama, ni ugaidi au ni kitendo chenye baraka zote kwa
vile ninalenga kuyalinda maisha ya watu wenye thamani kubwa hapa duniani?
Kitendo hicho kingefanywa na nchi nyingine kingelaaniwa kwa nguvu zote. Kwa
vile kimefanywa na kiranja wa dunia, sote tunafyata mkia na kushangilia.</span><span lang="SW"></span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53343" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53342" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Je ugaidi ni njia mojawapo wa wanyonge kutetea haki zao? Ugaidi ni njia
mojawapo ya kupigania uhuru na haki ya kujitawala? Mwenye nguvu kubwa kama
ilivyo Amerika njia pekee ya kupambana naye ni ugaidi? Inawezekana Osama,
alikuwa akiwatetea wanyonge? Bila kutaka kuingia sana kwenye mjadala wa ugaidi
na ugaidi ni nini, niendeleze swali langu kwa Raisi Obama. Gaidi ni nani?: Je
kifo cha Osama kitamaliza ugaidi duniani? Kwamba baada ya yeye kufa hatusikii
tenda vitendo vya kigaidi? Bila kuwa na dunia yenye haki na usawa; dunia ambayo
kila mtu anaruhusiwa kuishi na kuheshimiwa; dunia ambayo binadamu wote
tunatumia rasilimali kwa usawa; dunia ambayo haina ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa
dini ugaidi utakwisha?</span><span lang="SW"></span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53346" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53345" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa Amerika Osama, alikuwa gaidi na kwa watetezi wa haki za Waislamu, Osama
alikuwa shujaa na mtetezi wa wanyonge. Wakati Wamarekani wanashangilia kifo cha
Osama; kinyume kabisa na utaratibu wa maisha ya mwanadamu, maana tumefundishwa
kupenda adui na kutoushangilia msiba wa mwenzio, Pakistan maandamano
yanaendelea kupinga mauaji wa Osama. Maana yake ni kwamba uelewa wa Ugaidi kwa Wamarekani,
ni tofauti kabisa na uelewa wa ugaidi kwa watu wa Pakistan na nchi nyingine
ambazo bado ziko kwenye harakati ya kujikomboa kiuchumi na kupiga hatua ya
maendeleo.</span><span lang="SW"></span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53349" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53348" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Dunia nzima inapigana na ugaidi. Inataka kutokomeza
ugaidi. Kusema kweli hata na mimi ugaidi siupendi kabisa. Ugaidi unawaingiza
waliomo na wasiokuwemo, unapoteza maisha ya watoto wadogo na watu wema na
wapenda amani. <span> </span>Hatuwezi kufanikiwa
kupambana na ugaidi kama hatukubali kufutilia mbali mawazo potofu kwamba kuna
binadamu bora kuliko wengine. Kama hatukubali kufuta mawazo kama ya le ya
Hitler, kwamba kuna kitu kama “Royal Blood”. Watoto wa Gaza, wanaoshuhudia
unyama wa leo unaofanywa na Waisraeli, hawezi kulifuta hili akilini mwao mpaka
pale watakapokuwa na kushika bunduki au kuvaa mabomu na kwenda kulipiza kisasi
kwa kujilipua.</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53352" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53351" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Obam, alipoitembelea Israeli, alisema hata yeye
hawezi kumvumilia mtu anayerusha makombora kuelekea walikolala mabinti zake
wawili. Hivyo hivyo hakuna mtu yeyote duniani anayeweza kuvumilia kuona maisha
ya watoto wake yakiteketea. Hata Wapalestina hawawezi kuvumilia hilo. Hakuna
mtu anayeweza kuvumilia hilo; kama hana nguvu za kutosho atajaribu kutumia
mbinu zozote zile kuyalinda maisha ya watoto wake, maisha yake binafsi na
maisha ya watu wengine wanaomzunguka. Inawezekana mbinu hizi zikawa na sura ya
ugaidi, lakini kwa vyovyote haziwezi <span> </span>kuwa na tofauti kubwa na yule anayetumia nguvu
za kijeshi kuyalinda maisha ya mtoto wake au watu wake.</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal">
<span lang="SW"> </span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNoSpacing" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53355" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53354" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Waisraeli, wanasema wanawalinda
watu wao. Kama wao wana haki ya kufanya hivyo, kwa nini na Wapalestina wasiwe
na haki ya kuwalinda watu wao. Rais wa Amerika, Mheshimiwa Barack Obama,
anasema Amerika, itashirikiana na kila mpenda Amani. Ni imani yangu kwamba
dunia nzima inapenda Amani. La msingi ni kuhakikisha kwamba tunayatumia yote
tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu kwa usawa. Tunaitutumia ardhi kwa usawa na
kuyalinda mazingira kwa pamoja, tunatumia chakula kwa usawa na kuhakikisha
kwamba hakuna anayekufa kwa njaa, vinginevyo njaa inaweza kuvunja amani,
wanaokufa kwa njaa wanaweza kushawishika kuchukua silaha ili kupambana na wenye
chakula kingi. Tutumie maji kwa usawa, vinginevyo vita mbaya inayoweza kutokea
huko mbele ni kugombania maji. Hadi leo hii kuna sehemu hapa duniani ambako
maji yanavunja amani. Kwa ufupi ni kwamba tutumie rasilmali za dunia hii kwa
usawa. Maana yake ni kwamba, Obama, asishughulike tu na usalama wa Amerika,
bali atafute chanzo cha <span> </span>yale yanayoweza
kuvunja usalama si wa Amerika peke yake bali wa dunia nzima. Dunia ikiendelea
kugawanyika kwenye makundi ya walionacho na wasiokuwa nacho, wenye madaraka
makubwa na wanyonge, wenye damu safi na wenye damu chafu, wenye dini bora na
wenye dini duni, wenye rangi bora ya ngozi na wenye rangi duni, wenye haki na
wasiokuwa na haki, itakuwa ni ndoto kujenga Dunia yenye amani. Kama Obama,
anasimamia mabadiliko, kama kauli mbiu yake katika kampeni na katika utawala
wake – ni lazima ahakikishe mabadiliko ya kweli yanakuja si Amerika peke yake,
bali dunia nzima. Mwenyezi Mungu, alituumba tufaidi kila kilicho hapa duniani
kwa usawa!</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53366" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53364" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv7464778318MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_53362" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-7784145984981529292013-12-10T00:19:00.003-08:002013-12-10T00:19:48.762-08:00NDOA YANGU NINGEJUA<div class="yiv1151445140MsoBodyText" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50122" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50121" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">UHAKIKI WA KITABU:<span> </span>NDOA YANGU “NINGEJUA.....!”</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50125" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50129" style="margin-left: .5in; text-align: justify;">
<b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><span>1.<span style="font: 7.0pt;">
</span></span></span></b><b id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50128"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50127" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Rekodi za Kibibliografia.</span></b></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50132" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50135" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50134" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Jina la kitabu
kinachohahikiwa hapa ni NDOA YANGU ‘Ningejua...!’, Kimeandikwa na Charles B
Misango. Kitabu hiki kina namba ifuatayo katika sekwensia ya vitabu duniani
(ISBN): 9987 433 022. Kitabu kina kurasa 109 . Na anayekihakiki sasa hivi
katika safu hii ni mimi Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50137" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50139" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">II. <b>Utanguliz</b>i</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50141" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50144" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50143" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kinaitwa
Ndoa Yangu Ningejua...!<span> </span>Haina maana
kwamba mwandishi anaandika juu ya ndoa yake, bali kwa vile ameamua kuandika juu
ya ndoa anataka kila mtu aichunguze ndoa yake na yeye akiwemo. Kwa maoni ya
mwandishi kama angeandika “Ndoa yako” au “Ndoa zenu” ingekuwa sawa na
kuwanyoshea wengine kidole kana kwamba ndoa yake haina changamoto zozote zile.
Ni Ndoa yangu... tunaiboresha vipi? Au tuseme: Ndoa yangu, Ningejua....<span> </span>ningeiboresha au ningefanya chaguo zuri? Au
ningezingatia maadili na busara ya kuiongoza ndoa; kuwaunganisha watu wawili ni
kazi kubwa ambayo bila uvumilivu na kuchukuliana ni muungano wenye mashaka!</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50146" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50149" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50148" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Lengo kubwa la mwandishi
ni kumwalika kila mwenye ndoa kuichunguza ndoa yake na kutafakari kwa kulinganisha
na yale anayoyaandika mwandishi katika kitabu hiki. Msukumo wa kuandika kitabu
hiki umetokana na ukweli kwamba siku za hivi karibu na hasa kwenye Jiji la Dar-es-Salaam,
ndoa nyingi zinafungwa na sherehe kubwa zinafanyika kwenye kumbi mbali mbali,
na jinsi ndoa nyingi zinavyofungwa kwa mbwe mbwe ndivyo ndoa hizo zinavyovunjika
na nyingine zinakuwa na changamoto, vurugu na migogoro nyingi baina ya familia
za bwana harusi na bibi harusi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50151" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50154" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50153" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa liko wapi? Kwa nini
hakuna amani kwenye ndoa?<span> </span>Tumekosea wapi
kama jamii? Haya ndiyo maswali ambayo mwandishi anajaribu kuyajibu baada ya
kufanya utafiti wake na kuwahoji watu mbali mbali wenye ndoa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50156" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50159" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50158" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi wa kitabu hiki
ambaye pia ameoa, maana kwenye shukrani anasema hivi: “ Shukrani za pekee
zimwendee MKE WANGU ambaye kwa maisha yake, amenisaidia pasipo yeye mwenyewe
kujua, jinsi maisha ya ndoa yanavyoweza kubadilika kutoka namna mmoja hadi
nyingine na njia ya kukabiliana nayo”. Kwa wengi mwandishi huyu anajulikana
kama MC Kibonge, ingawa ni mwembamba kwa maana ya neno hilo – labda kwa vile
mambo yake ni ya “Ubonge bonge” kama alivyoandika kitabu hiki juu ya ndoa. Huyu
ni mwandishi aliyebobea na kwa wale wanaosoma gazeti la Tanzania Daima watakuwa
wanakutana safu yake ya Nani anajali..., Alifanya kazi kwenye gazeti la
Kiongozi na sasa ni mmoja wa wahariri wa gazeti la kila siku<span> </span>la Tanzania Daima.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50161" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">III. <b>Mazingira
yanayokizunguka kitabu</b></span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50163" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50166" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50165" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nitafanya uhakiki wa
kitabu hiki, lakini kwanza kwa kudokeza mazingira yanayokizunguka kitabu hiki.
Mwandishi alifanya utafiti juu ya maisha ya ndoa na dodoso lake lilikuwa na
maswali kwa wenye ndoa, matokeo yake ndio yalimsukuma kuandika kitabu hiki.
Nina imani kama angekutana na majibu chanya, asingeweza kupoteza muda wake
kuandika kitabu hiki. Kwa ufupi tu, tutayaangalia baadhi ya maswali:</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Swali la kwanza kwa
wanawake: Kama ungejua Mumeo atakuwa na tabia alizonazo sasa ungekubali akuoe?
Jibu lilikuwa ni ama Ningekubali au Nisingekubali.<span> </span>Wanawake 93 kati ya 100 waliofunga ndoa ya
kanisa, walisema kuwa wasingekubali kuolewa. Watano walisema wangekubali,
wakati wawili waliobaki walisema kuolewa ama kutoolewa kwao yote sawa. Lakini
hata wale watano waliokubali walipotakiwa waseme msingi wa kukubali kwao,
baadhi ya majibu yao yalisitisha. Watatu kati yao walisema kuwa wanamshukuru
Mungu kwa kuwa waume zao wanawapenda na ni waaminifu na wa kweli kati ndoa zao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Swali hilo hilo
waliulizwa wanaume, na majibu hayakuwa tofauti sana, maana wanaume 79 kati ya
100 walihojiwa walisema wasingekubali kuwaoa wanawake hao kama wangefahamu
tabia zao, ni 12 tu ndio waliosema wangekubali kuwaoa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Swali la pili kwa
wanandoa lilikuwa: Je, Umeoa/kuolewa na Mtu uliyemtaka; Ni chaguo lako halisi.
Hapa jibu lilitakiwa Ndiyo au hapana. Ukweli uliojitokeza ni kwamba wengi
wamefunga ndoa na watu ambao hawakuwapenda kwa dhati. Wanaume 49 kati ya 100
yalisema walifunga ndoa na watu ambao hawakuwataka na wanawake 73 walisema
waliolewa na wanaume ambao hawakuwa chaguo lao. Kwa lugha nyingine ,ndoa 120
kati ya 200 zilifungwa pasipo hiari wala upendo wa dhati wa wanandoa wenyewe.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Utafiti huu umebaini
sababu nyingi za kuwalazimisha watu kuolewa bila upendo wa kweli, na sababu
hizo ni kama vile Kukosa uaminifu wakati uchumba, Kupata ujauzito bila
kutarajia na kulazimika kuolewa na huyo aliyekupatia ujauzito na wakati
mwingine kulazimishwa na wazazi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Matatizo katika ndoa yanasababisha
ndoa kuvunjika, lakini wakati mwingine ndoa inaendelea hivyo hivyo kwa
matatizo. Mtafiti alichunguza na hili pia kutaka kujua:<span> </span>Sababu gani zinakufanya Uendelee kuishi na
Mkeo/Mumeo hadi sasa? Ni watoto? Ni kwa vile ndoa ya kidini? Ni kuogopa laana
za wazazi? Ni kuvumilia, Ni upendo? Au ni kuishi kwa mazoea?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wanawake 9 katika ya 100
waliohojiwa walisema wanaishi kwenye ndoa hata kama ina matatizo kwa sababu ya
upendo kwa waume zao. Na 4 kati ya hao wanasema pamoja na ukatili wanaoupata
katika ndoa zao bado wanaendelea kuwapenda waume zao. Wanawake 86 katika 100
walihojiwa walisema wanaendelea kuishi kwenye ndoa kwa sababu ya watoto wao. Ni
wanawake 3 tu kati ya 100 walihojiwa waliosema wanaogopa laana ya wazazi wao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa upande wa wanaume ni
kwamba 16 kati ya 100 aliohojiwa walisema pamoja na matatizo kwenye ndoa
wanawapenda wake zao na wala hawajuti kuwaoa. Na wanaume 51 walisema ni kwa
vile ni ndoa ya kanisa ndio maana wanaendelea kuvumilia matatizo kwenye ndoa
zao na wanaume 24 walisema wanavumilia kwa sababu ya watoto. Waliobaki, ingawa
majibu hayakufanana sana, lakini maana halisi<span>
</span>ni kwamba kwao kuishi kwenye ndoa au kutokuwa na ndoa ni sawa sawa,
wanaishi kwa mazoea tu!</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Swali jingine la utafiti
lilikuwa: Nini chanzo kikubwa cha matatizo katika ndoa?<span> </span>Je ni kwa kutokuwa <span> </span>na kipato kizuri pande zote mbili? Au ni
wazazi wa pande zote mbili au ni mtu binafsi ndani ya ndoa yake au ni umasikini
na kumuasi Mungu?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wanawake 33 kati ya 100
walihojiwa walisema chanzo cha matatizo katika ndoa ni kipato kizuri cha waume
zao kinachowafanya wawe na “jeuri” ya kutumia fedha katika starehe na kuiacha
familia ikiteseka. Wanawake sita, walisema chanzo ni wazazi wao na 14 walisema
chanzo ni wakwe zao. Wanawake saba, walisema marafiki wao wa kike ndio
wanasababisha matatizo katika ndoa zao. Kwa bahati mbaya, hakuna mwanandoa
aliyekubali kwamba yeye binafsi amechangia kuleta matatizo katika ndoa yake,
kila mmoja anajaribu kutafuta mchawi nje ya ndoa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa upande wa wanaume,
13 kati ya 100 aliohojiwa walisema chanzo ni kipato kidogo, hii inasababisha
wanawake kuwadharau na vurugu inaanzia hapo. Na wanaume 14 walisema shinikizo
la wazazi na hasa mwanamke akichelewa kuzaa ndo chanzo cha vurugu. Katika
majibu yote hakuna mwanandoa aliyesema kuwa chanzo cha matatizo ni kuwa mbali
na Mungu. Wote wanafikiri wakienda kwenye ibada mara kwa mara wanakuwa karibu
na Mungu, hawaangalii ukaribu wa Mungu na maisha yao ya siku kwa siku kwenye
ndoa zao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Swali la kizushi, ni
kwamba kama talaka ingeruhusiwa mambo yangekuwa vipi? Kusema kweli asilimia 70,
wangeomba talaka na kuachana na ndoa zao. Na hili linaonyeshwa na ukweli kwamba
wanaume 78 katika ya 100 walihojiwa walikubali kuwa na mahusiano ya kingono nje
ya ndoa zao, na wanawake 62 pia walikubali kutembea nje ya ndoa zao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia kuna utata wa
watoto. Kwa vile siku hizi mtu anaweza kupima DNA, kuna mshangao mkubwa wa
kujitokeza; inasemekana kwamba asilimia kubwa ni watoto wa kubambikizwa;
wanaume wengi wamekuwa wakiwatunza watoto ambao si wao; ni watoto wa nje.
Lakini mtafiti alipoulizia wanaume kuwa na watoto nje ya ndoa asilimia 12,
walikubali kuwa na watoto nje ndoa. Na fumbo kubwa linabaki watoto wengi kuwa
na baba tofauti na wale wanaojulikana rasmi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mazingira
yanayokizunguka kitabu hiki ni utata katika ndoa, vurugu na magomvi hadi ndoa
kuvunjika. Ni kwamba ndoa nyingi hazina amani na hasa ndoa zinazofungwa siku za
hivi karibuni hazidumu. Tatizo liko wapi? Tufuatane na mwandishi wa kitabu
kuona majibu.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">IV. <b>Muhtasari wa
Kitabu</b></span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kina sura
sita, baada ya kutanguliwa na dibaji, shukrani na utangulizi. Dibaji ya kitabu
hiki imeandikwa na mheshimiwa Msgr. Padri Deogratias H. Mbiku wa jimbo katoliki
la Dar-es-Salaam. Ina maana hiki si kitabu cha mzaha, maana padri huyu ni
mgongwe katika Kanisa Katoliki, msomi na mtu anayeheshimika katika jamii.
Kukubali kuandika dibaji, ina maana alikisoma kitabu na kuona kinafaa kwenye
jamii yetu.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika dibaji, padri
Mbiku, anasema hivi: “ Katika nyanja za dini, jamii, Serikali na siasa, ndoa
ni<span> </span>muhimu sana; kwa sababu bila kuwa na
ndoa nzuri na imara, dini, jamii, Serikali na hata siasa zitalegalega na kukosa
maadili mema, haki na amani miongoni mwa watu...”. Juu ya mwandishi anasema “
Mwandishi wa kitabu hiki anazungumzia kwa undani na ufasaha sababu za kuvunjika
kwa ndoa: sababu za msingi ni ubinafsi, kukosa maandalizi ya kina; binadamu
wenzetu; na ibilisi... Lakini mwandishi haachii uchambuzi wake kwenye sababu
tu, bali pia anatoa ushauri na rai kuhusu nini kifanyike ili kuboresha ndoa.
Hatimaye, anaongelea wajibu wa Kanisa katika kuzishughulikia ndoa ili ziwe
msingi imara kwa jamii, dini, Serikali na hata siasa”</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Utangulizi, umeandikwa
na mwandishi mwenyewe. Hapa anajaribu kuelezea kwa undani juu ya kichwa cha
kitabu kuitwa “Ndoa yangu”. Hakutaka kusema ndoa yako au ndoa yenu, kwa maana
kwamba anapozungumzia maisha ya ndoa kwa vilele na yeye anayaishi maisha hao,
hawezi kujiweka kando. Lakini pia anaposema ndoa yangu haina maana kwamba
anaongelea ndoa yake mwenyewe. Anataka kila mtu atakapokuwa anakisoma kitabu
hicho, aseme “Ndoa yangu, ningejua...”</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kwanza ya kitabu
hiki ni Ningejua. Kwa kiasi kikubwa sura hii mwandishi anatoa mrejesho wa
utafiti alioufanya juu ya ndoa. Mrejesho wa jumla ni kwamba kati ya watu 200,
waliohojiwa, 170 wanajuta kufunga ndoa na wenzio, kama wangejua tabia zao
mapema, wangefanya uamuzi mwingine. Kadhalika 122 kati ya 200 waliohojiwa
wanakiri kufunga ndoa na watu ambao hawakuwapenda kwa dhati na hawakuwa changuo
lao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika sura hii ya
kwanza, kutokana na maswali ya dodoso: Kama ungejua mumeo atakuwa na tabia
alizonazo sasa ungekubali akuoe, Kama ungejua mkeo atakuwa na tabia alizo nazo
sasa, ungekubali kumuoa? Mmeo/Mkeo ni chaguo lako halisi? Tunaona kwamba
asilimia kubwa katika ndoa wanaangukia mikononi mwa watu ambao hawakuwatarajia.
Mwandishi anatoa<span> </span>asilimia kuonyesha
jambo hili. Na sababu kubwa zikiwa ni kulazimishwa na wazazi, kukosa uaminifu
wakati wa uchumba, kupata ujauzito kabla ya ndoa na mambo mengine kama kufuata
mali na cheo cha mtu.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pamoja na ndoa kuwa na
matatizo bado watu wanaendelea kuishi kwenye ndoa hizo. Asilimia kubwa ya
wanawake walihojiwa walisema wanavumilia magumu ya ndoa kwa sababu ya watoto.
Si upendo na wala si shinikizo la dini, bali nia watoto. Na asilimia kubwa ya
wanaume wanavumilia machungu ya ndoa kwa shinikizo la dini.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia kwenye utafiti huu,
mwandishi naweka wazi kwamba wanandoa wengi wanatembea nje ya ndoa na kuzaa
watoto nje ya ndoa zao. Asilimia kubwa wanalifanya suala la watoto wa nje ya
ndoa kuwa ni la siri na wengine wanalifichua kwa wenzao wa ndoa. Wanaume
wanaongoza kuwa na namba kubwa ya watoto wa nje ya ndoa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya pili ni swali:
Nilikosea wapi?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika sura hii
mwandishi anajaribu<span> </span>kuangalia sababu
zinazopelekea watu kuangukia kwenye chaguo baya na kujiingiza kwenye matatizo
ya ndoa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la kwanza ni:
Hatukujijua! Ni muhimu mtu kujijua yeye ni nani na aliumbwa kwa ajili gani. Ili
mtu afanye uchaguzi mzuri na kumpata mwenzi wa maisha ni vyema, ajijue kwanza.
Kwa kujiua, anaweza akawajua na wengine na hatima kumjua ni mtu gani anaweza
kuwa mwenzi wa maisha.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la pili ni <span> </span>kwamba:<span>
</span>Hatukujua wito wetu: “ Kila mtu ameletwa duniani kwa sababu maalumu. Hivyo,
si kila mwanaume ama mwanamke alipangiwa maisha ya ndoa kama ambavyo wengi wetu
tunadhani..” (uk wa 19). Ka kutetea hoja hii mwandishi naonyesha historia ya
watu ambao waliishi maisha yao yote bila kuingia kwenye ndoa na wengine
walizaliwa wakiwa matowashi. Ili ndoa iwe ya furaha na amani ni muhimu wanandoa
wakatambua wito wao.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la tatu:
Tulikurupuka! Kwamba watu wanapotafuta wachumba hawatulii na kuchunguza na
kutafakari juu ya wachumba wao: “ Ni kama tulirukia gari lililokuwa katika
mwendo bila ujuzi..” (Uk wa 22). Mtu anapomtafuta mchumba kwa lengo la kufunga
ndo ni lazima ajipatie muda wa kutosha. Uchumba wa siku moja na ya pili kufunga
ndoa ni hatari kubwa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la nne: Hatukuzijua
familia za wenzetu: “ Tulitakiwa kujua historia ya maisha ya familia ya wenzetu
kikamilifu. Kujua kama wana maisha ya ajabu kama vile uchawi ama<span> </span>wapenda ushirikina. Maana kama huyu
alizaliwa, akalelelewa katika maisha ya aina hii, uwezekano wa yeye kushiriki
matendo hayo ni mkubwa...” ( Uk wa 26).</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la tano ni:
Hatukuwajua wenzetu:</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ni muhimu kumfahamu mwenzako
vizuri kabla ya ndoa. Ni muhimu pa kuwafahamu marafiki zake, kufahamu kama huyu
ni msiri au ni muwazi? Na je mlikutana katika mazingira gani? Ni mazingira ya
kuruhusu mtu kuwa wazi au ni mazingira ambayo yanaweza kuwa ni shinikizo? Je
tulikutana kazini? Tulikutana kanisani au kwenye baa? Kama tulikutana kwenye
baa, kesho na keshokutwa tabia kama hiyo inaweza kujirudia.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kosa la sita na saba, ni
kutojua uzito wa agano. Maana ndoa ni <span> </span>agano linalowaunga watu wawili, kwa imani
nyingine, hawa wanakuwa kitu kimoja. Si wawili tena bali ni kitu kimoja. Je
wanandoa tunajua uzito huu kabla ya kufunga ndoa? Tunatafakari juu ya uzito huu
kabla ya kufanya uamuzi?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya tatu ni swali
pia: Ndoa yangu ni mpango wa Mungu?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi, anataka
tutafakari juu ya ndoa kama mpango wa Mungu. Tunafunga ndoa kujifurahisha au
tunafunga ndoa kuendeleza Mango wa Mwenyezi Mungu wa kupendana na kuzaa kwa
lengo la kuujaza ulimwengu?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya nne ni swali
jingine: Nani maadui wa ndoa yangu? Katika utafiti uliofanywa, ambao unajadiliwa
kwenye sura ya kwanza. Wanandoa walipoulizwa swali hili, wote waliwanyoshea
wengine kidole, kwamba maadui wa ndoa zao ni ndugu, wazazi na marafiki.
Walishindwa kutaja kwamba adui mkubwa wa ndoa ni wanandoa wenyewe. Kuna suala
la kuendeleza utoto katika ndoa. Mtu anafunga ndoa lakini anashindwa kuachana
na tabia zake za kitoto; hiki ni chanzo cha matatizo katika ndoa nyingi. Pili
kuna suala la kuendeleza ukahaba kwenye ndoa na hiki ni chanzo cha matatizo
mengi kwenye ndoa. Kuna tatizo la kunyimana tendo la ndoa; likisababishwa na
kutembea nje ya ndoa na wakati mwingine unywaji wa pombe kupindukia. Kuna kauli
mbovu kwenye ndoa, ujeuri, majivuno na kudharauliana.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ni wazi hatuwezi kukwepa
kabisa ushawishi wa wazazi katika ndoa zetu. Bila uangalifu, uhusiano wa wazazi
unaweza kujenga matatizo makubwa katika ndoa zetu. Ndugu, jamaa na marafiki nao
wanaweza kuleta matatizo makubwa kwenye ndoa. Na la mwisho ambalo watu wengi
wanasahau ni kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu.<span> </span>Ndoa, ambayo haina msingi wa dini ni vigumu
kusimama na kustawi. Hayo ndo maoni ya mwandishi juu ya matatizo yanayozikumbwa
ndoa nyingi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya tano ni swali
pia: Tufanye nini sasa?</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anasema: “ Kwa
sisi tulioingia<span> </span>katika ndoa, sasa si
wakati wa kujihukumu wala kuhukumu wengine. Si wakati wa kujua kama tulikuwa na
wito wa ndoa ama hapana. Si wakati wa<span>
</span>kuwashambulia wenzetu kwa mabaya yanayotendeka ama yaliyotendeka siku za
nyuma ndani ya ndoa zetu. Si wakati wa kujua iwapo tulifunga ndoana watu wasio
wetu wala chaguo la Mungu..”. Kwa maoni ya mwandishi, kila wakati ni wakuanza
maisha upya. La msingi ni kumrudia Mwenyezi mungu na kuishi kwa kutekeleza
mpango wake. Na la msingi ni kujuta na kuomba msamaha, kuwaomba wenzetu wa ndoa
msamaha, kuwaomba watoto msamaha na kuiomba jamii nzima msamaha.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya sita: Wajibu wa
kanisa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika sura ya mwisho,
mwandishi analigeukia kanisa na kulibebesha mzingo mkubwa wa kulinda na kutunza
ndoa. Kwa maoni yake ni kwamba Familia ndiyo msingi wa kila kitu. Msingi wa
kanisa, msingi ya jamii. Bila kuwa na ndoa nzuri ni vigumu kuwa na jamii nzuri.
Hivyo kanisa lina wajibu mkubwa kuhakikisha ndoa zinakuwa imara na zinadumu.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">V. TATHIMINI YA KITABU.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nianze kwa kumpongeza
Charles B. Misango, kwa kazi hii nzuri sana aliyoiandika. Kusema kweli kazi hii
inaburudisha, inasikitisha na kufikirisha. Utafiti wake juu ya ndoa, umeweka
ukweli wazi. Na kila atakayekisoma kitabu hiki atakuwa makini kumchangua mwenzi
wa maisha.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pili, ni maoni ya baadhi
ya watu waliokisoma kitabu hiki:</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Fred Jackosn wa<span> </span>Keko Dar-es-Salaam, anasema “ Kama nisingesoma
kitabu hiki na kuamua kufuatilia kwa ukaribu historia ya familia na ukoo wa
mchumba wangu, ningejikuta naishi na mtu aliyebobea uchawi. Kitabu hiki
kimeokoa maisha yangu” (uk wa 109)</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Naye Betty wa NMB Makao
Makuu Dar-es-Salaam, anasema: “ Huu ni funuo wa ajabu sana katika maisha yangu
ya ndoa. Kitabu kimenisaidia sana kujua namna gani kudumisha upendo na amani
kati yangu na mume wangu, upi wajibu wangu katika ndoa yangu” (uk 109).</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na Peter Mizambwa wa
Kisarawe, anasema hivi : “ Kama kuna wachumba watakaokisoma kitabu hiki na
kuamua kufuata kile kilichoanikwa, hakika wataamua kuanza upya, maana wengi
tumechumbiana kienyeji kabisa...”(Uk 109)</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kyaruzi-Rc wa Magomeni,
anasema “ Hiki ni kitabu kilichoanika ukweli mtupu wa maisha ya wanandoa wengi.
Kitasaidia sana kuamsha akili za wanandoa na kurejesha amani katika ndoa nyingi
zilizosambaratika na hata zisizo na amani. Kimetoa pia ukweli juu ya wajibu wa Kanisa
kuhusiana na malezi ya wanandoa na kitaokoa wengi”</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50168" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Zainabu Rahab wa
Mikocheni, naye anasema “ Kitabu hiki ni kioo halisi cha kila mwanandoa.
Ingefaa kila aliye katika uchumba akisome kwa makini ili kupata msaada wa Mungu
katika safari <span> </span>ya uchumba...” (Uk wa
109).</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50171" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50170" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tatu, mwandishi wa
kitabu hiki ametuingiza ndani ya tafakuri. Utafiti wake unaonyesha wazi jinsi
ndoa nyingi zilivyokuwa na matatizo. Swali la kujiuliza sote ni je, ndoa ni
Mpango wa Mungu? Je, Mungu alitaka tuishi kwenye kifungo hiki cha ndoa, au
mpango wake ulikuwa ni sisi pia kuishi kama wanyama wengine? Ukiangalia
asilimia ya wanandoa wanao kwenda nje ya ndoa zao, unakuwa na mashaka. Na je
mbona Mwenyezi Mungu, anaendelea kuumba watu wazuri bila kukoma? Mbona hawezi
kuviwekea kizingiti vishawishi ndani ya miili yetu? Yeye si ni Muumba wa vyote?
Vinavyoonekana na visivyoonekana? Je ndoa ni tendo la ndoa au ni zaidi ya hapo?
Mvuto unaokuwepo kati ya Me na Ke, unaweza kufungiwa tu kwenye ndoa? Mbona hata
baada ya mtu kufunga ndoa, bado macho yanaendelea kuona na mvuto unabaki? Mvuto
ni dhambi au kuutukuza uumbaji wa Mwenyezi Mungu? Kusifia uumbaji wa Mwenyezi
Mungu ni dhambi? Na kusifia mipaka yake ni wapi? Kuona na kuacha? Kuona na
kugusa? Au Kuiingia kwenye ndoa? Na tuiingie na wangapi kwenye ndoa? Ndoa ya mke
mmoja na mwaume mmoja? Mwanaume mmoja wanawake wengi? Au wanawake wengi mme
mmoja? Au maisha ya uhuru bila ndoa, lakini tunatenda tendo la ndoa? Ni upi ni
mpango wa Mungu? Ni changamoto!</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50173" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50175" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nne, mwandishi ameonyesha
wazi kwamba mara nyingi tunachezea kifungo hiki cha ndoa. Hakuna mafunzo kwa
vijana. Tumepuuzia mafundisho yetu ya jando na unyago kiasi kwamba vijana wetu
wanatenda na kufuata uzoefu wa kila siku bila kuwa na mafunzo ya maisha.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50178" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50177" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tano, mwandishi
anaonyesha wazi kwamba ndoa nyingi zina siri kubwa; watoto wa nje na nyumba
ndogo. Hata wale ambao ni watu wa “Mungu” nao wana nyumba ndogo na watoto wa
nje. Mungu, apishe mbali maana kufuatana na utafiti wa kitabu hiki, watu
wakiamua kupima DNA, ndoa nyingi zitasambaratika maana watoto wengi watagundulika
ni wa kubambikizwa.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50181" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50180" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sita, kitabu hiki
kianzishe mjadala kwenye jamii yetu, ili tutafute mamoja na ushauri wa
mwandishi, jibu<span> </span>la tufanye nini ili ndoa
zetu ziwe imara. Tufanye nini ili tufanye uchaguzi mzuri wakati wa kuwatafuta
wenzi wa maisha.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">VI. HITIMISHO.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kama kawaida yangu,
ningependa kuwashauri watanzania kukitafuta kitabu hiki na kukisoma. Ni imani
yangu kwamba watajifunza mengi kutoka kwenye kitabu hiki na hasa utafiti
uliofanywa na mwandishi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50183" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50186" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50185" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Lakini, pia ningependa
kuwashauri wale wote watakaokisoma kitabu hiki watafute pia na vita bu vya Dr.
Binagwa, juu ya ndoa. Utafiti wa mwandishi wa kitabu hiki unamwandaa msomaji
kuvisoma vitabu vya Dr. Binagwa, ambaye anaandika kwa undani juu ya mahusiano
kwenye ndoa. Maana, haitoshi kutaja kwamba kuna suala la kunyimana tendo la
ndoa, lakini pia kuna maelezo juu ya tendo lenyewe na sababu za kufikia hatua
ya kunyimana.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Dr.Binagwa, anafafanua
vizuri hata juu ya tendo lenyewe. Haitoshi tendo tu, bali kuna namna ya
kutenda<span> </span>tendo hilo. Hivyo kuna mengi juu
ya ndoa, na kwa kusoma vitabu hivi, mtu atagundua kwamba ndoa ni kitu kipana
ambacho bila mafunzo ni vigumu kukiishi. Ndoa zinavunjika kwa vile sote
tumepuuzia suala la kufundisha juu ya ndoa. Ni muhimu kurudisha mafundisho ya
Jando na Unyago. Pia ni muhimu kusoma na vitabu vya Jando na Unyago, ambavyo
zamani tulivisoma tukiwa sekondari.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwisho ni ushauri kwa
mwandishi, kwamba sasa ana kazi ya kufanya.<span>
</span>Yeye pia ni lazima atafute vita bu vya Dr. Binagwa na kuvisoma na kuona
jinsi vinavyomsaidia kuandika kita bu kingine juu ya ndoa. Hiki sasa ni
utafiti. Tunataka kitabu cha ndoa kutoka kwa mtu wa ndoa kama yeye na
ikiwezekana atoe mifano ya ndoa yake mwenyewe. Kama tunataka kulisaidia taifa
letu, na kama tunakubaliana kwamba taifa imara linajengwa na familia imara ni
lazima mwandishi aonyeshe hili kwa mifano zaidi.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50218" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50220" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Je watu wawili wanaweza
kuishi ndoa yao na ikawa imara? Au wanaihitaji msaada wa ndugu jamaa na
marafiki? Tendo la ndoa, ni la wawili, lakini maisha mengine yanayoizunguka
ndoa, kama uwazi, kujifunua na kutafuta msaada kwa wengine, kutafuta <span> </span>ushauri, ndoa na ndoa kusaidiana; kufundishana
uvumilivu na kuchukuliana ni jambo la muhimu sana. Hatimaye ndoa si ya watu
wawili, bali ni suala la jamii nzima. Ndoa ikibaki kwenye kuta za watu wawili,
ni vigumu sana ndoa hiyo kusimama na kudumu.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50216" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50214" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50212" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus
Karugendo.</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50210" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50188" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv1151445140MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_50207" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-74837320182139527452013-12-10T00:18:00.000-08:002013-12-10T00:18:06.805-08:00LINE ZA SIMU<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_48999" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_48998" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">KODI YA LINE ZA SIMU NI
MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49001" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49004" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49003" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wakati bei ya muda wa
maongezi iko<span> </span>juu na yenye utata; na hili
si kwa Vodacom peke yake bali ni kwa mitandao yote ya simu; wakati tunashangaa na
kulalamika ni kwa nini wawakilishi wetu Bungeni, wasilione hili na kuhakikisha
bei ya muda wa maongezi inakuwa na unafuu ili tuweze kufikia kile kinachoitwa
maisha bora kwa kila Mtanzania tunaongezewa na hii kodi ya line za simu. Pamoja
na faida kubwa itakayotokana na kodi hii (kama tulivyoelezwa, ambavyo si
tofauti sana na yale tunayoelezwa kila mwaka bila kuona utekelezaji) bado huu
ni mzigo mkubwa kwa mtu anayeitumia simu yake kwa matumizi ya lazima na muhimu.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49015" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49018" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49017" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><span> </span>Binafsi nina mashaka na uwiano wa fedha na
muda. Kwamba ninapolipa shilingi elfu moja ni mfumo gani unatumika kuhakikisha
kwamba muda nilioutumia thamani yake ni shilingi elfu moja. Kuna mfumo gani wa
wazi wa kuhakikisha fedha tunazolipa kwa kununua vocha za muda wa maongezi
zinawiana na muda; mfano kama ni elfu moja kwa daika tatu ikajulikana, ikiwa
kinyume mtu akalalamika<span> </span>Pia na uwiano wa
kodi na matumizi ya line ya simu; kwamba anayetumia simu kuzalisha milioni moja
kwa mwezi, alipe kodi ya shilingi elfu moja na yule anayezalisha elfu kumi kwa
mwezi alipe kodi ya line ya simu shilingi elfu moja na anayebeep akapigiwa
alipe kodi ya elfu moja kwa mwezi! Tumelishwa kasumba na makampuni haya ya simu
(Sawa na madawa ya kulevya) kwamba fedha zikiisha kwenye simu ni lazima
utakwenda mwenyewe kununua. Hatulalamiki ili kutaka kujua uwiano wa fedha na
muda. Kama mtandao una wateja milioni mmoja, hata ukigonga shilingi miambili
kwa kila mteja, unakuwa una fedha nyingi. Inajionyesha wazi kwamba Vodacom, na
mitandao mingine ya simu wanatengeneza faida kuliko kutoa huduma. Hii ni sawa
kwa vile wao wanafanya biashara. Basi, biashara yao iwe nzuri kwa kutoa huduma
iliyo juu ya kiwango na si chini<span> </span>ya
kiwango. Na biashara yao iwe na uwiano wa fedha na muda. Lakini pia kwa vile
kodi ya line za simu imeanza, kuwepo uwiano kati ya matumizi ya simu<span> </span>na ulipaji kodi.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49020" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49023" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49022" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa mitambo ya kisasa,
makampuni ya simu yanaweza kujua ni watu gani wanatumia huduma yao kutengeneza
faida kubwa na ni watu gani wanatumia mitandao yao kwa huduma ya lazima kama
kutoa taarifa za misiba, kutuma karo na matumizi mengine madogo madogo. Mfano,
wale wanaotumia huduma ya Mpesa, wale wanaopitishia zaidi ya milioni kumi
kwenye mtandao kwa mwezi, watalipa je kodi ya elfu moja sawa sawa na
anayepitisha elfu hamsini kwa mwezi?</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49025" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49028" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49027" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wakati baadhi yetu tunajiuliza
mantiki ya serikali inayoamini kwenye kauli mbiu ya Maisha bora kwa kila
Mtanzania, kukubali viwango vya muda wa maongezi kuwa sawa kwa watanzania wote;
maskini wa vijijini, wafanyakazi na wafanyabiashara<span> </span>wakubwa, bado tunaletewa na<span> </span>kodi hii ya line za simu iliyo sawa kwa
watanzania wote. Katika hali ya kawaida na kwa nchi ambayo bado katiba yake
inatambua na kufuata Ujamaa, mkulima wa kijijini anayetumia simu yake kuita
gari la<span> </span>wagonjwa kumbemba mama mjamzito,
atalipa muda wa maongezi sawa na mfanyabiashara anayetumia simu yake kufanya
“Dili” la bilioni tano? Au mkulima wa vijijini anayetumia simu kusambaza ujumbe
wa msiba kwa ndugu na jamaa, atalipa muda wa maongezi sawa sawa na
mfanyabiashara anayetumia simu yake kusambaza ujumbe wa kudai madeni yake kwa
wateja wake zaidi ya bilioni kumi?</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49030" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49033" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49032" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa wengine mawasiliano
ya simu ni anasa, wengine ni biashara na walio wengine ni huduma ya muhimu.
Kuna wanaotumia simu kutongoza wanawake na kuzungumza mambo ya mapenzi siku
nzima, hawa wakilipishwa kodi ya line za simu ni sawa, kuna wanaotumia simu
kufanya biashara na kuwasiliana na wateja, hawa nao wakilipishwa kodi ya line
za simu ni sawa, lakini<span> </span>wale wanaotumia
simu kama huduma muhimu kwenye jamii kuwatoza kodi ya line za simu si sawa
sawa. Mfano mtu anayenunua simu ya kiganjani kwa bei ya shilingi milioni moja,
na wakati mwingine anazo zaidi ya tano za bei hiyo hiyo, maana kila mtandao una
simu yake, atalipaje kodi ya line za simu na muda wa maongezi sawa sawa na mtu
anayenunua simu ya kiganjani kwa bei ya shilingi hamsini?</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49035" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49038" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49037" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kiasi kikubwa cha watu
wa vijijini wenye watoto wao wanaoishi na kufanya kazi mijini, wanakuwa na simu
ambazo mara nyingi hawana uwezo wa kununua muda wa maongezi, wanachofanya ni
“Kubeep”, wasipotumiwa muda wa maongezi basi wanapigiwa simu na watoto wao. Leo
hii hawa kuwatoza kodi ya line za simu ni kuwalazimisha kuachana na huduma hii
muhimu.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49040" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49043" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49042" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wakati tunategemea
serikali iwe upande wa wananchi na kuwalinda dhidi ya makampuni makubwa ya
uwekezaji, tunashuhudia kinyume chake. Makampuni ya simu kama yalivyo makampuni
mengine yapo hapa kufanya biashara na kuendelea kuwapumbaza wananchi:</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49045" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49047" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49050" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49049" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tarehe 27 Januari
Alhamisi mwaka 2005 vyombo vya habari vilitoa habari inayosema: " Vodacom
yawaangukia wateja wake - KAMPUNI ya simu za<span>
</span>mkononi Vodacom imetoa maelezo yaliyosababisha hitilafu na kukatika kwa
mawasiliano katika mtandao wake uliosambaa nchini kote Ijumaa iliyopita.....
Tunawaomba radhi wateja wetu wapendwa kwa usumbufu uliotokea na hasa katika
kipindi cha sikukuu na tunapenda kuwafahamisha wateja wetu kuwa tatizo
limerekebishwa na huduma za Vodacom zitaendelea kama kawaida....Taarifa
ilimkariri Jose dos Santos, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, akisema kama ishara
ya kuonyesha masikitiko na nia njema, wateja wote wa Vodacom watapewa SMS 10 za
bure kwa mkupuo kuanzia Januari 27,2005".</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49054" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49053" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wateja wa Vodacom,
walifurahia meseji za bure. Kama kawaida yetu watanzania hatupendi kutafakari
na kuyaangalia mambo kwa undani. Ofa hii inaweza kumfumba mtu macho akaacha
kuona mambo mengine muhimu. Na kwa vile Vodacom, hawana mfumo wa kutoa maoni na
kujadiliana na wateja wao, furaha hii ya meseji ilibaki kuwa furaha ya mtu
mmoja mmoja au vikundi. Ukweli ni kwamba jambo hili linaigusa jamii nzima maana
mtadao wa Vodacom umeenea nchi nzima. Na jambo la mawasiliano linamgusa kila
mwananchi. Mtwara hadi Karagwe, Kigoma hadi Arusha, wanaguswa na mafanikio au
matatizo ya Vodacom. Mawasiliano si anasa, ni kitu muhimu na cha lazima katika
jamii yoyote ile.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49056" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49059" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49058" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mbali na na sms za bure,
makampuni haya ya simu yamekuwa yakitoa misaada ya madawati na vitu vingine
vidogo vidogo vya kuwapumbaza watanzania na kuwafumba macho, lakini ukweli ni
kwamba makampuni haya yanapata faidi kubwa. Kufuatana ukweli huo, serikali
iliyo makini ingetengeneza mfumo wa viwango tofauti vya bei ya muda wa
maongezi; watu wanaozitumia simu kwa anasa, wawe na viwango vyao, watu
wanaozitumia simu zao kwa biashara wawe na viwango vyao na watu wanaotumia simu
kwa matumizi ya lazima na muhimu wa wawe na viwango vyao. Na kwa mantiki hiyo
hiyo basi hizi kodi za line za simu zitolewe na makampuni yenyewe, hata hivyo
yanakuwa yamevuna vyakutosha. Kwa mfumo huu, tunaweza kuimba wimbo wetu wa
maisha bora kwa kila Mtanzania, vinginevyo ni kuendelea kuwahadaa wananchi na
kuwalazimisha kuendelea kuishi kwenye umaskini mkubwa.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49062" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49064" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49066" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus
Karugendo.</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49068" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49070" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">www.karugendo.net</span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49072" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7029916997MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_49074">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-72991583777932528572013-12-10T00:16:00.002-08:002013-12-10T00:16:33.274-08:00WAAFRIKA TUSIPIGANE<div class="yiv2558248316msobodytext" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46338" style="background-color: transparent; color: black; font-family: times new roman, new york, times, serif; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46426" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">WAAFRIKA TUNA MATATIZO MENGI,
TUSIPIGANE!</span></div>
<div class="yiv2558248316msobodytext" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46428" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><br /></span></div>
<div class="yiv2558248316msobodytext" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46431" style="background-color: transparent; color: black; font-family: times new roman, new york, times, serif; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46430" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho
Kikwete, ambaye ndiye amiri jeshi mkuu wa taifa letu la Tanzania, ametoa tamko
kali kwamba atakayeichokoza Tanzania, tutamchapa. Inafurahisha kujua kwamba
jeshi letu liko imara. Hapana shaka kwamba tuna jeshi zuri la kizalendo na
Jeshi letu ni Jeshi la Wananchi. Pamoja na pongezi hizi kwa Rais wetu na jeshi
letu, ni lazima tuwe wazi kabisa kwamba vita si kitu kizuri. Vita ni kumwaga
damu, vita ni kupoteza maisha, vita ni kuzalisha wakimbizi na mahangaiko ya
watu na hasa watoto na wanawake, vita ni kuvuruga uchumi. Na vita si mpango wa
Mungu! Kama kuna njia nyingine ya kumaliza tatizo, bila kuingia kwenye vita, ni
busara kuifuata njia hiyo.</span></div>
<div class="yiv2558248316msobodytext" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46435" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46434" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">La pili, ni je hawa
wanaotuchokoza, na tunataka kuwachapa ni watu gani? Ni Wachina, Wajapani, Wamarekani
au Waafrika wenzetu? Kama ni Waafrika, tuseme hapana: Waafrika tuna matatizo
mengi, tusipigane! Tunahitaji kuungana zaidi ya kupigana; hatuna chakula cha
kutosha, hatuna maji, hatuna makazi bora kwa kila mwananchi, tunakufa kwa
magonjwa yanayotibika kama malaria na mengine, watoto wengi bado wanakufa
wakiwa chini ya umri wa miaka mitano, hatuna elimu ya kutosha na matatizo
mengine mengi yanayotufanya kujuliana kama “Masikini” wa dunia hii au watu wa
dunia ya tatu. Tuna maadui wengi, na maadui wetu wanafanana, hivyo ni lazima
kuungana ili kupambana nao. Wale wanaotuchukia wanatukejeli kwamba Afrika
hatuna la kutufanya kuungana: tunaunganisha umasikini wetu? Tunaunganisha
ufisadi wetu? Tunaunganisha nini? Kama tumeshindwa kujenga utaifa,
tutaweza kujenga Afrika moja iliyoungana? Kama makabila bado yanatengana na
kubaguana ndani ya nchi mmoja, itawezekana kuunganisha bara zima la Afrika? <span> </span>Ingawa utaifa ni kitu kilichopandikizwa
vichwani mwetu na wakoloni, lakini sasa hivi ndiyo ukweli uliopo kwamba tuna
nchi za Afrika, zina mipaka na uhuru wake. Hata tukifanikiwa kuondoa mipaka hii
siku moja, swali ni je watu wa nchi hizi ni wamoja? Watu wa nchi hizi wana
mshikamano? Maana huwezi kuwa na mshikamano na wengine kama wewe huna
mshikamano nyumbani kwako. mbona hadi leo hii hakuna sauti moja ya Afrika?
Mbona Afrika inashindwa kutatua matatizo yake yenyewe? </span></div>
<div class="yiv2558248316msobodytext" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46438" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46437" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Afrika inahitaji mshikamano
kupambana na utandawazi na matatizo mengine mengi. Tukumbuke utandawazi hauna
rangi. Afrika inahitaji mshikamano kupambana na Ubeberu unaosambaa kwa kasi na
kutishia uhai na ustawi wa Waafrika. Vita nyingi kwenye bara la Afrika inakuwa
na msukumo wa nje; inakuwa na msukumo wa wale wanaotaka tupigane ili watutawale
tena kwa njia za kisasa zenye kubeba maneno ya kinafiki “ dunia ni kijiji
kimoja”. Ubeberu hauna rangi. Tulizoea ubeberu wa Wazungu, lakini sasa hivi
kuna tishio la ubeberu wa Kichina na hata ubeberu wa Kiafrika; maana kuna nchi
za Afrika ambazo zinaanza kuwa na nguvu kubwa ya kiuchumi na nyingine
zinatumiwa na nchi za magharibi kuzinyanyasa nchi changa za Afrika. Je sababu
zilizowasukuma wazee wetu kusimama na kupinga ukoloni bado zipo? Ni kiasi gani
Mwafrika amejikomboa kifikira baada ya Uhuru? Ni kiasi gani Mwafrika ametambua
kwamba mipaka ya nchi za Afrika iliwekwa na wakoloni?</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46441" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46440" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mshikamano wa Waafrika, ni
tofauti na muungano wa nchi za Afrika. Wakati muungano wa nchi za Afrika
unatengenezwa na viongozi, mshikamano unachipuka kwa njia nyingine tofauti;
Maana mshikamano unatengenezwa na watu wenyewe; vuguvugu hili linajenga
mazingira ya kwamba Mwafrika popote alipo akishikwa sote tumeshikwa. Mshikamano
unaweza kuzaa muungano imara kuliko muungano unaoshinikizwa na viongozi wa
Afrika.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> Mfano, mshikamano wa
Watanganyika na Wazanzibari; unaweza kuunda muungano wa nchi hizi mbili ulio
imara. Watu wakihusiana kwenye mambo ya kijamii ya kuoana, kufanya
biashara kwa pamoja, kutembeleana, kuabudu pamoja na kuibua uzalendo imara wa
nchi hizi mbili, swala la muungano linakuja lenyewe. Leo hii watu wameanza
kuhoji Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, maana kuna ushahidi kwamba muungano
huu ulizaliwa au ulitengenezwa na urafiki wa watu wawili; inawezekana pia
kwamba watu hawa walisukumwa na hekima, busara na mapenzi ya nchi zao, lakini
ukweli unabaki pale pale, kwamba Marehemu Mwalimu Nyerere na Marehemu Abed
Karume, hawakuwashirikisha wananchi juu ya swala la muungano.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na kuziunganisha nchi za Afrika
ni wazo ambalo mpaka sasa limekuwa likishughulikiwa na viongozi wa Afrika bila
ya kuwashirikisha wananchi wa Afrika. Kwa kifupi ni kwamba umoja wa nchi uhuru
za Afrika ni umoja wa viongozi wa nchi za Afrika. Viongozi wanafanya mikutano
na kutafuta namna ya kuunganisha nchi zao. Lakini hatujasikia viongozi hawa
wakitafuta maoni ya wananchi juu ya kuziunganisha nchi hizi za Afrika. Muungano
wa Tanganyika na Zanzibar ni mfano mzuri wa umoja wa nchi za Afrika. Vingozi wa
nchi hizi mbili walikutana na kukubaliana juu ya muungano wa nchi zao mbili
bila kuuliza maoni ya watu. Historia imetufundisha kwamba muungano huu
umeendelea kuwa na matatizo hadi leo hii. Ni wazi waanzilishi wa muungano
walikuwa na nia njema kwa watu wao. Lakini leo hii mambo yamegeuka; huwezi kumwakilisha
mtu bila kusikia matakwa yake.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46444" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46443" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">La kujifunza hapa ni kwamba tunahitaji sauti moja ya
Afrika. Na sauti moja hii haiwezi kujengwa na viongozi wa nchi hizi za Afrika.
Sauti moja ya Afrika italetwa na wananchi wa Afrika. Mshikamano wa Waafrika, ndio
chombo pekee cha kuleta sauti moja na kusukuma kasi ya maendeleo ya nchi
za Afrika. Marais wetu wakitupiana maneno, haina maana kwamba wananchi wa nchi
hizo wana magomvi miongoni mwao. Marais wetu wakichukiana, haina maana kwamba
nyuma yao kuna wananchi wanaochukiana pia.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46447" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46446" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kuna watu wana utata juu ya
Umajumui (Pan Africanism) na Umoja wa Afrika, <span> </span>ingawa maneno haya yanafanana, yana maana
mbili tofauti. Umajumui unamaanisha zaidi Mshikamano wa Waafrika; au Mshikamano
wa watu weusi popote walipo duniani. Na Umoja wa Afrika unamaanisha zaidi
kuunganisha nchi zote za Afrika. Na kuna ndoto kwamba siku moja Afrika itakuwa
na rais mmoja na kuwa na fedha moja ya Afrika.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46466" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46465" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">La msingi, na lenye maana kubwa
kwetu ni mshikamano wa Waafrika. Hili likifanikiwa, hatuwezi kuwa <span> </span>na vita katika Bara letu la Afrika. Mara
nyingi wanaoleta vita, si wananchi bali ni viongozi. Ni wakati wa kusimama
kidete na kuwaambia viongozi wetu kwamba hatutaki vita. Kama kuna matatizo, ni
muhimu kukaa kwenye meza ya majadiliano. La muhimu ni ushirikishwaji. Viongozi
wasijadili peke yao na kugombana hadi kufikia hatua ya “Kutishiana” kwa
kupigana, bali viongozi wetu watushirikishe mabishano ili na sisi tuchangie na
mjadala wetu uanze na hitimisho kwamba tutajadiliana, tutatofautiana,
tutachukiana hata kwa sura, lakini hatutoani uhai!</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46463" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46462" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46460" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46459" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122.</span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46449" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46457" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46451" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv2558248316msonormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_46455" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com2tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-63047727418555270122013-12-10T00:14:00.000-08:002013-12-10T00:14:02.166-08:00UTHIBITI WA HUDUMA ZA KIUCHUMI TANZANIA- MWANDOSYA<div class="yiv3612888677MsoBodyText" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44136" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44135" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">UHAKIKI WA KITABU:<span> </span>UTHIBITI WA HUDUMA ZA KIUCHUMI TANZANIA</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44133" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44130" style="margin-left: .5in; text-align: justify;">
<b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><span>1.<span style="font: 7.0pt;">
</span></span></span></b><b id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44129"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44128" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Rekodi za Kibibliografia.</span></b></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44126" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44123" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44122" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Jina la kitabu
kinachohahikiwa hapa ni UTHIBITI WA HUDUMA ZA KIUCHUMI TANZANIA , Kimeandikwa
na<span> </span>Profesa Mark Mwandosya. Mchapishaji
wa kitabu hiki ni E&D Vision Publishin Limited na amekipatia namba<span> </span>ifuatayo katika sekwensia ya vitabu duniani
(ISBN): - 978-9987-735-09-9 Kitabu kina kurasa 151<span> </span>. Na anayekihakiki sasa hivi katika safu hii
ni mimi Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44015" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44140" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">II. <b>Utanguliz</b>i</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44142" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44144" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44146" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Udhibiti ni njia
mojawapo inayotumika kusimamia uchumi wa nchi na kuendeleza ustawi wa jamii.
Udhibiti wa huduma za kiuchumi (Public utilities) unahusu kuweka mizania kati
ya kuwawezesha watoa huduma na kuwalinda watumiaji wa huduma kama vile maji,
umeme, uchukuzi na mawasiliano. Suala Udhibiti wa huduma za uchumi lilijitokeza
kwanza miaka zaidi ya 150 iliyopita, huko Marekani na Ulaya kwa madhumuni
makubwa ya kumlinda mlaji katika mazingira ya uchumi wa soko huria.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44148" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kinaelezea
chimbuko la udhibiti Tanzania katika muktadha wa mabadiliko ya uchumi duniani
pamoja na udhibiti katika nchi nyingine. Ni kitabu chenye maarifa ya msingi kwa
kila mtuamiaji wa huduma za kiuchumi, pamoja na wanafunzi, wasomi, wafanyakazi
na viongozi. Lakini pia ni kitabu kinachomsaidia mwananchi kuelewa udhibiti na
kufahamu jinsi mfumo huu unavyolenga kumtetea katika mfumo wa soko huria.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44151" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44150" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kina sura 15
ambazo zinaongelea: Sura ya kwanza ni Utangulizi, sura ya pili ni Dhana ya
Udhibiti, ambayo inajadili malengo ya udhibiti, huduma za kiuchumi, mazingira
sawa ya ushindani, uhuru wa Mdhibiti, Uteuzi wa Bodi na Ofisa Mtendaji Mkuu,
Uhai wa bodi, nidhamu ya usimamizi wake. Sura ya<span> </span>tatu ni juu ya Maeneo Muhimu ya Udhibiti,
ambayo inajadili kwa undani juu ya Leseni, Kudhibiti Mwenendo wa Bei na <span> </span>tozo Mbali mbali, mwongozo wa maadili. Sura ya
nne ni juu ya Uwezo wa kifedha wa Mdhibiti. Sura ya tano ni juu ya kuwalinda
watumiaji wa huduma na bidhaa. Sura ya sita ni juu ya Muundo wa vyombo vya
Udhibiti. Sura ya saba inajadili Udhibiti wa sekta za Kiufundi na kufafanua
zaidi juu ya Mifano ya dhibiti wa Masuala ya kiufundi, usimamizi wa Masafa ya
Redio, Muunganisho wa mawasiliano na namba za simu kama rasilimali muhimu. Sura
ya nane inajadili juu ya Uhusiano Kati ya serikali na mthibiti. Sura ya tisa inajadili
juu ya Udhibiti na ushindani wa Biashara; Utaratibu wa kumlinda mlaji na mtoa
huduma, Uhusiano wa udhibiti na huduma na wa biashara. Sura ya kumi inajadili
juu ya Sheria za Kisekta. Sura ya kumi na moja inajadili juu ya Uhusiano kati
ya Bunge na Mdhibiti. Sura ya kumi na mbili ni juu ya Udhibiti katika nchi
nyingine. Sura ya kumi na tatu inaongelea Masuala Mtambuka. Sura ya kumi na nne
inajadili Mafanikio na changamoto za udhibiti; Kusimamia utekelezaji wa sheria,
utoaji wa Leseni, sekta ya mawasiliano, sekta ya maji, sekta ya umeme, sekta ya
uchukuzi, sekta ya mafuta ya petroli na watumiaji wa hudumaza kiuchumi. Sura ya
mwisho ya kumi na tano ni hitimisho na kitabu kinafunga na orodha ya marejeo.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi wa kitabu
hiki, Mark Mwandosya, amewahi kuwa Profesa wa Uhandisi wa Umeme Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam, Kamishana wa Nishati na Masuala ya Petroli, Katibu Mkuu Wizara
ya Maji, Nishati na Madini, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Waziri
wa Mawasiliano na Uchukuzi, Waziri wa Nchi (Mazingira), Ofisi ya Makamu wa
Rais, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, na waziri wa Maji. Kwa sasa yeye ni waziri
wa Nchi(Kazi Maalum), Ofisi ya Rais.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika aya zifuatazo nitafanya
uhakiki wa kitabu hiki, lakini kwanza kwa kudokeza mazingira yanayokizunguka
kitabu hiki. </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">III. <b>Mazingira
yanayokizunguka kitabu</b></span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kimeandikwa
na msomi tena profesa. Tumekuwa tukiwalalamikia wasomi wetu kukaa kimya na
kushindwa kulielekeza taifa letu la Tanzania. Sasa mwandishi wa kitabu hiki
amekata mzizi wa fitina. Ameandika, labda sisi tushindwe kusoma. Tumekuwa tukiwalalamika
wasomi wanaojitahidi kuandika, lakini wanafanya hivyo kwa lugha za kigeni.
Mwandishi wa kitabu hiki amekata mzizi wa fitini<span> </span>kwa kuandika kitabu kwa lugha ya Kiswahili.
Tumekuwa tukiwalalamika wanasiasa wetu kuhubiri majukwaani na kushindwa kutuandikia
vitabu kama kumbukumbu za leo, kesho, keshokutwa na vizazi vijavyo, mwandishi
wa kitabu hiki amekata mzizi wa fitini, atakuwa ni miongoni mwa wanasiasa
wachache wa Tanzania wanaoandika vitabu. Tumekuwa tukiwalalamikia wanasiasa
kuchanganya siasa na kila kitu hata kuiingilia taaluma nyingine za kisomi,
mwandishi huyu amekata mzizi wa fitina, pamoja na kwamba anaongelea huduma za
kijamii, huduma za kiuchumi, kitabu chake kutoka sentensi ya kwanza hadi ya
mwisho hakuna neno CCM. Ingawa mwandishi ni kada, lakini amevuka ufinyo huo na
kuwa juu katika uwanja wa wanazuoni. Anaandika kwa watanzania wote bila kujali
siasa, dini wala kabila. Ni kitabu cha aina yake!</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Udhibiti ni kitu kipya,
na kusema kweli ni msamiati ambao ni mgumu kueleweka kwa watu<span> </span>wengi ingawa tunashiriki mfumo huu siku kwa
siku. Kitabu hiki, au niseme mwandishi wa kitabu amefanya kazi ya peke kuelezea
maana ya udhibiti. Na sikuelezea tu, bali huyu ni mmoja wa watanzania
walioshiriki kiazi kikubwa uanzishwaji wa udhibiti katika taifa letu.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tumekuwa tukisikia EWURA
– Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji, TCRA – Mamlaka ya Udhibiti wa<span> </span>Mawasiliano, TCAA – Mamlaka ya udhibiti wa
Usafiri wa Anga, SUMATRA – Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Maji.
Lakini ni kiasi gani tumekuwa tukielewa misamiati hii? Ni kiasi gani wananchi
wamefahamu vyombo hivi vya udhibiti na jinsi wao wanavyoweza kushiriki na kutoa
maoni kwenye uendeshaji wa vyombo hivi? Mwandishi amejaribu kwa kiasi kikubwa
na lugha nyepesi kuelezea maana ya udhibiti na chimbuko lake; kipindi cha
mabadiliko makubwa ya mfumo wa uchumi wa Tanzania kutoka mfumo wa uchumi hodhi
hadi mfumo wa uchumi wa soko. Katika uchumi hodhi, Serikali ilishikilia na
kusimamia mihimili yote ya uchumi, kuanzia mitaji, njia za uzalishaji, upangaji
wa bei na uendeshaji wa masoko kupitia mauzo ya jumla na maduka ya<span> </span>rejareja. Katika mfumo huo, serikali kupitia
idara zake, mashirika na kampuni zake, ilikuwa ndiye mwajiri mkubwa katika
uwanja wa ajira rasmi. Kipindi hiki ni na zama hiyo ni ile ya kabla ya mwaka
1985.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44153" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44152" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Kipindi cha mwaka 1985
hadi 2005<span> </span>ni kipindi cha miaka 20
ambacho kimehusisha Awamu ya Pili ya uongozi wa nchi kutoka mwaka 1985<span> </span>hadi 1995; na Awamu ya Tatu, mwaka 1995 2005
iliyokuwa chini ya uongozi wa Rais Benjamin William Mkapa. Kipindi hiki cha
miaka 20 ni kipindi ambacho kinaweza kikausishwa na zama ya mageuzi ya mfumo wa
uchumi wa nchi kutoka mfumo hodhi na kuanzisha misingi na utekelezaji wa mfumo
wa soko. Katika mifumo yote miwili, kumekuwa na udhibiti na usimamizi wa huduma
za kiuchumi na miundombinu. Katika mfumo hodhi, udhibiti na usimamizi huo
ulifanywa moja kwa moja na Serikali kupitia wizara na idara zake wakati mfumo
wa soko umehitaji uanzishaji wa vyombo huru vilivyo nje ya mfumo rasmi wa
wizara na idara<span> </span>za serikali. Kwa urahisi
wa uelewa, angalau kwa nadharia tu, fumo wa vyombo huru vya usimamizi wa huduma
za kiuchumi na miundombinu unafana na uhuru, udhibiti na usimamizi unaofanywa
na Benki Kuu katika sekta ya fedha nchini kupitia sera ya fedha” (Uk xv na
xvi).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44155" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44158" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44157" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi wa kitabu hiki
hafanyi kazi ya kubahatisha, maana mwaka 1985 aliteuliwa na Baba wa Taifa,
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa kamishna wa kwanza wa Nishati na Petroli
na hivyo kuanzisha kwa mara ya kwanza idara kamili ya huduma ya kiuchumi, Idara
ya Nishati. Pia aliwahi kuwa mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya lililokuwa
Shirika la Posta na Simu Tanzania na mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kwa nafasi hizo
aliweza kuwa na uzoefu na uelewa wa huduma tatu za kiuchumi, mawasiliano ya
posta, simu na nishati.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44161" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44164" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44163" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwaka 1992, mwandishi wa
kitabu hiki alihamishiwa Wizara ya<span>
</span>Viwanda na Biashara kama katibu mkuu, akapata nafasi ya kuhusiana moja
kwa moja na mageuzi ya kiuchumi kwa kuanzisha mfumo wa na taratibu za awali za
ubinafsishaji wa viwanda. Pia alikuwa mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya
shirika la Petroli Tanzania (TPDC) na kupata nafasi ya kusimamia huduma muhimu
ya kiuchumi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44166" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44169" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44168" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi wa kitabu hiki
kati ya mwaka 2000 na 2005, alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi na kupata
fursa ya kipekee ya kusimamia maandalizi ya kupitisha Bungeni sheria
zilizoanzisha mamlaka<span> </span>tatu za udhibiti;
Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano(TCRA), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa
Anga (TCAA), Mamlaka ya udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA).
Na mwaka 2008, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, alimteua mwandishi wa kitabu hiki
kuwa waziri wa Maji na Umwagiliaji. Waziri mwenye dhamana ya sekta ya maji kwa
sasa ndiye Waziri anayesimamia Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati ya Maji
(EWURA). Hivyo mwandishi anajua vizuri mada hii hivyo atatufumbua macho.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">IV. <b>Muhtasari wa
Kitabu</b></span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kitabu hiki kinajadili
na kufafanua kwa kina juu ya suala la udhibiti wa huduma za uchumi; kwamba
suala hili la udhibiti<span> </span>lilijitokeza
kwanza miaka zaidi ya 150 iliyopita, huko Marekani na Ulaya kwa madhumuni
makubwa ya kumlinda mlaji katika mazingira ya uchumi wa soko huria. Pia kwamba
mfumo wa sasa wa udhibiti nchini Tanzania ulianza kipindi cha muongo mmoja
uliopita ikiwa ni matokeo ya mabadiliko ya mfumo wa uchumi, kutoka uchumi hodhi
kwenda uchumi wa mseto, mfumo ulioutambua umuhimu wa soko huru na sekta binafsi
katika kuchochea kukua kwa uchumi. Taratibu za kuanzisha mfumo wa sasa wa
udhibiti zilienda sambamba na zoezi la ubinafsishaji. Na kwamba mfumo wa sasa
wa udhibiti unafanana na mifumo katika nchi nyingi, na kwa kiwango kikubwa,
umefuata misingi mizuri ya kimataifa. Misingi hiyo imefafanuliwa katika kitabu
hiki. Mwandishi wa kitabu hiki anaweka wazi kwamba: “ Ni jambo la kujivunia
kwamba nchi nyingi hasa za Afrika kusini mwa Sahara zimekuja Tanzania kujifunza
jinsi ya kudhibiti huduma za nishati, maji na mawasiliano”<span> </span>(Uk 132).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kwanza ya kitabu
hiki ni Utangulizi. Hapa mwandishi anafafanua kwamba udhibiti kwa maudhui ya
kitabu chake unahusu huduma za kiuchumi, na kwamba mfumo wa sasa wa udhibiti wa
sekta za uchumi Tanzania unatokana na mabadiliko ya mfumo wa uchumi kutoka
uchumi hodhi kwenda kwenye uchumi wa kati au uchumi mchanganyiko.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Hapa ndipo mwandishi
anatuelezea na kufafanua juu ya Uchumi wa soko (Market economy): Kwamba “ huu
ni mfumo wa uchumi ambao maamuzi kuhusu uwekezaji, uzalishaji na ugawaji wa
bidhaa na huduma hutegemea upatikanaji wake na mahitaji... katika mfumo huu wa
uchumi, bei za bidhaa na huduma hupangwa na soko lililo huru..” (uk 1);</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia juu ya Uchumi hodhi
au uchumi wa mipango (planned economy), kwamba “Mfumo huu wa uchumi unatoa
maamuzi yanayohusu uwekezaji, uzalishaji na ugawaji wa rasilimali, huduma na
bidhaa yanatokana na mpango wa Serikali. Kwenye mfumo wa aina hii, mipango ya
uzalishaji na utekelezaji wake inatakiwa kuzingatia mahitaji ya jamii na
watumiaji wa huduma...”( Uk 1-2);</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na juu ya Uchumi mseto (
mixed economy), kwamba huu ni mfumo ambao “ Serikali na sekta binafsi
hushirikiana katika kuendesha uchumi. Katika uchumi wa aina hii, uwekezaji
unaachiwa sekta binafsi wakati Serikali inauwa na wajibu wa kuweka mazingira
mazuri ya uwekezaji...” (Uk 2). Katika mfumo huu wa uchumi Serikali hutumia
vyombo vya udhibiti katika kusimamia uchumi. Mwandishi anatufahamisha kwamba
nchi nyingi duniani zina uchumi wa mfumo huu. Na Tanzania ni miongoni mwa nchi
hizo zinazofuata mfumo wa aina hii. Na kudokeza kwamba..<span> </span>“... inabidi soko huria lisimamiwe na
lidhibitiwe ili kumlinda mlaji au mtumiaji wa huduma na kumhamasisha mto huduma
aongeze<span> </span>tija na kuleta faid katika
uchumi kwa ujumla...” (uk 3).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Baada ya ufafanuzi huo,
mwandishi anajadili juu ya Udhibiti kabla ya Sera ya ushindani na kipindi cha
mpito. Linalo elezwa hapa na mwandishi ni kwamba hata kabla ya mabadiliko au
mageuzi ya kiuchumi yaliyoletwa na kuanzishwa kwa soko huru na serikali kujitoa
katika kufanya biashara,<span> </span>kwa kiwango
kikubwa, usimamizi na udhibiti ulifanywa na wizara husika na idara za Serikali.
Waziri muhusika na sekta ndye aliyekuwa na mamlaka ya mwisho katika usimamizi
wa sekta husika , akisaidiwa na<span> </span>Mkurugenzi
wa Idara, Kamishna mhusika na Katibu mkuu wa wizara.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Hata hivyo, katika
sekta za kiufundi na miundombinu, kama vile uchukuzi na mawasiliano, vilikuwepo
vyombo ambavyo vilianzishwa kisheria kusimamia baadhi ya maeneo yaliyohitaji
udhibiti wa kiufundi. Kwa mfano, kabla ya mageuzi ya uchumi, sehemu kubwa ya
sekta ya mawasiliano ya simu na posta ilidhibitiwa na Shirika la Posta na Simu
la Tanzania (TPTC)...”</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Kwa upande wa
uchukuzi, udhibiti, pamoja na<span> </span>kusimamiwa
na wizara yenye dhamana ya uchukuzi, kiutendaji ulikuwa chini ya vyombo
vilivyoanzishwa chini ya wizara mbali mbali...” (Uk 7).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44172" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44171" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Jeshi la Polisi nalo
lilikuwa ni Mdhibiti kwa minajili ya Sheria ya Usalama wa Barabarani, kupitia
Kikosi cha Usalama Barabarani. Wizara yenye dhamana na uchukuzi nayo ilikuwa na
Kitengo cha Usalama Barabarani (Road Safety Unit). Wakala wa Barabara, kupitia
sehemu ya mizani, nao ni sehemu ya udhibiti pamoja na kwamba lengo lao kuu ni
kutunza barabara na kurefusha uhai wa barabara...” (Uk 8).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44175" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44178" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44177" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anaendelea
kutuelimisha juu ya kipindi hiki cha udhibiti kabla ya sera ya ushindani kwamba
“... nyenzo muhimu ya udhibiti kabla ya mfumo wa sasa ilikuwa ni marekebisho ya
bei... Kwa eneo la bidhaa, kiliundwa chombo kilichofahamika sana, Tume ya Bei.
Tume ya bei ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya udhibiti wa Bei ya mwaka 1973” (Uk8).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tukiwa bado kwenye sura
ya kwanza ambayo kwa kiasi kikubwa ni utangulizi, mwandishi anaelezea juu ya
udhibiti wa Huduma za Maji Dar es salaam, Kipindi cha mpito. Kwamba “ Wazo la
kuwa na mdhibiti kwa ajili ya kusimamia sekta ya maji lilijitokeza wakati wa
zoezi la kubinafsisha shughuli za Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar-es-Salaam
- DAWASA au kuwe na udhibiti kupitia mkataba wa ubinafsishaji. Hatimaye,
ilikubalika kwamba awepo mdhibiti maalum” (Uk 11).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44182" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44181" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia katika sura hii
mwandishi anafafanua juu ya udhibiti wa Kimataifa. Kwamba kwa vile Tanzania ni
sehemu ndogo ya ulimwengu, katika masuala ya kimataifa, inaongozwa na
makubaliano ambayo kwa kiwango kikubwa yanasimamiwa na Umoja wa Mataifa na
mashirika yake. Anaelezea chanzo cha kuanzishwa Umoja wa mataifa na sheria
zinazoongoza mashirika ya umoja wa mataifa na kwamba mikataba yote ambayo
Tanzania inaingia na umoja wa mataifa ni lazima ipate nguvu za kisheria.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Katika maeneo ya
matumizi ya rasilimali za pamoja, makubaliano ya kimataifa yamewezesha
kuanzishwa kwa vyombo au mashirika ya usimamizi na udhibiti wa kimataifa.
Mashirika haya yamewezesha pia kuwekwa kwa sheria za kimataifa, taratibu na
kanuni za usimamizi na udhibiti wa kijumla” (Uk 15). Taasisi au vyombo hivyo
vinavyojadiliwa hapa ni pamoja na Shirika la Simu Duniani, Shirika la posta
duniani, Shirika la Kimataifa la Usalama wa usafiri wa Anga na Shirika la
Kimataifa la Usafiri Majini. Aidha, kuna mashirika ya kimataifa yasiyo chini ya
Umoja wa Mataifa moja kwa moja lakini yanadhibiti maeneo muhimu kama viwango
vya kimataifa vinavyoshughulikiwa na Shirika la Viwango Duniani.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya pili ya kitabu
hiki, mwandishi anafafanua juu ya dhana ya udhibiti. Hapa ndipo anapotuelezea
malengo ya udhibiti, huduma za kiuchumi, mazingira sawa<span> </span>ya ushindani, uhuru wa mdhibiti, uteuzi wa
bodi na ofisa mtendaji mkuu, uhai wa bodi, nidhamu na usimamizi wake.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“ Kwa maoni ya
mwandishi, madhumuni muhimu ya udhibiti ni kukuza uchumi wa nchi, ingawa
madhumuni haya hayajitokezi waziwazi katika kazi za udhibiti za kila siku. Bila
udhibiti wenye ufanisi, uwekezaji utalegalega na uchumi hautaweza kukua
haraka...” (Uk 17)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Maneno ‘Huduma za
Kiuchumi’(Public Utilities) yanatumika katika kitabu hiki kumaanisha huduma
ambazo hutolewa kupitia miundombinu ambayo inakuwepo wakati wote na ambayo
inamwezesha mtumiaji wa huduma kuipata huduma hivyo wakati inapohitajika.
Huduma hizi ni kama vile umeme, mafuta ya petroli, gesi asilia, maji, uondoaji
maji taka , mawasiliano ya posta na mawasiliano ya kielektroniki kama vile
simu, intaneti, radio na<span> </span>televisheni.
Kwa maana hiyo pana ya huduma za kiuchumi, huduma hizo ni pamoja huduma za
uchukuzi, kama vile uchukuzi wa anga, ardhini (reli, mabasi, malori) na
uchukuzi wa majini” (Uk 18).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">La kujifunza hapa ni
kwamba huduma za kiuchumi huangaliwa kwa karibu na Serikali zote duniani.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kazi kubwa ya mthibiti
ni kuweka mazingira sawa ya ushindani ( Uwanja sawa wa ushindani) “...Kwani
inatarajiwa kwamba soko litajirekebisha lenyewe na huduma na bidhaa kuendelea
kutolewa ipasavyo. Lakini soko la namna hiyo ni ndoto tu ambayo kama ilivyo
njozi nzuri, tungependa itimie. Kwa kawaida haiwezekani. Ndipo unapokuja
umuhimu wa mdhibiti. Na moja ya majukumu yake muhimu sana ni kuweka mazingira
sawa ya ushindani, kwa lugha nyingine kuweka uwanja wa ushindani ulio sawa
(level playing field)” ( Uk 19).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ili mdhibiti aweze
kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kusimamia ushindani kwa ufanisi na
kutenda haki ni lazima awe huru. Uhuru unamwezesha kupima katika mizania haki
za mtumiaji wa huduma au bidhaa, haki za mtoa huruma au mzalishaji na muuzaji
wa bidhaa, gharama za kutoa huduma, gharama za kuzalisha bidhaa na kuzisambaza,
kudhibiti mwenendo wa bei ya huduma hizo au bidhaa hizo kwa mtumiaji na
kuhakikisha sera za nchi zinafuatwa na sheria na taratibu zinatekelezwa.
Mwandishi anafafanua vizuri zaidi juu ya uhuru huu wa mdhibiti katika kitabu
chake. Kwa kukisoma, mtu ataelewa vizuri juu ya uhuru wa mdhibiti na kwamba: “
Katika kurekebisha hali hii ya kumpa Mdhibiti uhuru wa kutosha wa kutenda kazi
kwa misingi ya haki bila woga, sheria zote zinazoanzisha mamlaka za udhibiti
zinampa Waziri uwezo wa kusimamia mamlaka hizi kisera na kiutawala tu na sio
katika masuala yaliomo ndani ya himaya ya Mdhibiti...” ( Uk 21).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Dhana muhimu ya uhuru wa
Mdhibiti inadhihirika pale ambapo muhula wa kazi wa bodi unalindwa kisheria na
taratibu za uteuzi wa bodi na ofisa mtendaji mkuu zinatambuliwa kisheria.<span> </span>“Sheria zote zinazoanzisha vyombo vya
udhibiti Tanzania zinaunda Kamati ya Uteuzi (Nominations Committee). Kamati hii
si kamati ya kudumu. Inakutana pale tu inapohitajika kupendekeza majina ya
uteuzi wa mjumbe au wajumbe wa bodi pamoja na ofisa mtendaji mkuu wa mamlaka ya
udhibiti... Kamati huwa chini ya uenyekiti wa katibu mkuu wa wizara ya kisekta
inayomsimamia Mdhibiti. Sheria pia zinafafanua sifa na aina ya wajumbe wa
kamati ya uteuzi, ikisisitizwa kuwepo kwa mwakilishi wa sekta binafsi..” (Uk
23).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika sehemu hii,
mwandishi ameelezea vizuri uhuru wa mdhibiti na sheria zinazompatia uhuru huo
na kuulinda. Pia, hapa anatuelezea Uhai wa Bodi, mfano kwamba “ ... kwa mujibu
wa sheria ya TCRA, sheria Na.12 ya 2003, Mwenyekiti wa bodi anateuliwa kwa
muhula wa miaka (4),Makamu wa Mwenyekiti muhula wake ni miaka mitatu na wajumbe
wengine wawili kipindi chao ni miaka mitano” (Uk 26).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Kwa mamlaka zote,
mjumbe wa bodi akimaliza muhula wake anaweza kuchaguliwa tena kwa kipindi
kingine kimoja. Hawezi akazidisha mihula miwili. Vilevile, katika mamlaka zote,
mkurugenzi mkuu ambaye ndiye ofisa mtendaji mkuu, ni mjumbe wa bodi kwa wadhifa
wake...” (26). Katika sehemu hii mwandishi anaelezea<span> </span>vizuri uzoefu uliopo, mfumo ulivyo juu ya
uhai wa bodi. Hivyo mtu akijisomea mwenyewe kitabu hiki atapata ujuzi na uelewa
mpana juu ya suala zima la udhibiti, uteuzi wa bodi na uhai wa bodi hizi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya tatu ya kitabu
hiki inajadili juu ya<span> </span>Maeneo<span> </span>Muhimu ya udhibiti, Leseni, Kudhibiti
Mwenendo wa Bei na Tozo Mbalimbali na mwongozo wa maadili. “ Sheria
zilizoanzisha mamlaka za udhibiti Tanzania zimeainisha maeneo muhimu matatu
ambayo mamlaka zinatakiwa kisheria, kufanya uchunguzi wa kina, wa wazi, na
unaohusisha wadau na wananchi kwa ujumla (taftishi) . Maeneo hayo yanahusu:
Kutoa leseni, kuongeza muda wa leseni au kufuta leseni ambazo mdhibiti ana
uwezo wa kufanya hivyo; Kudhibiti mwenendo wa bei ya bidhaa na /au huduma
zinazotolewa katika sekta inayodhibitiwa; na kupitishwa kwa kanuni za maadili
(code of conduct)” (Uk 33). Hayo yote yaliyotajwa hapo juu yanajadiliwa kwa
ufasaha mkubwa katika kitabu hiki.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya nne ya kitabu
hiki inajadili Uwezo wa kifedha wa Mdhibiti: “Kutokana na yaliyoelezwa mpaka
sasa, ni dhahiri mdhibiti ana madaraka na mamlaka makubwa, na hali kadhalika
ana dhamana kubwa aliyopewa na Taifa kupitia sheria za kisekta na sheria
zinazoanzisha vyombo vya udhibiti. Ana uhuru mkubwa katika masuala na maamuzi
yanayohusu udhibiti. Mamlaka, madaraka, dhamana na uhuru huo unaweza
kudhihirika pale tu ambapo mdhibiti ana uwezo wa kujiendesha; na pale
upatikanaji wa rasilimali fedha na rasilimali watu unatabirika ili aweze
kuendesha shughuli zake. Vinginevyo atakwazwa katika utekelezaji shughuli
zake...” (Uk 39).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Katika sehemu hii
mwandishi anaelezea jinsi mdhibiti anavyopata fedha za kujiendesha na ni
kutokana na:</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">- Ada zinazolipwa kwa
mdhibiti ikiwa ni pamoja na ada za kudurusu au kutoa leseni;</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">- Tozo mbalimbali kutoka
kwa wazalishaji na/au watoa huduma; na</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">- Misaada ya aina
mbalimbali au michango inayoweza kutolewa kwa Mdhibiti.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mfano: “ Mapato ya EWURA
kwa kiwango kikubwa yanatokana na tozo ya udhibiti (regulatory levy) ambayo
wadhibitiwa (regulated entities) wanatozwa kiwango kisichozidi asilimia moja
(1%) ya mapato ghafi, katika sekta za umeme, petroli, gesi asilia, maji na
uondoaji majitaka.” (45).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi, anaelezea
mapato ya mdhibiti, matumizi na sheria zinazoongoza kukusanya na kutumia mapato
haya. Mtu akijisomea kitabu hiki ataelimishwa kwa kina juu ya jambo hili
la<span> </span>uwezo wa kifedha wa mdhibiti.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya<span> </span>tano inajadili juu ya<span> </span>kuwalinda watumiaji wa huduma bidhaa
zinazodhibitiwa... “Pamoja na haki za mlaji au mtumiaji wa bidhaa kuwekwa
bayana kisheria, baina ya wadau wote wa udhibiti, mlaji au mtumiaji ndiye asiye
na nguvu na anaweza akaonewa. Hii inatokana na ukweli kuwa mlaji kwa kawaida
hajajipanga kutetea maslahi yake kama ilivyo kwa watoa huduma na wazalishaji.
Jamii imelitambua hilo na kuanzisha mifumo mbalimbali ya kisheria kutambua
makundi au vikundi vya watumiaji. Katika nchi zilizoendelea, vikundi vya hiari
vya watumiaji wa huduma vina nguvu na ushawishi mkubwa. Hata katika nchi hizo
bado imewekwa mifumo rasmi ya kupokea na kushughulikia kwa haraka kero na
migogoro inayoweza kuadhiri utoaji wa huduma au inayotokana na haki kutotendeka
(Ombudsman)” (uk 49)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Katika nchi
zinazoendelea, Tanzania ikiwa ni mfano, hakuna vyama vya hiari
vinavyounganisha<span> </span>watumiaji wa huduma au
bidhaa ambavyo vingeweza kutetea kundi hilo la jamii katika sekta
inayodhibitiwa. Baada ya mjadala mrefu uliohusu uanzishaji wa mamlaka za
udhibiti, ilionekana vema yakaanzishwa mabaraza ya ushauri ya watumiaji wa
huduma zinazodhibitiwa (Consumer Consultative Councils- CCC). Mabaraza haya ni
EWURA-CCC, SUMATRA-CCC, TCAA-CCC, na TCRA-CCC, Pia, chini ya Sheria ya Fair
Competition Act limeanzishwa Baraza la watumiaji linaloitwa National Advocacy
Council (NCAC)” (Uk 49)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anaendelea
kufafanua zaidi kuhusu kuwalinda watumiaji wa huduma na bidhaa zinazodhibitiwa.
Msomaji wa kitabu hiki atapa hayo yote na kupata majibu ya maswali mengi ambayo
watu wamekuwa wakijiuliza kuhusu dhana nzima ya udhibiti wa huduma za kiuchumi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya sita, inajadili
muundo wa vyombo vya udhibiti. Hapa tunafahamishwa kwamba: “...mifumo ya vyombo
vya udhibiti ina mambo mengi yanayofanana. Hata hivyo, mfumo wa uchumi,
historia, ushirikiano wa kikanda, na ushirikiano wa kimataifa ni baadhi ya
vigezo vinavyotofautisha mfumo mmoja na mwingine” (Uk 54).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Hapa mwandishi anaelezea
mfumo unaotumika Tanzania. Faida na hasara zake. Na kulinganisha mfumo wetu wa
udhibiti na mifumo ya nchi nyingine. La kuzingatia hapa ni kwamba misingi ya
udhibiti inafanana na inakubalika kote duniani. Kwa mfano ukilinganisha mfumo
wa udhibiti wa Tanzania na Uingereza, tofauti<span>
</span>zake ni matokeo ya tofauti za mazingira ikiwa ni pamoja na historia ya
utawala, utamaduni, biashara, mazingira ya masoko, ushindani, na hali ya
uchumi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya saba inahusu
Uthibiti wa Sekta za Kiufundi. Hapa ndipo tunafafanuliwa juu ya mifano ya
udhibiti wa Masuala ya Kiufundi, Usimamizi wa Masafa ya Redio, Muunganisho wa
Mawasiliano na Namba za simu kama Rasilimali Muhimu.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Sekta ya mawasiliano
ina mifano mzuri inayohusu udhibiti wa masuala ya kiufundi. Ni sekta yeye
changamoto kubwa kwa wadhibiti. Kwani teknolojia katika sekta hii inabadilika
kwa kasi kubwa sana na kufanya<span>
</span>teknolojia ya miaka miwili au mitatu iliyopita kuwa ya kizamani”<span> </span>(Uk 62-63)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Usimamizi wa masafa ya
redio unahusu kuhakikisha matumizi bora ya masafa, kupunguza mwingiliano wa
masafa kwa watumiaji mbalimbali, kuhakikisha kwamba hakuna anayetumia masafa ya
redio bila kuruhusiwa kisheria, na kwamba aliye na leseni ya kutumia masafa ya
redio anayatumia vizuri na kwa mujibu wa masharti yaliyo katika leseni...” (uk
63)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anaelekea kwa kirefu
juu ya muunganisho wa mawasiliano. Anaelezea jinsi muunganisho wa mawasiliano
unavyorahisisha mawasiliano ya kampuni mbali mbali za simu. Anatoa mfano
muunganisho wa mawasiliano baina ya TTCL, Vodacom, Tigo, Airtel, Zantel,
Sasatel na kampuni nyingine.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">“Suala la muunganisho
linapohusu mawasiliano ya kimataifa linasimamiwa na Umoja wa Simu Duniani (ITU)
kama mdhibiti wa kimataifa wa mawasiliano. Usimamizi huo unahusu makubaliano
yavifaa, viwango vya huduma na miongozo kuhusu malipo” (65).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia katika sura hii ya
saba, mwandishi anaelezea juu ya namba ya simu kuwa rasilimali muhimu: “ Namba
ya simu huwezesha mteja kutambulika mahali ilipo</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kijiografia; kampuni
ambayo yeye ni mteja kujulikana; mteja kuunganishwa na mtumiaji mwingine wa
simu katika eneo lake na eneo la mbali na hata nje ya nchi. Namba ya simu kwa
mpangilio wake humwezesha mitambo kutambua chanzo cha simu na kuiwezesha
mitambo hiyo kuielekeza kwenye kituo au vituo vya mpito mpaka kumtambua na
kumfikia mlengwa” (Uk 67)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kuhusu namba ya simu na
udhibiti, mwandishi anafafanua hivi: “ Namba za simu ni rasilimali ambayo iwepo
itahodhiwa na kampuni moja, itakuwa sirahisi kampuni hiyo kugawa rasilimali
hiyo kwa kampuni nyingine, na hivyo kuzuia ushindani na kuongeza gharama kwa m
teja wa simu. Kabla ya kufungua sekta ya mawasiliano ya simu na kuruhusu ushindani,
TTCL ilikuwa ndiyo pekee iliyopanga na kutoa namba za simu. Baada ya soko la
mawasiliano kuwa huru, jukumu la kupanga na kusimamia namba za simu limekuwa ni
jukumu halali la Mdhibiti wa mawasiliano ya simu” (Uk 68).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi, kwenye sura
hii anaendelea kuelezea umuhimu wa namba ya simu, jinsi zinavyopangwa, namba za
kila nchi na namba ya kila mteja. Kusema kweli hapa anatupatia elimu ambayo
wengi wetu hatukuwa nayo.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya nane, mwandishi
anatuelezea uhusiano uliopo kati ya serikali na mdhibiti. “Changamoto kubwa inayomkabili
Mdhibiti yeyote hasa katika nchi zinazoendelea ni uhusiano wake na Serikali.
Katika mazingira ya kawaida, changamoto hii haipaswi kumpa shida Mdhibiti au
kuisumbua serikali. Kwanza, ili Mdhibiti awepo kisheria, ni Serikali ambayo
inamwanzisha. La, pili na la muhimu ni madhumuni ya kuanzishwa kwa Mdhibiti na
majukumu ambayo anapewa kisheria. Madhumuni makubwa ni kuhakikisha kwamba
maisha ya wananchi yanaboreshwa. Madhumuni haya ndiyo yanayoifanya Serikali
iwepo. Madhumuni haya hayawezi kuwa chanzo cha mgogoro kati ya serikali na
Mdhibiti...” (70)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa maoni ya mwandishi
ni kwamba sheria zikifuatwa na kila mtu akajua mipaka yake, haiwezekani hata
kidogo pakatokea changamoto kati ya Mdhibiti na Serikali. Lakini: “ Katika nchi
kama Tanzania, mara nyingi hutokea kutokuelewana kati ya Serikali na mdhibiti
hususan pale ambapo mwekezaji, au mtoa huduma anapoona kwamba kwa kupitia
maamuzi yake mdhibiti, hataweza kuyapata yale anayoyataka na hasa katika
kipindi alichojiwekea. Anakuwa hapendi ushindani huru, na kwa hakika huyu si
mwekezaji mwenye tija...”</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anatoa mifano
kuonyesha changamoto zinazojitokeza kati ya mdhibiti na serikali ya Tanzania: “
Mawasiliano na makubaliano kati ya<span>
</span>Wizara ya Nishati na Madini na Songas yalikuwa ni njia ya kujaribu
kukwepa udhibiti wa EWURA. Kama hii haitoshi, na kwa kuwa EWURA ilishikilia
msimamo wake wa kuhakikisha Songas haikiuki maagizo ya kiudhibiti, Kampuni ya
Songas ilifungua kesi kwenye Baraza la Ushindani (FCT). Katika tukio ambalo
halitarajiwi kwenye utawala bora, Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO
waliamua kuisaidia Songas katika kesi yake dhidi ya EWURA ingawaje EWURA kwa
wakati ule ilikuwa inatetea maslahi ya Taifa. Ikumbukwe pia kwamba waziri wa
Nishati na Madini ni waziri msimamizi wa sekta ya nishati kwa mujibu wa Sheria
ya EWURA, Sura ya 414 ya Sheria za Tanzania. TANESCO ilikwenda mbali zaidi na
kuomba kuunganisha katika kesi hiyo kama mlalamikaji, yaani ikiungana na Songa
dhidi ya EWURA katika shauri lililofunguliwa kwenye Baraza la Ushindani, ombi
hilo lilikataliwa. Hata hivyo, mwezi Desemba 2009, Songas iliondoa mashitaka
yake kabla hayajasikilizwa” (Uk 74)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pamoja na mfumo mzuri
unaoeleweka kama huu wa udhibiti, bado kuna changamoto na mgongano. Labda ni
kwa vile mambo haya yalikuwa hayajafafanuliwa vizuri kama alivyofanya mwandishi
wa kitabu hiki. Kwa mfano, mwandishi anaelezea vizuri nafasi ya waziri na
katibu mkuu katika mfumo huu wa udhibiti na kuonyesha wazi kwamba kila mtu
akifuata wajibu wake vizuri katika mfumo huu ni vigumu kabisa kutokea mgongano.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya tisa mwandishi
anafafanua kwa kina juu ya udhibiti na ushindani wa biashara. Na hapa ndipo
tunatambua utaratibu wa kumlinda mlaji na mtoa huduma na uhusiano wa udhibiti
wa huduma na wa biashara.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anatoa
historia ya chanzo cha kumlinda mlaji na mwongozo wa ushindani. Mfano hapa
Tanzania “ Ili kusimamia, kukuza, na kulinda ushindani wa haki katika biashara,
na kuwalinda walaji dhidi ya mwenendo wa soko usio na haki, ilitungwa sheria ya
Ushindani wa Haki ya mwaka<span> </span>2003 (Fair
Competition Act, 2003). Sheria hii imeanzisha vyombo viwili vya kutekeleza azma
ya Serikali ya kusimamia biashara ya haki vyombo hivi ni Tume ya ushindani
(FCC), na Baraza la Ushindani (FCT). FCC inashughulikia udhibiti wa mwenendo
unaokwaza au unaozuia ushindani wa kibiashara (anti-competitive conduct).” (Uk
84).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi, mwandishi
anafafanua na kuelezea kwa kina juu ya sheria za kisekta, taratibu, maagizo na
miongozo ya kisheria.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi na moja
inaelezea vizuri uhusiano kati ya Bunge na Mdhibiti: “ Kwa upande wa Bunge,
Mdhibiti anawajibika kwa njia moja iliyo dhahiri ambayo pamoja na uhuru alionao
hawezi kukwepa. Fedha anazokusanya na kuzitumia Mdhibiti ni fedha za umma. Kwa mantiki
hiyo, hesabu zake za mapato na matumizi hukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Serikali (CAG). CAG anatakiwa kuwasilisha ripoti ya ukaguzi wa hesabu hizo
kwa Rais na baada ya hapo kupitia waziri mwenye dhamana ya fedha, ripoti hiyo huwasilishwa
Bungeni...”</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi anaendelea
kufafanua zaidi juu ya uhusiano uliopo kati ya mdhibiti na Bunge, hivyo kwa
kukisoma kitabu hiki, msomaji atajipatia elimu zaidi juu ya suala zima la udhibiti
wa huduma za kiuchumi Tanzania.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi na mbili,
mwandishi anaelezea na kufafanua udhibiti katika nchi nyingine. Hapa
tunaelimishwa jinsi nchi nyingine zinavyofanya katika suala zima la udhibiti.
Changamoto na mafanikio katika nchi nyingine. Hii inatufumbua macho na kutambua
kwamba si Tanzania peke yake inatumia mfumo huu wa udhibiti wa huduma za
kiuchumi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi na tatu,
mwandishi anajadili masuala mtambuka, kama vile kupima ubora wa udhibiti,
udhibiti wa utawala bora, kupima ufanisi wa udhibiti na uthibiti wa sera za
kitaifa.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi na nne,
mwandishi anaelezea juu ya mafanikio na changamoto za udhibiti katika kusimamia
utekelezaji wa sheria, utoaji wa Leseni, sekta ya mawasiliano, sekta ya maji,
sekta ya umeme, sekta ya uchukuzi, sekta ya mafuta ya petroli na watumiaji wa
huduma za kiuchumi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sura ya kumi na tano ni
hitimisho: “ Kwa kuhitimisha, inatarajiwa kwamba huko utendako udhibiti
hautahusika tu na fikra finyu ya udhibiti wa kiufundi. Tasnia ya udhibiti itapimwa,
pamoja na mambo mengine, kwa jinsi uwepo kwake kutakavyokuwa kumechochea kasi
ya kukua kwa uchumi wa nchi. Ili iweze kufanikisha jukumu hilo, lazima tasnia
ya udhibiti iwe wakala wa mabadiliko ya mtazamo katika jamii, mabadiliko<span> </span>yanayozingatia uaminifu, uwajibikaji, utawala
bora, utawala wa sheria, amani, usalama, haki za binadamu, demokrasia, na
wajibu wa kulinda kushirikisha jamii zisizojiweza katika maendeleo” ( Uk 140)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Sehemu ya mwisho ni
marejeo.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">V. TATHIMINI YA KITABU.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nianze kwa kumpongeza Profesa
Mark Mwandosya <span> </span>kwa kazi hii nzuri sana
aliyoiandika. Kusema kweli kazi hii inafundisha na kufumbua macho. Tulikuwa
tukisikia EWURA, lakini hatukufahamu kwa undani hiki ni kitu gani. Wengine
walifahamu kidogo, lakini hawakuwa na uelewa mpana na elimu ya kutosha juu ya
chombo hiki. Sasa kwa kusoma kitabu hiki watafahamu zaidi. Tumekuwa tukisikia
SUMATRA, lakini hakuna aliyetambua maana yake, zaidi ya kuchukiwa na wenye
daladala na wasafiri. Kwa wengine SUMARA, ilikuwa ni kero na kuchukuliwa kwa
kusema kwamba hii ni miradi ya wakubwa. Kwa ufafanuzi uliotolewa kwenye kitabu
hiki, wale watakao soma kitabu hiki, wataelewa vizuri na hawezi hata siku moja
kuibeza na kuichukia tena SUMATRA.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pili, nimpongeze
mwandishi wa kitabu hiki kutumia lugha ya Kiswahili kuandika kitabu hiki.
Imekuwa ni tabia ya wasomi wetu kuandika kwa lugha za kigeni na kuifanya elimu
kuwa ni faida wanayoipata <span> </span>wachache. Kwa
kuandika kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, watu wengi watakisoma na kuipata
elimu hii.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tatu, ni kumshukuru kwa
kuandika. Wanasiasa wetu wanapenda kuhubiri na kupiga siasa za maneno bila
kuandika. Viongozi ambao wanapata uzoefu mkubwa kwa kutunga sera na sheria, na
baadaye kusimamia utekelezaji wa sera hizo na sheria hizo, hawafanyi kazi
kuandika ili uzoefu wao uwe na faida leo, kesho, keshokutwa na siku zijazo.
Profesa Mwadosya amefanya kazi hii kubwa kama anavyosema yeye mwenyewe: “
...wazo la kuandika kitabu hiki ni na chimbuko lake ni mazungumzo niliyoyafanya
na wenzangu wawili: Ndugu Haruna Masebu, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti
wa Huduma za Nishati na Maji; na Profesa John Nkoma, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
ya Udhibiti wa Mawasiliano. Mazungumzo haya yalifanyika ofisini kwa Waziri wa
Maji na Umwagiliaji, Ubungo, Dar-es-Salaam, tarehe 7 Septemba 2009. Sote, kwa
nafasi zetu tofauti, tulikuwa tumehusika katika mijadala ya kisera, kuandaa miswada
ya sheria na kuanzisha mamlaka za udhibiti. Baada ya mjadala mrefu, tukakubaliana
kwamba njia pekee ya kuwa na mchango wa kudumu kwa Taifa, ni kwa kila mmoja
wetu katika nafasi yake kuweka katika maandishi, uelewa na uzoefu tulioupata,
tukiamini kwamba uelewa na uzoefu huo utakuwa wenye manufaa katika usimamizi wa
uchumi ,kwa zama hizi, na rejea muhimu kwa zama zinazokuja” ( xviii – xix)</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nne, ni kumshukuru
mwandishi jinsi alivyofafanua Udhibiti, historia yake, sera yake na<span> </span>sheria zake. Kusema ukweli, baada ya kukisoma
kitabu hiki mtu anakuwa na ufahamu mpana juu ya suala hili la udhibiti. Ni
vigumu kabisa baada ya kukisoma kitabu hiki mtu akapinga suala hili.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tano, ni kumshukuru
mwandishi, ambaye ni mwanasiasa na kada wa chama tawala kukumbuka usomi wake,
na kuandika kitabu hiki “Kisomi” bila kutawaliwa na “upepo” wa siku hizi wa
kushabikia vyama vya siasa hata pale ambapo si nafasi yake. Mwandishi ameandika
kitabu hiki kwa watanzania wote bila kuangalia itikadi za siasa, maana ustawi
wa jamii na maendeleo ya watanzania ni ya wote na wala hakuna itikadi.
Ameandika kitabu chake, neno la kwanza hadi la mwisho bila kutaja CCM. Hii si
kawaida kwa kada wa<span> </span>chama kwa utamaduni
uliojengeka. Angeweza kusema kwamba udhibiti ni sera iliyoanzishwa na chama cha
mapinduzi. Angeweza kukitukaza chama chake kwa mafanikio hayo, kama tulivyozoea,
lakini Profesa Mwandosya, ameonyesha kuvuka mipaka ya “Uchama”; wakati huu
ambapo taifa letu linaelekea kuchanganyikiwa na kuingia kwenye mapambano ya
vyama vya siasa; tunawahitaji watu kama Profesa Mwandosya, ili waweze
kuturudisha kwenye njia sahihi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">VI. HITIMISHO.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kama kawaida yangu,
ningependa kuwashauri watanzania kukitafuta kitabu hiki na kukisoma. Wasiishie
kusoma uchambuzi huu kwenye gazeti. Huu ni uchambuzi mfupi na kitabu ni kikubwa
zaidi na kimesheheni mambo mengi ambayo nimeyagusia kidogo tu. Ni imani yangu
kwamba kwa kukisoma kitabu hiki watajifunza mengi kutoka kwenye kitabu hiki na
hasa juu ya ufafanuzi wa udhibiti na mambo mengine kama EWURA,SUMATRA<span> </span>na mengine kama hayo ambayo kwa kiasi kikubwa
yalikuwa ni msamiati kwa wananchi wengi.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwandishi ameonyesha
wazi kwamba Tanzania bado haina sera ya kumlinda mtumiaji wa huduma za kiuchumi.
Na kuonyesha wazi kwamba hakuna popote mtumiaji anaposhirikishwa katika
uanzishwaji wa vyombo hivi vya udhibiti kama vile EWURA na SUMATRA. Hivyo ni
muhimu hili kuzingatiwa ili itungwe sera ya kumlinda mtumiaji na ushirikishwaji
wa watumiaji katika mfumo mzima wa<span>
</span>udhibiti.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Dokezo la mwandishi
kwamba<span> </span>“ Katika hali ya kawaida vyombo
vya udhibiti vingeanzishwa kwanza kabla ya zoezi la ubinafsishaji. Ingekuwa
vema pia iwapo zoezi la ubinafsishaji lingekwenda sambamba na uanzishwaji wa
vyombo vya udhibiti...” (Uk 4) ni la kuzingatiwa, ingawa lilifanyika kinyume,
lakini jitihada zinaweza kufanyika, hasa kwa kuwaelimisha watu juu ya mfumo huu
wa udhibiti, kama mwandishi alivyofanya kwenye kitabu chake. Udhibiti usibaki
ni “fumbo” au chombo cha kunyanyasa pande zote mbili, watoa huduma na
watumiaji.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Pia, ni muhimu
kuzingatia maneno yanayotolewa na mwandishi kwenye kitabu chake kama vile : “
Mamlaka za Udhibiti huwajibika kwa maamuzi yake, lakini pasipo na changamoto
chanya baina ya serikali, Mamlaka za Udhibiti na watoa huduma, maendeleo
hayawezi kupaikana”(Uk 100). Na “ Pamoja na uhuru wa Mdhibiti, ili aweze
kufanikiwa ni muhimu Mdhibiti akayaelewa mazingira ya kisiasa” (Uk 100).</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa upande wake Profesa
Mwandosya, amefanya kazi yake. Ametuelezea umuhimu wa kuwa na mfumo wa udhibiti
na jinsi mfumo huu unavyopaswa kufanya kazi. Amedokeza changamoto na baadhi ya
mafanikio. Mtu mwingine anaweza kuanzia hapa na kuandika juu ya mafanikio ya
mfumo huu, je unafanya kazi, je ni kitu gani kinakwamisha mfumo huu? Je ni
kuingiza siasa katika utendaji au ni watu kutotambua nafasi zao au ni watu
kutofahamu mfumo wenyewe. Bado kuna kazi kubwa kwa upande wa wachambuzi, watoa
huduma na watumiaji.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44214" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44213" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus
Karugendo.</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44210" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44209" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44205" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44208" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><a href="mailto:pkarugendo@yahoo.com" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44207" rel="nofollow" target="_blank">pkarugendo@yahoo.com</a></span></div>
<div class="yiv3612888677MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_44203" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-58014333143698849232013-12-10T00:09:00.003-08:002013-12-10T00:09:52.022-08:00Picha ya Urais<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43389" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43388" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">SURA YA URAIS INAFANA VIPI NA UWAZIRI JE?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43394" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43392" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43391" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kama maneno haya yangetamkwa na mtu ninayemdharau, mtu ambaye si mzalendo
na akili yake ina kasoro kidogo, nisingepoteza muda wangu kuandika. Kwa vile ni
maneno haya yalitamkwa <span> </span>na mtu
ninayemheshimu, tena kijana msomi, ni lazima niandike na kukaripia kwa nguvu
zangu zote. Waswahili wanasema tusipoziba ufa tutajenga ukuta. Na kwamba rafiki
wa kweli ni yule anayekueleza ukweli. Rafiki mbaya ni yule mnafiki anayekusifia
wakati akijua anakudanganya. Labda nianze na swali: Sura ya “Urais” inafanana
vipi na sura ya “Uwaziri” inafanana vipi? Je urais ni mashindano ya urembo?
Tunaongozwa na sura au tunaongozwa na akili, hekima na busara? Rais wa Kenya,
Mheshimiwa Uhuru Kenyatta, alipoulizwa akienda kwenye mahakama kule Holland,
nchi ataiongozwa vipi, alijibu kwamba kuna twiter. Je tunahitaji sura ipi ya
kutumia twiter? Au tunahitaji sura ipi ya kuweka misingi ya utawala bora,
demokrasia na kufuata katiba ya nchi? Ni sura ya namna gani hiyo?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43398" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43397" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mheshimiwa Januari Makamba, amesikika akiwahutubia vijana wa CCM kule Misenyi
Kagera kwamba, CCM, bado ina nafasi kubwa ya kuliongoza taifa letu, maana
akiangaza kwenye vyama vya upinzani haoni mtu yeyote mwenye sura ya Urais na
hakuna mtu mwenye sura ya uwaziri. Kwamba vyama vya upinzani ni wanaharakati
tu! Hakuna historia ya wanaharakati kuongoza nchi?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43401" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43400" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ninajua kwamba Januari ni kada wa chama cha Mapinduzi, na yuko kwenye uongozi
wa juu kwenye chama chake hicho, lakini sikutegemea kama angeweza kutoa
matamshi kama haya ambayo yanaturudisha nyuma kabisa wakati wa utawala wa
kifalme. Enzi ambazo uongozi ulitegemea familia na damu ya watu wateule. Hata
kama ungekuwa na akili za kupindukia, bila kuzaliwa kwenye ukoo wa kifalme
usingepata nafasi ya uongozi. Lakini leo hii wakati wa demokrasi, wakati wa
vyama vingi, wakati wa kuwaingiza viongozi madarakani kwa kura, mtu anaweza
kuongea juu ya sura ya Urais na sura ya uwaziri? Huku ni kwenda mbele au ni
kurudi nyuma? Haya ni maneno ya kutamkwa na kijana au mzee ambaye anakaribia
kumaliza maisha yake hapa duniani?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43404" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43403" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tunaweza kusema kwamba labda Mheshimiwa Makamba, alikuwa anatoa vijembe vya
kisiasa. Hili linawezekana na wala sina matatizo yoyote , lakini si Makamba,
tunayemfahamu. Tunamfahamu Januari Makamba, mtu mwenye busara na hekima, mtu
anayepima kila neno analotaka kusema. Mtu ambaye zaidi ya miaka minne, alikuwa
msaidizi wa Mheshimiwa Rais<span> </span>Jakaya
Kikwete, akiandaa hotuba zake. Huyu si mtu wa kuropoka tu, ni mtu makini.</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43407" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43406" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Vijembe kama vijembe, sina matatizo navyo. Angesema haoni mtu mwenye uwezo
wa kuongoza nchi kwenye vyama vya upinzani, tungecheka tu na kufurahia
vijembe<span> </span>vyake, maana baada ya hotuba
yake tungempelekea orodha ndefu ya watanzania wenye uwezo mkubwa kuongoza ambao
si wanachama wa CCM, tungempelekea orodha ndefu ya watu wenye busara, hekima na
kipaji cha hali ya juu kuongoza hata kwa viwango vya kimataifa. Tatizo langu
kubwa ni pale anaposema, upande wa wapinzani haoni mtu mwenye “Sura” ya “Urais”
na mwenye “Sura” ya “Uwaziri”. Sura hizi nzuri ziko CCM. Hizi ni sura gani?
Maana kama hizo “sura” zinaendana na uongozi, basi Tanzania tungekuwa mbali;
tusingekuwa na ufisadi wa kutisha; wimbo wa ufisadi hata mtoto aliyezaliwa leo
anaufahamu, hivyo si lazima kutoa mifano</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43411" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43410" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mtu, tunayemheshimu kama Januari Makamba, akiacha kuona matatizo ya taifa
letu, akaacha kuona changamoto ya Katiba, changamoto ya muungano wetu,
changamoto ya kufuata na kutekeleza mfumo wa demokrasia katika taifa letu,
changamoto ya kuondoa umaskini, changamoto ya kupambana na rushwa na ufisadi,
changamoto ya kupambana na bidhaa bandia, changamoto ya kupambana na madawa ya
kulevya, changamoto ya kuondoa msemo wa “ Tutawasaka popote walipo na
kuwafikisha mbele ya sheria”: Tulisikia hivyo kwa Ulimboka, Kibanda, Mwangosi,
Kamanda Barlow,<span> </span>Mabomu ya Arusha, Mauaji
ya Padri wa Zanzibar na Sasa wasichana Wazungu wamemwagiwa tindikali. Hakuna
anayekamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.. ni misemo ya kutowajibika! “Tutawasaka
popote walipo na kuwafikisha mbele ya sheria”. Badala ya<span> </span>kupambana na kutowajibika na uzembe mwingine
katika taifa letu, Januari Makamba, anatwambia “Sura”. Sura inaweza kupambana
na changamoto zote hizo hapo juu?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43414" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43413" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Uongozi ni mashindano ya urembo? Kwamba mtu kabla ya kugombea ahakikishe
anajipamba na kujiremba, kujifunza namna ya kutembea na kuongea kwa madaha?
Uongozi unategemea sura ya mtu? Kwamba awe na sura nzuri? Kusema kwamba vyama
vya upinzani havina mtu mwenye sura ya urais, maana yake hakuna mwenye sura
nzuri au sura ya urais inafanana vipi? Uongozi ni sura au ni akili, busara na
hekima? Uongozi ni mtu kuwa na fikra pevu au kuwa na sura ya kuvutia?</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43417" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43416" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tanzania, sasa hivi iko njia panda na tunapita kwenye kipindi cha mpito. Ni
wakati ambapo tunahitaji kiongozi mwenye upeo mkubwa, kiongozi mwenye akili
nzuri, kiongozi ambaye hafungamani na upande<span>
</span>wowote ule, kiongozi ambaye hafungamani na imani za kidini, kiongozi ambaye
hafungamani na “Upuuzi” wa ushabiki wa vyama vya siasa. Tunahitaji kiongozi
aliyejikomboa kutoka kwenye minyororo ya ukabila na ukanda. Tunahitaji kiongozi
anayeangalia Tanzania kwa umoja wake; kiongozi mzalendo anayeheshimu haki za
binadamu na usawa wa kijinsia. Tunahitaji Kiongozi anayeguswa na matatizo ya
watanzania wote. Nina mashaka makubwa kama sifa hizo hapo juu zinaendana na
sura ya mtu.</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43436" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43435" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ubaguzi wa hatari kubwa katika dunia yetu hii, ni kuwadhamini watu kwa
kuangalia sura zao, kuangalia rangi ya ngozi, kuangalia pua na nywele, ufupi na
urefu, unene na wembamba. Leo hii utasema hawana sura ya urais, kesho utasema
hawana sura ya “utanzania”, kesho kutwa utasema hawana sura “ukabila” na hasa
kabila lako. Na mwisho utasema hawa si wenzetu! Na matokeo yake ni mapambano ya
kutisha ambayo sina haja ya kutoa mifano, maana sote tunaifahamu. Ubaguzi wa
sura ni hatari na si wa kushabikia. Kama Mheshimiwa Januari Makamba, ni
muungwana na analitakia taifa letu mema, asimame na kuomba msamaha kwamba
maneno yale kule Misenyi, alimponyoka na ulimi uliteleza. Tutaelewa na
kumsamehe, vinginevyo anajiweka kwenye kapu la watu wa kuogopwa katika taifa
letu.</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43431" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43433" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mategemeo makubwa ya taifa letu ni vijana wetu. Lakini kama vijana wenyewe
wanaanza kuchanganyikiwa kiasi cha kuchanganya uongozi na sura, badala ya
kuuona mnyororo wa uongozi ambao ni akili, hekima, busara na uzalendo, ni hali
ya hatari. Ni lazima sote kwa pamoja kushirikiana kuliokoa taifa letu,
tukiendeleza ushabiki wa “Kipuuzi” na kuendelea kuamini kwamba kuna watu
wateule waliozaliwa kuongoza au kuishi maisha bora zaidi ya wengine,
tutaliangamiza taifa letu badala ya kuliokoa.</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43429" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv9637532934MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43425" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_43427" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-47278105066463882622013-12-10T00:07:00.003-08:002013-12-10T00:07:26.475-08:00Ushoga<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40992" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40994" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">USHOGA NA USAGAJI, PAPA HANA MSIMAMO MPYA.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40982" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40981" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Papa Francis wa Kanisa Katoliki Duniani, akiwa Brazil, alitoa matamko
kuhusu ushoga na usagaji na baadhi ya watu wakafikiri amekuja na msimamo mpya
na labda kuonyesha kuunga mkono Ushoga na usagaji. Alisema: “ Kwa kuwa
watangulizi wangu walikua na msimamo mkali dhidi ya watu Mashoga na suala zima
la ushoga na mimi nasema ushoga ni dhambi na chukizo kubwa mbele ya Mungu na
Binadamu... Mimi nani hadi nitoe hukumu dhidi ya watu hao, kwani Yesu mwana wa
Mungu alifundisha ya kwamba usimhukumu mtu yeyote kwani na wewe utakuja
kuhukumiwa”.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40977" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40979" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Huu si msimamo mpya hata kidogo. Tumekuwa tukiandika na kuelezea jambo
hili. Kwamba ni wazi ushoga na usagaji ni dhambi na ni kitu kisichokubalika.
Lakini ukweli ulio mbele yetu ni kwamba watu hawa wanaishi miongoni mwetu. Tuwasikilize,
tuwashauri na kuwabadilisha kutokana na hali yao hiyo. Kuwatenga na kuwalaani
haisaidii.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoBodyText" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40975">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40974" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tarehe 1Oktoba 1986 Kadinali Ratzinger (Papa
Benedict wa 16 aliyestaafu), alitoa mwongozo wa Kanisa Katoliki juu ya watu
wanaovutiwa na jinsia zao (homosexuality). Mwongozo huu ilikuwa ni barua
aliyowaandikia Maaskofu wote wa Kanisa Katoliki:</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40972" style="text-align: justify;">
<b id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41005"><i id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41004"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41003" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“ON THE PASTORAL CARE OF HOMOSEXUALS”.</span></i></b><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_40971" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> Katika barua hii Kadinali Ratzinger, aliwakumbusha maaskofu juu ya
mwongozo mwingine kuhusu swala hili hili uliotolewa Desemba 1975: <b id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41007"><i id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41009">“
Declaration of Certain Questions Concerning Sexual Ethics”</i></b> uliosisitiza
kwamba hali ya mtu kuvutiwa na jinsia yake ifanyiwe utafiti na ichukuliwe kwa
uangalifu na busara.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41012" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41011" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Katika barua hiyo
Kadinali Ratzinger, aliwashauri maaskofu kwamba hali ya mtu kuvutiwa na jinsia
yake inahitaji wachungaji (mapadri) wenye kufanya utafiti kwa uangalifu mkubwa,
wenye kujali, wa kweli na wenye theolojia isiyokuwa ya msimamo mkali.</span><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"></span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41015" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41014" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ingawa Kadinali
Ratzinger, anapinga hali hii na kuiona kama hali<span> </span>Fulani ya ugonjwa na kufanya mambo kinyume na
maumbile, anashauri watu wenye matatizo ya kuvutiwa na jinsia zao wasitengwe.
Wapatiwe huduma za kiroho, washauriwe na kuvumiliwa hadi pale watakapobadilika.
Anasema wachukue njia ya msalaba. Wakubali kuwekwa msalabani na kufa na
kufufuka kama alivyofanya Yesu Kristu. Wazaliwe upya na kupata maisha mapya.
Anakubali kwamba ni kitu kigumu mtu kuachana na tabia yake aliyozaliwa nayo,
lakini hiyo ndiyo njia ya msalaba. Si jinsi mtu anavyotaka yeye bali ni jinsi
anavyotaka Mwenyezi Mungu!! Ni wangapi wanaukubali ukweli huu wa maisha ya
msalaba? Huu ni wajibu wa wakristu wote si wale tu ambao miili yao
inawalazimisha kuvutiwa na jinsia zao wenyewe!</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41018" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41017" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><span> </span>Hapa ndipo kuna
tofauti kidogo. Wakati Kadinali Ratzinger, aliuchukulia ushoga na usagaji kama
aina Fulani ya ugonjwa na ulemavu, Papa Francis, anakataa. Anasema si ugonjwa,
bali ni tabia ambazo mtu anajifunza na kuna uwezekano wa kuzikomesha tabia
hizi. Na kwa mapadri na watawa wanaojifunza tabia hizi ni kwamba: “
Wanachotakiwa ni kutubu na kusamehewa na kuacha dhambi hiyo mara moja na kurudi
kwenye maisha ya tawa waliokuwa nayo na kutimiza viapo walivyoapa katia kufanya
kazi yao ya kumtumikia Mungu maisha yao yote”</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41021" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41020" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Matendo ya ushogo na
usagaji si matatizo ya wakristu peke yao. Haya ni matatizo ya dunia nzima.
Hivyo kuyapinga ni lazima tuwe na misingi inayokubalika kwa watu wote. Ikibidi
na sayansi itumike. Kuipinga sayansi, ni sawa na uwenda wazimu – waliokataa
kwamba dunia haizunguki, sasa hivi wanajionea aibu kule kuzimu waliko. Si watu
wote wanaoamini kuumbwa kwa mwanamke na mwanaume kama kunavyoelezwa kwenye
Biblia. Hata hivyo si watu wote wanaoiamini Biblia. Dunia hii ina watu wangapi,
na ni kiasi gani imani yao imesimikwa kwenye biblia?</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41024" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41023" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Watu ambao imani yao
haiongozwi na biblia wanasema nini kuhusiana na ushoga na usagaji. Je sisi
Waafrika, kabla ya<span> </span>ujio wa hizi dini za
kigeni, tulikuwa na maadili gani juu ya hali mtu kuvutiwa na jinsia yake
mwenyewe. Kuna ushahidi wa utamaduni kama kula yamini miongoni mwa makabila
mbali mbali. Watu wa jinsia moja walikuwa wanapendana kiasi wanaamua kuungana
na kuwa kitu kimoja. Kuwa kitu kimoja maana yake nini? Ni kuunganisha mwili na
roho – jinsi mkono wako unavyozigusa sehemu zote za mwili wako, ndivyo na mkono
wa ndugu yako uliyeungana naye utakavyozishika na kuzigusa sehemu zote za mwili
wako,<span> </span>jinsi usivyokuwa na mipaka juu ya
mwili wako ndivyo hivyo hivyo hutakuwa na mipaka juu ya mwili wa ndugu yako
utakayeungana naye! Huu ni undugu au urafiki uliokuwa na masharti magumu kweli.
Ilikuwa ni kuungana katika taabu na katika raha, mfano rafiki wa kuchanjana,
akiugua na wewe unaugua, akifiwa na wewe umefiwa, akiwa na sherehe na wewe ni
sherehe yako, akakiugua ugonjwa wa ukoma huwezi kumtenga, akiugua ugonjwa wa
kifafa huwezi kumtenga, mke wake anakuwa mke wako, na watoto wako wanakuwa watoto
wake. Akikutembelea unahama chumbani kwako, unamwachia kitanda na mke wako! Ni
vigumu kusema kwamba katika<span> </span>uhusiano wa
namna hii watu walikuwa hawawakiani tamaa<span>
</span>ni vigumu kuwa na uhusiano mzito hivi na mtu ambaye hakusisimui kimwili
na kiroho! kuna haja ya kufanya utafiti juu ya jambo hili!</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41027" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41026" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ushoga ni aina Fulani ya
uhusiano wa mtu na mtu. Watu wa jinsia moja wanajenga uhusiano mkubwa kiasi
wanashindwa kujua ni wapi waweke mipaka katika uhusiano wao. Mfano kama mtu
anaweza kushirikiana mke wake na rafiki yake, bila kujificha kwa kukubaliana,
kama mtu akishindwa kumtenga rafiki yake akiugua kifafa na ukoma, kama mtu
anaweza kumwogesha rafiki yake hata kumsindikiza hadi chooni,<span> </span>kama mtu anaweza kuugusa mwili wote wa rafiki
yake ni kitu gani hawawezi kufanya pamoja? Ni wapi waweke mpaka? Wao peke yao
hawawezi hadi wapate msaada wa jamii inayowazunguka. Swali linakuwa je, hiyo
inakuwa ni tabia ya baadhi ya watu katika jamii, au ni tabia inayokubalika
katika jamii nzima. Je tabia hii inaweza kuvuruga amani ya jamii kama vile
kusengenya, uchoyo, wivu na wizi? Haya ndiyo mambo ya kujadiliana.</span><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"></span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41030" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41029" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Wakati sisi tunaishikia
bango kubwa hali ya mtu kuvutiwa na jinsia yake, wakati tunalaani matendo ya
kulawiti, kufira, usenge, ushoga na usagaji, Paulo, anazichanganya dhambi hizi
na dhambi nyinginezo kama vile uchoyo, ulevi, kusengenya na kulaghai. Na bahati
mbaya hakutofautisha ili kuonyesha ni dhambi ipi ni ndogo na ipi ni kubwa. Kama
ushoga na usagaji zingelikuwa ni dhambi kubwa kuliko nyingine, basi Paulo,
angezitaja peke yake ili kuuonyesha mkazo. Lakini yeye anaziweka kwenye ngazi
moja na dhambi nyingine. Tuna watu wangapi katika jamii zetu wanaosema uongo,
walevi, walaghai na wanaosengenya? Na je hawa tumewashikia bango mara ngapi
kama tunavyowashikia mashoga? Je, wachoyo ni wangapi? Dunia yetu imegawanyika
katika makundi ya maskini na matajiri kwa sababu uchoyo wa mali ni mkubwa sana.
Hili tumelishikia bango? Hili tunalilaani kama tunavyolaani ushoga na usagaji?
Katika hali ya kawaida uchoyo wa mali ni dhambi kubwa, maana uchoyo wa mali
unasababisha vita, mashindano na kuvuruga amani katika dunia yetu. Ushoga
umeleta vita? Umeleta matabaka katika jamii? Hili ni jambo la kujadiliana kwa
kina na wala si kulipinga kwa kufuata mkumbo.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41033" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41032" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kazi kubwa iliyo mbele
yetu ni kufafanua uhusiano wa mtu na mtu. Ni kuwafanya watu wa kawa wazi juu ya
uhusiano wao. Walio wengi na hasa katika jamii zetu za Kiafrika, wanakuwa
wagumu kuweka wazi swala hili la uhusiano. Watu wangependa kuhusiana kwa siri, lakini
mapenzi ni kikohozi hayawezi kujificha. Yawe ni mapenzi yanayoruhusiwa au ya
kinyume na maumbile, penye mapenzi hapakosi dalili!</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41037" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41036" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hadi sasa hivi watu
wanaogopa kuutaja udhaifu wao ili wasichekwe na kutengwa. Jinsi tunavyoficha
ukweli juu ya ugonjwa wa UKIMWI, ndivyo tunavyoshindwa kusema ukweli juu ya
mambo mengine yanayozunguka uhusiano wa mtu na mtu. Tunaogopa kuchekwa,
kunyoshewa kidole na unyanyapaa. Hivyo walio wengi wanaamua kuendelea kuishi na
udhaifu wao. Msimamo huu umeleta madhara mengi katika kanisa na katika jamii
nzima. Mfano watu wanaoshindwa kumudu sheria ya mke mmoja mme mmoja,
wanashindwa kujitokeza na matokeo yake ni ndoa za mitala ambazo mara nyingi
watoto wa nje hapawapati haki kama wanazozipata watoto walio kwenye ndoa
zinazotambuliwa na kanisa na jamii nzima. Hali hii imezalisha watoto wengi wa
mitaani. Pia uhusiano wa mtu na mtu limekuwa ni jambo la kufanywa kwa siri
kiasi watu wengi wameanguka kwenye hatari ya ugonjwa wa UKIMWI, bila kupata
ushauri maana wengi wao wanakutana kisiri. Ni vigumu kumpatia mtu ushauri wa
kujikinga kama hajakueleza kwamba anatembea na mtu ambaye una hakika ana virusi
vya UKIMWI.</span><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"></span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41040" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41039" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hivyo tusifikiri Papa, amekuja na msimamo mpya.
Tusifikiri Papa anaunga mkono ushoga na usagaji. Ni jambo la busara na hekima
na kama anavyosema Papa Francis: “... anayestahili kuhukumu ni Mungu pekee na
si mwingine”</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41043" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41045" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv0313865152MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_41047" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 6331 22</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-53532312356543965612013-12-10T00:04:00.001-08:002013-12-10T00:04:16.013-08:00NI YESU WA WAPI?<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36654" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36656" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">JE,NI YESU WA NAZARETI , WA ULAYA AU WA NAGERIA?<br />
<br />
</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36543" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36542" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Jana usiku (31.8.2013) nilikuwa uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere, nilikuwa napokea mgeni kutoka Ujerumani. Wakati tukisubiri ndege
kuwasili, niliona kundi la watu wamevaa T-shirt zenye maneno<span> </span>“Karibu Mchungaji <span> </span>Ma, uione Tanzania”. Walikuwa wakimsubiri
mgeni wao kwa hamu. Nilitaka kufahamu huyo mchungani anayesubiriwa hivyo ni
nani? Nikaambiwa ni mchungaji wa Kanisa... nimesahau jina la kanisa, ametumwa
kutoka Nigeria, kuja hapa Tanzania kuhubiri neno la Mungu na kuimarisha “Ukristu”.
Alikuwa anahamia hapa na familia yake. Sina uhakika ni makanisa mangapi hapa
Tanzania yanaendeshwa na wachungaji kutoka Nigeria; mengine makubwa, na wana
makanisa makubwa pia,<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36661"> </span>mengine madogo,
wanasalia kwenye kumbi za starehe, mfano hawa niliokutana nao uwanja wa ndege
wanasalia kwenye kumbi za Sunset Mbezi Makonde. Ni wazi hizi zote ni harakati
za kupambana na matatizo yanayotuzunguka.</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36664" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36663" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Nilichojiuliza usiku ule, baada ya kuona wamisionari hawa wa Nigeria, ni je
hawa wanakuja kuleta Neno la Mungu, au ni wawekezaji kama wengine wanaokuja
kuwekeza na kuchota kila kitu? Wanigeria wanaogopwa dunia nzima kwa tabia zao
za ujanja na udanganyifu. Labda hawa wachungaji <span> </span>“wameokoka”? Fedha zinazokusanywa kwenye
makanisa haya zinajenga Ufalme wa Mungu, au zinachangia kuongeza matatizo
yanayotuzunguka?</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36667" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36666" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mbele yetu kuna hitaji muhimu na la haraka. Ni hitaji la kutafuta mfumo wa
kupambana na matatizo yanayomzunguka mwanadamu wa leo. Mamilioni ya watu
wanaishi kwenye mateso kila siku ya Mungu. Kuna njaa, vita, umasikini, upweke,
magonjwa, uonevu, ubaguzi nk. Hapa Tanzania, watu wanakufa kwa UKIMWI, malaria
na magonjwa mengine yanayotibika. Ujambazi, ufisadi, rushwa na kutowajibika
vinasambaratisha uchumi wetu. Namba ya wajane na wagane inaongeza kwa kasi,
watoto yatima, watoto wa mitaani na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi
inaongezeka kwa kasi ya kutisha. Tufanye nini kuondokana na mateso na mambo
mengine yanayotishia uhai wa mwanadamu na hasa Mtanzania. Je, huyu Yesu wa
Nazareti, Ulaya na Nigeria, anaweza kuwa jibu? Anaweza kutusaidia kutengeneza
mfumo wa kupambana na matatizo yetu? Tunaweza kumgeukia? Tunaweza kumkimbilia?
Anaweza kutulinda? Anaweza kutusaidia? Anaweza kutuwezesha? Anaweza kututoa
usingizini? Anaweza kutupatia mwanga wa Hekima na Busara, ili tuyatawale
mazingira yetu na kuyalazimisha yatutumikie? Je wote wanaomfuata Yesu wa
Nazareti, wa Ulaya na Nigeria, wamekuwa wakivutiwa na mfumo wake wa kupambana
na matatizo ya dunia yetu? Au wanavutiwa na mambo mengine ambayo si muhimu sana
katika kusaidia maisha ya binadamu? Je, wanapambana na matatizo au wanayakimbia
na kujifanya hawayaoni?</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36671" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36670" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Wanaojiunga na<span> </span>makanisa haya ya Kinigeria,
wanavutiwa na neno la Mungu au miujiza ya uponyaji na utajiri usiokuwa na
maelezo? Taarifa za kuaminika ni kwamba kila anayejiunga na makanisa haya ni
lazima awe tajiri. Atamiliki magari, manyumba na utajiri mwingine mkubwa. Waumini
wanavutiwa na mali au Neno la Mungu?<br />
<br />
Mamilioni ya watu kwa miaka mingi wamekuwa wakilitaja jina la Yesu na
kumwabudu, lakini wachache kati ya mamilioni ndiyo waliomwelewa Kristu na namba
chache kabisa ndiyo waliofuasa kile alichokitaka kitendeke. Maneno ya Yesu
Kristu, yamebadilishwa na kupindishwa ili yatekeleze kile watu wanachokitaka,
na wakati mwingine maneno yake yamebadilishwa na kupindishwa yasimaanishe kitu
chochote! Jina la Yesu, limetumiwa kubariki maovu ya kila aina, kama wale
waliokuwa wakiongoza vita na kuuwa watu huku wakitanguliza msalaba na Biblia.
Latin Amerika, mamilioni ya watu walipoteza maisha yao na sehemu nyingine
kizazi kilifutika kabisa katika harakati za kueneza neno na mafundisho ya Yesu
Kristu. Lakini pia jina la Yesu, limetumiwa kuwashawishi na kuwaletea imani
kubwa wanaume na wanawake wengi hata kufikia hatua ya kupumbazika na kufanya
matendo ya kijinga, kama kujinyima chakula na kuitesa miili yao kufikia kiwango
cha uwendawazimu. Yesu amekuwa akitukuzwa na kuabudiwa kwa yale ambayo
hakuyalenga, yale aliyo yapinga na kuyakemea kuliko yale aliyoyalenga,
aliyoyahubiri, aliyoyatetea na kuyafia. Jambo la kushangaza ni kwamba mambo
ambayo Yesu, aliyapinga wakati wa uhai wake, yalifufuliwa, yalihubiriwa na
kusambazwa dunia nzima kwa jina lake.<br />
<br />
Hatuwezi kumuunganisha moja kwa moja Yesu wa Nazareti na hii dini kubwa ya
Kizungu, inayojulikana kama Ukristu. Yeye alikuwa mwanzilishi wa dini kubwa
zaidi ya hii tunayoifahamu. Yeye anasimama juu ya Ukristu na kutoa hukumu
juu yale yote dini hii imeyafanya kwa jina lake. Hata hivyo Ukristu, hauwezi
kudai mumiliki Yesu Kristu, maana mtu huyu alikuwa ni wa binadamu wote.<br />
<br />
Je, hii ina maana kwamba kila binadamu (Mkristu na asiyekuwa Mkristu) ana uhuru
wa kumtafsiri Kristu katika maisha yake jinsi anavyotaka? Inawezekana kabisa
kila mtu akamtumia Kristu anavyotaka kwa mabaya na mazuri? Lakini yeye alikuwa
ni mtu aliyekuwa na imani nzito ambayo alikuwa tayari kuifia. Je, hakuna namna
ya watu, wenye imani na wasiokuwa na imani kumpatia nafasi takika maisha yao
Yesu huyu wa Nazareti, akazungumza yeye mwenyewe kwenye mioyo yao? Je, hakuna
namna ya watu kulinganisha matatizo yao, nyakati zao na zile za Yesu wa
Nazareti?</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36675" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36674" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tishio lililopo leo si la mtu binafsi, kabila, taifa au bara. Tishio ni la
dunia nzima, ni tishio la ubinadamu. Tumefika mahali tunachanganyikiwa na
kufikiri kwamba hakuna mwenye uwezo wa kuzuia tishio la kuumaliza ulimwengu na
binadamu. Wapo vichaa kama Kibwetere na wajinga wengine wanaofikiri kwamba
mwisho wa dunia na ubinadamu vinashuka kwa miujiza, kwamba tunaweza kulala na
kuamka tunakuta dunia imekwisha. Huu ni ujinga mtupu! Mwisho wa dunia, unaletwa
na matendo ya binadamu ya muda mrefu. Matendo ya ubinafsi yasiyozingatia
umuhimu wa binadamu na viumbe vingine, yanaweza kupelekea mwisho wa dunia. Hili
si jambo la kutokea leo ama kesho, lakini mtu anayejali ni lazima kuhakikisha
anarithisha dunia hii kwa vizazi vijavyo. Tunakata tamaa kwamba hakuna tena
mfumo mzuri wa maisha unaowafaa binadamu wote. Mfumo wa kuweza kuangalia na
kutengeneza maisha bora ya mwanadamu wa leo na kesho.<br />
<br />
Siku za nyuma kidogo tulifikiri labda silaha za nyukilia zingeweza kutumika
kuteketeza ulimwengu. Tumeanza kupunguza woga huu, lakini mambo mengine mengi
kama vile uharibifu mazingira, uchimbaji ovyo wa madini, upungufu wa chakula na
ardhi nzuri ya kustawishia chakula, hatari ya kupungua kwa maji na ongezeko la
binadamu, ni vitisho vipya kwa uhai wetu na ulimwengu tunamoishi. Ukweli kwamba
binadamu wanaongezeka kwa kiasi cha milioni 80 kwa mwaka, ni tishio
kwamba kwa miaka michache ijayo, matumizi ya maji na chakula yatakuwa katika
hali mbaya duniani kote. Ukweli kwamba magazeti, vitabu na utengenezaji wa
karatasi za kuandikia unaitafuna misitu ni tishio la uharibifu wa mazingira
katika enzi hizi tulizomo.</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36678" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36677" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kuna uharibifu mkubwa katika kila biashara zinazofanywa kwa lengo la kupata
faida. Kila mtu analenga kupata faida bila kuangalia matokeo ya vitendo vyake.
Viwanda vingi vimekuwa vikiharibu mazingira kwa moshi unaotoka viwandani,
lakini pia uchafu unaotiririshwa kutoka viwandani kwenda mitoni na kwenye
maziwa na bahari umechangia uharibifu mkubwa wa viumbe katika maji. Ni wazi ili
tupone, panahitajika mabadiliko makubwa. Swali ni je ni nani atakubali
hasara ya kusimamisha viwanda vyake?</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36681" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36680" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Inakuwa ngumu kuwashawishi watu kubadili mtido wa maisha, ili kurefusha
maisha yao wenyewe, inakuwa ngumu zaidi kuwashawishi kufanya hivyo ili
kuyarefusha maisha ya watu wengine. Inakuwa ngumu zaidi na zaidi kuwaambia
kufanya hivyo kwa lengo la kunusuru maisha ya mabilioni ambao bado
hawajazaliwa; kuicha dunia yetu ikiwa salama kwa vizazi na vizazi. Sisi
tuliikuta salama, ni jukumu letu kuiacha ikiwa salama.</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36684" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36683" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kuna ukweli kwamba dunia hii ina baadhi ya watu, wake kwa waume wenye
nia njema, na wanayaona matatizo yote hayo na wangependa kufanya chochote
kuleta mabadiliko. Daima wanaonyesha nia yao njema na wengine wako tayari hata
kuyapoteza maisha yao ili kufanikisha kuleta mabadiliko. Lakini wanaweza
kufanya nini? Mtu mmoja, au kikundi cha watu wachache kinaweza kufanya nini
kwenye matatizo haya ya Ulimwengu wa kisasa? Kilicho mbele yetu ni kitu
kikubwa, ni mifumo ya dunia hii iliyojikita na kustawi! Ni mifumo ya ubepari,
soko huria na utandawazi. Mara ngapi tunasikia kilio cha watu kwamba mtu hawezi
kupambana na mifumo?</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36687" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36686" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Nani wa kutuokoa? Yesu wa Nazareti, Yesu wa Ulaya au Yesu wa Nigeria?
Tutaokolewa na Uislamu au Ukristu? Tutaokolewa na dini nyingine au dini za
jadi? Au tukimbilie ukombozi wa fikra na kutawaliwa fikra pevu?<br />
Na,<br />
Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv0203023299MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_36694" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122.</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-49843728186599360842013-12-10T00:01:00.004-08:002013-12-10T00:01:52.640-08:00MTWARA KUCHELE 1<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34850" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34923" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">MTWARA “KUCHELE”, VURUGU ZA MTWARA JIBU ANALO RAIS KIKWETE.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34926" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34925" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34926" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34925" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34926" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34925" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Moja ya ziara zake katika mkoa wa Mtwara, Rais Jakaya Mrisho Kiwete,
aliwaambia watu wa Mtwara: “Mtwara Kuchele”, maana yake “ Mtwara kumekucha”.
Ziara hii ilifanyika kabla ya vurugu za Mtwara. Mheshimiwa Rais aliwaambia watu
wa Mtwara, kwamba gesi iliyovumbuliwa kwenye mkoa wao itaharakisha maendeleo na
yeye atahakikisha viwanda vingi vinajengwa, vijana wanapata kazi , uchumi wa
mkoa huo unapanda na mji wa Mtwara <span> </span>unabadilika na kufanana Dubai. Na kwa matani,
akawaambia , “ Ningekuwa na uwezo, ningehamisha gesi yote hii na kuipeleka
Bagamoyo”. Maneno haya yako midomoni na moyoni mwa kila mtu wa Mtwara,
aliyesikiliza hotuba hiyo ya Mheshimiwa Rais.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34932" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34931" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tarehe 11.9.2013 mpaka tarehe 15.9.2013, nilifunga safari kwenda Mtwara,
kuchunguza chanzo cha vurugu ya “Haitoki”. Hatukuzoea kusikia vurugu hizi mkoa
wa Mtwara. Mwaka 2005, nilikuwa mwangalizi wa uchaguzi mkuu kupitia TEMCO;
nilishuhudia upole wa watu Mtwara. Kampeni za wagombea mwaka huo wa uchaguzi
zilitawaliwa na wali na vinywaji. Wakipikiwa wali na kunywa pombe za kienyeji,
wanaimba na kucheza na kusahau matatizo mengine ya mkoa wao. Hivyo vurugu za
gesi zilipotokea, watu wakafa na mali zikaharibiwa, kila mtu aliyeufahamu mkoa
huu wa Mtwara, alishangaa na kujiuliza kulikoni.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34935" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34934" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mtu wa kwanza niliyeongea naye, ni kijana wa Bajaji, ambaye kwa maoni yake
kasheshe zote za vurugu za gesi zilianzishwa<span>
</span>na Hotuba ya Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, ya kuibadilisha Mtwara
kufanana na Dubai, ahadi ya kujenga viwanda na kuhakikisha vijana wanapata
ajira.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34938" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34937" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“Huwezi kuamini, hotuba hiyo ya Mheshimiwa Rais, ilianza kuleta matunda,
maana tulianza kuona watu wengi wanakuja kununua viwanja hapa Mtwara. Kuna mzee
ninayemfahamu, aliuuza kiwanja chake ufukweni, kwa bei ya milioni mia mbili
hamsini” alinieleza <span> </span>huyu kijana wa
Bajaji.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34941" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34940" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“La kushangaza, hata kabla ya kuliona jiwe la msingi la kuijenga Dubai ya
Mtwara, tulisikia kwamba gesi inasafirishwa kwenda Bagamoyo”.<span> </span>Hayo ni maneno ya kijana aliyenibeba kwenye
Bajaji, kutoka maeneo ya Bima- Mtwara kuelekea Makao makuu ya kanisa la KKKT
mjini Mtwara. Hakukubali kunitajia jina lake. “Tunaogopa sana siku hizi, jina
langu likitokea gazetini, nitakamatwa na kupelekwa Gwantanamo, huko nitapigwa
na kuteswa, kama ambavyo watu wengine wamepigwa na kuteswa, wengine hadi leo
hii hawajarudi” alinieleza huyo kijana wa Bajaji. Gwantanamo ni kituo cha Jeshi
cha Nalyendele. Kilikuwa ni kituo cha ukombozi wa nchi ya Msumbiji, lakini leo
hii kimegeuka kuwa ni kituo cha mateso makubwa ya kunyamazisha sauti za “Gesi
haitoki”</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34944" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34943" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“Utani ukawa ukweli, gesi inakwenda Bagamoyo. Rais wetu alitwambia angekuwa
na uwezo, angesomba gesi yote na kuipeleka Bagamoyo. Wakati huo tulijua ni
utani. Tunamjua Rais ana utani mwingi. Lakini baada ya kuambiwa kwamba mabomba
yatasafirisha gesi yetu ya Mtwara kwenda Bagamoyo, tukajua sasa si utani bali
ni kweli. Na tulijua, maana Rais wa nchi ana uwezo wote...” Aliendelea
kunieleza kijana wa Bajaji.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34947" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34946" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa maelezo ya kijana huyu ni kwamba wazee walipoona Dubai ya Mtwara
inayeyuka, walitaka kuwa na maongezi na Mkuu wa Mkoa, ili kujua kulikoni.
Lakini kwa kiburi, Mkuu wa Mkoa, alikataa kukutana nao. “ Hivyo wazee walipanga
kuitisha maandamano, lakini Mkuu wa Mkoa aliyapiga marufuku maandamano hayo”
Aliendelea kunieleza huyu kijana wa Bajaji.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34950" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34949" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa maoni ya kijana huyu wa Bajaji, kama Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
angelikubali kuwasikiliza wazee au kuwakubalia maandamano yao, vurugu, vifo na
uharibifu wa mali uliojitokeza Mtwara usingekuwepo. Alihitimisha maongezi yetu
kwa kusema “ Vurugu za Mtwara chanzo chake ni ahadi za Mheshimiwa Rais Kikwete
na kiburi cha Mkuu wetu wa mkoa...”</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34952" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34954" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ingawa sababu za vurugu zinatajwa mbili ambazo ndizo kubwa, bado kuna mambo
mengine mengi, kama mpasuko ndani ya chama cha CCM mkoani Mtwara, <span> </span><span> </span>elimu
ndogo watu waliyonayo juu ya masuala ya gesi na suala zima la ushirikishwaji.
Kila mtu unayezungumza naye kwenye mji wa Mtwara, atakwambia kwamba suala zima
la gesi limezungukwa na usiri mkubwa na wananchi hawakushirikishwa. Hata na
viongozi wa serikali za mitaa, madiwani na wenyeviti wa mitaa, wanalalamika
kutoshirikishwa.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34957" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34956" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Inashangaza kusikia watu wakisema kwamba gesi inakwenda Bagamoyo, hakuna
anayesema inakwenda Dar-es-Salaam. Pia uelewa <span> </span>wa gesi, kuhusu uchimbaji wake hadi hatua ya
kuisafirisha ni mdogo, maana nilielezwa juu ya mzee mmoja ambaye ni mvuvi wa
miaka mingi, siku moja aliona meli kubwa baharini, akarudi na kutangaza kwamba
meli zimeanza <span> </span>kuinyonya gesi na
kuisafirisha bila hata serikali kujua. Kumbe hizo ni meli zinazofanya maandalizi
ya kuanza kuchimba gesi baharini.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34960" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34959" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na uelewa mdogo wa masuala ya gesi, wana hoja nzito: Kama mchakato
wa gesi unachua miaka mingi kumi na <span> </span>tano
hadi ishirini kama wataalam wanavyoeleza, kwa nini wanaona magari yamebeba
mabomba na vituo vya mabomba haya vimewekwa sehemu mbali mbali kutoka Mtwara
hadi Dar-es-Salaam? Maandalizi yanaoyesha gesi inaondoka kesho ama keshokutwa!</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34963" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34962" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Siku tano nilizokaa Mtwara, nikijaribu kutafiti na kuchunguza chanzo cha
vurugu za “Gesi haitoki”, uharibifu wa mali na vifo vilivyotokea, nilipata
majibu yanayofanana kwa karibu sana na maoni ya kijana wa Bajaji. Niliongea na
viongozi wa serikali, vijana wa vijiweni, wazee, wanawake, viongozi wa dini, wafanyabiashara,
vyama vya siasa, na wote majibu yalifanana! Ukimtoa diwani mmoja wa CCM,
aliyekubali jina lake kutajwa wengine wote hawakutaka kwa kuogopa kupelekwa
Gwantanamo. Hivyo si busara hata kulitaja jina la Diwani huyo wa CCM.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34966" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34965" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mbali na sababu mbili kubwa za kuanzisha vurugu za gesi nilizozitaja hapo
juu, watu wa Mtwara, wazee<span> </span>kwa vijana
wanaimba historia ya machungu ya <span> </span>mkoa <span> </span>wao. Kwamba: Kulikuwa na reli inatoka
Nachingwea hadi Mtwara, lakini iling’olewa; Kwamba kulikuwa na mtambo wa
kusukuma maji, lakini uliondolewa na kupelekwa sehemu nyingine; Kwamba kulikuwa
na mpango wa Mtwara corridor <span> </span>lakini
ulipotelea kusikojulikana; Kwamba Bandari ya Mtwara ndiyo yenye kina kirefu na
uwezo wa kupokea meli nyingi kwa wakati mmoja, lakini ilitelekezwa na vifaa
vingine kuondolewa na kupelekwa Dar-es-Salaam, Kwamba uwanja wao ndege ni
miongoni mwa viwanja vikubwa vya mwanzo kabisa baada ya uhuru, lakini kiwanja
chao cha ndege kilitelekezwa, wakasikia vikiendelezwa viwanja vingine kama vile
cha Kilimanjaro na cha Dar-es-Salaam; Kwamba kulikuwa na kiwanda cha kubangua
korosho, lakini hakipo tena; kwamba kwa vile Mtwara ulikuwa ni uwanja wa
mapambano ya kuikomboa Msumbiji, hakuna aliyependa kuwekeza au kufanya kazi
Mtwara; Kwamba kulikuwa na kilimo cha pamba lakini kimekufa jumla; kwamba
barabara ilikuwa mbaya hadi siku za hivi karibuni walipojengewa daraja la Mkapa
na Barabara ya lami ambayo hata hivyo bado zaidi ya kilomita thelathini <span> </span>hazijakamilika; Kwamba bei ya korosho
imeendelea kuwa chini na umasikini umeongezeka na kubwa zaidi kwamba ahadi za
Songosongo kuleta maendeleo mkoa wa Lindi mbona hazijatekelezwa?</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34969" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34968" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“Uamuzi wa kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Bagamoyo, umeamsha
mshikamano miongoni mwa wananchi, kusema kweli imetonesha vidonda vya historia
ya machungu ya Mkoa wetu. Na kusema ukweli hakuna aliye nyuma ya vurugu hizi;
ni mshikamano wa wananchi wa Mtwara” alinieleza diwani wa CCM, ambaye jina lake
nalitunza kwa sasa.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kufuatana na maelezo ya diwani huyu ni kwamba vuguvugu za “Gesi haitoki” zilikuwa
na hatua kuu nne:</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Baada ya kusikia matangazo ya kuisafirisha gesi kutoka Mtwara kwenda
Bagamoyo, na baada jitihada za kukutana na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa
kushindikana, wanamtwara waliibuka na kauli mbiu ya: “ Gesi kwanza, vyama
baadaye”. “Vyama vyote vya siasa viliungana na kuwa na sauti moja juu ya gesi”
alinieleza diwani huyu wa CCM.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hatua ya pili, ilikuja na kauli mbiu ya “ Gesi kwanza, uhai baadaye”. Hapa
ndipo mapambano yalianza baina ya polisi na wananchi. Kijana wangu wa Bajaji
aliniambia kwamba mapambano hayo yalikuwa makubwa na yakutisha! “Kama wananchi
tungelikuwa na silaha, mapambano haya yangekuwa mabaya sana” Alinieleza kijana
huyu.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hatua ya tatu ya vuguvugu na vurugu za Gesi katika Mkoa wa Mtwara, ilikuja
na kuli mbiu ya “Gesi haitoki” .Hapa ndipo serikali ilipoamua kutumia nguvu
kubwa, mali ziliharibiwa na watu walikufa. Hadi sasa serikali inasema walikufa
watu watatu. Lakini kuna habari za pembeni zinazosema watu waliokufa kwenye
machafuko haya ni zaidi ya 18,<span> </span>na
wengine wanasema ni kama 100! Hata hivyo hadi leo hii bado watu wanakamatwa,
wanapelekwa Gwantanamo, wanateswa na wengine hadi leo hii hawajarudi kwenye
majumba yao.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hatua ya nne ya vuguvugu na vurugu za Gesi ni “Gesi itoke tu lakini...”.
Sasa hivi kila mtu unayekutana naye Mtwara, anasema “Gesi itoke”. “Wameamua
kutuletea jeshi letu la Wananchi, kutupiga na kutufanya vibaya, Gesi itoke,
lakini tutasusia shughuli zote za serikali na tunawasubiri kwenye uchaguzi wa
2015” Alinieleza mfanyabiashara ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tarehe 14.9.2013, tulishuhudia Mwenge wa Uhuru ukiingia Mtwara kimya kimya
kwa ulinzi wa kutisha. Siku tatu kabla ya ujio wa Mwenge, vipepererushi na
ujumbe mfupi kwenye simu za viganjani ulianza kupita kuwahamasisha watu kususia
sherehe za Mwenge. Ni kwamba Mtwara, wanaheshimu sana ujumbe mfupi wa simu,
hata bila kujua unatoka wapi; ujumbe ukisema maduka yasifunguliwe, agizo
linatekelezwa; ujumbe ukisema hakuna kutoka nje, mitaa inashinda bila watu.
Hivyo na ujumbe wa kususia sherehe za Mwenge, ulitekelezwa kiasi kikubwa;
Wanafunzi na wafanyakazi wa serikali ndio waliojitokeza kuupokea Mwenge wa
Uhuru.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa kuangalia kwa nje, ni kwamba sasa hivi Mtwara kuna utulivu, lakini
hakuna amani. Kuna utulivu kwa vile jeshi linatumia nguvu na watu hawana tena
jukwaa la kutoa maoni yao, wanaishi kwa woga. Jeshi linaweza kutesa miili yao
na kuweka utulivu wa nje tu, lakini ndani ya mioyo yao wana makovu makubwa na
hasira. Mtu mwenye hekima, angeshughulikia kuponya makovu na wala si kuendelea
kutumia nguvu kubwa kuwalazimisha watu kukubali yale wasiyoyaelewa vizuri na
wala kufahamu jinsi watakavyofaidika nayo.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34972" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34971" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Baadhi ya watu wameamua kuishi porini kwa kuogopa nguvu za Jeshi. “Kuna mtu
aliyekaa porini siku saba kwa kuwaogopa wanajeshi. Mtu huyu alikuwa ni dreva
kwenye kampuni Fulani ya mhindi, baada ya siku saba aliporudi kazini,
alifukuzwa kwa utoro. Kitendo cha kumfukuza kilimshutua sana, na baada ya siku
chache alikufa kwa shinikizo la moyo. Mifano kama hii tunayo mingi, lakini
tumeamua kukaa kimya” Alinieleza mwenye kiti wa mtaa ambaye hakutaka jina lake
litajwe.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34975" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34974" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ubakaji, kuwangilia watu kinyume na maumbile, udhalilishaji na mateso
mengine ni baadhi ya vitu vinavyotajwa kutokea na kuendelea kutokea Mtwara. “Vurugu
zote hizi Mbunge wetu wa Mtwara mjini alisimama upande wa wananchi na kutetea
haki za Mkoa wetu bila woga. Hata Mkuu wa wilaya ya Mtwara, alikuwa upande
wetu. Hawa wawili wanakubalika na wakisema jambo tunasikia, ingawa tumemgomea
Mkuu wetu wa Wilaya kushiriki sherehe za Mwenge”. Alinielezea mama mmoja ambaye
alionekana kama mwanasiasa, lakini hakutaka kusema ni wa chama gani</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34978" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34977" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“Si kweli kwamba hatutaki Gesi itoke na kuwanufaisha watanzania wengine.
Hoja yetu ni je Gesi ikitoka, sisi tunabaki na hali gani? Umasikini? Dubai yetu
iko wapi? Kama ni kuisafirisha Gesi kwenda kuiuza nchi za nje kwa nini isisafirishwe
kwa kupitia bandari ya Mtwara? Kama ni kuzalisha umeme, kwa nini mitambo ya
kuzalisha umeme isijengwe Mtwara, na umeme ukasafirishwa kwa<span> </span>nguzo?”<span>
</span>Alilalamika kiongozi mmoja wa dini niliyeongea naye.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34981" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34980" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Katika harakati za kurudisha imani ya wananchi, serikali imewapeleka baadhi
ya watu wa Mtwara , nchini Thailand kujifunza mafanikio ya miradi ya Gesi.
Lakini kuna manung’uniko kwamba safari hiyo haikuwa ya lazima, ni matumizi
mabaya ya fedha, wakati kuna kipindi cha Baragumu la Msimbati, kinachorushwa
kwenye luninga na kuelezea mafanikio ya Gesi ya Songosongo. Kwa nini watu hawa
wasingepelekwa Songosongo kujifunza mafanikio ya huko kuliko kutumia fedha
nyingi kuwasafirisha watu kwenda nchini Thailand? Hata hivyo na uchaguzi wa
nani aende Thailand, haukuwa wa wazi. Tulipoongea na mmoja kati ya wale<span> </span>waliokwenda Thailand, alisema<span> </span>“ Mimi nafikiri nilichanguliwa kwa vile niko
karibu na Waziri Fulani”</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34997" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34996" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mtu wa kumaliza vurugu za Mtwara, ni Rais mwenyewe. Kila mtu tuliyeongea
naye, alitoa jibu hili. “Tunamtaka Rais wetu aje hapa abadilishe usemi wake,
aje atwambie kwamba sasa Dubai ni ndoto, mbali na hapo hatumtaki mtu yeyote
hapa...” Alinieleza mzee ambaye ilionyesha ana ushawishi mkubwa kwenye jamii
inayomzunguka..</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34993" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34992" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa kifupi ni kwamba watu wa Mtwara wamepoteza imani na Mkuu wao wa Mkoa,
hawataki kumsikia waziri wa Elimu, ambaye wanasema alikwenda Mtwara kuwatukana:
“Mtwara mnafanya kazi ya kutiana<span> </span>mimba
mambo ya Gesi mtayafahamu?” Hawataki kumsikia Shehe Mkuu wa Mkoa. Pia hawataki
kumsikia waziri wa<span> </span>nishati na madini,
ambaye naye wanasema aliwatukana. Wanamtaka Rais wao ambaye wakati wa kuomba
kura, alienda kuongea nao, na sasa wanataka aende aongee nao.</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34990" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34988" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo</span></div>
<div class="yiv5557671131MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_34986" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-25763272258470674212013-12-09T23:58:00.001-08:002013-12-09T23:58:26.299-08:00MTWARA KUCHLE 2<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:WordDocument>
<w:View>Normal</w:View>
<w:Zoom>0</w:Zoom>
<w:TrackMoves/>
<w:TrackFormatting/>
<w:PunctuationKerning/>
<w:ValidateAgainstSchemas/>
<w:SaveIfXMLInvalid>false</w:SaveIfXMLInvalid>
<w:IgnoreMixedContent>false</w:IgnoreMixedContent>
<w:AlwaysShowPlaceholderText>false</w:AlwaysShowPlaceholderText>
<w:DoNotPromoteQF/>
<w:LidThemeOther>EN-US</w:LidThemeOther>
<w:LidThemeAsian>X-NONE</w:LidThemeAsian>
<w:LidThemeComplexScript>X-NONE</w:LidThemeComplexScript>
<w:Compatibility>
<w:BreakWrappedTables/>
<w:SnapToGridInCell/>
<w:WrapTextWithPunct/>
<w:UseAsianBreakRules/>
<w:DontGrowAutofit/>
<w:SplitPgBreakAndParaMark/>
<w:DontVertAlignCellWithSp/>
<w:DontBreakConstrainedForcedTables/>
<w:DontVertAlignInTxbx/>
<w:Word11KerningPairs/>
<w:CachedColBalance/>
</w:Compatibility>
<m:mathPr>
<m:mathFont m:val="Cambria Math"/>
<m:brkBin m:val="before"/>
<m:brkBinSub m:val="--"/>
<m:smallFrac m:val="off"/>
<m:dispDef/>
<m:lMargin m:val="0"/>
<m:rMargin m:val="0"/>
<m:defJc m:val="centerGroup"/>
<m:wrapIndent m:val="1440"/>
<m:intLim m:val="subSup"/>
<m:naryLim m:val="undOvr"/>
</m:mathPr></w:WordDocument>
</xml><![endif]--><br />
<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:LatentStyles DefLockedState="false" DefUnhideWhenUsed="true"
DefSemiHidden="true" DefQFormat="false" DefPriority="99"
LatentStyleCount="267">
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Normal"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="heading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="35" QFormat="true" Name="caption"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="10" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" Name="Default Paragraph Font"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="11" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtitle"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="22" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Strong"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="20" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="59" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Table Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Placeholder Text"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="No Spacing"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Revision"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="34" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="List Paragraph"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="29" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="30" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="19" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="21" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="31" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="32" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="33" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Book Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="37" Name="Bibliography"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" QFormat="true" Name="TOC Heading"/>
</w:LatentStyles>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 10]>
<style>
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:"Table Normal";
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:"";
mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;
mso-para-margin-top:0in;
mso-para-margin-right:0in;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0in;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:"Calibri","sans-serif";
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-font-family:"Times New Roman";
mso-fareast-theme-font:minor-fareast;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-bidi-font-family:"Times New Roman";
mso-bidi-theme-font:minor-bidi;}
</style>
<![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapedefaults v:ext="edit" spidmax="1026"/>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapelayout v:ext="edit">
<o:idmap v:ext="edit" data="1"/>
</o:shapelayout></xml><![endif]-->
<br />
<div class="MsoNormal">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;">MTWARA KUCHELE 2</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;">Makala iliyopita ya Mtwara Kuchele, ni matokeo ya utafiti uliofanywa na
mwandishi wa safu hii akishirikiana na Mtandao wa Madeni na Maendeleo (TCDD)
kama sehemu ya mafunzo ya ushawishi na utetezi yaliyofanyika tarehe 10-13
Septemba 2013 kwa wanachama wake 30 waliotoka kwenye mikoa ya Mbeya, Iringa,
Ruvuma, Mtwara, Lindi, Mara, Kigoma, Mwanza, Pwani, Dar es Salaam na Tabora
ilifanya utafiti kwenye manispaa ya Mtwara Mikindani juu ya ukweli kuhusu
sakata la mradi wa Gesi Mtwara lilitokea kuanzia tarehe 17 Mei 2013. Mafunzo
haya yalifanyika kwenye ukumbi wa Lutheran Centre Mtwara na mwandishi wa makala
hii alishiriki kuendesha mafunzo hayo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;">TCDD ilifanya mahojiano na watu<b style="mso-bidi-font-weight: normal;"> 257</b>
kwenye kata 7 kati ya 15 za Manispaa ya Mtwara Mikindani, ambao kati yao
walikuwa Viongozi wa ngazi ya mkoa 4Viongozi wa ngazi ya wilaya <b style="mso-bidi-font-weight: normal;">6</b> Madiwani 10Viongozi wa serikali za
mitaa <b style="mso-bidi-font-weight: normal;">46</b>Wananchi wa kawaida <b style="mso-bidi-font-weight: normal;">193.</b></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;">Wote waliohojiwa,<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>waliomba majina
yao yasitajwe, kwa kuogopa kichapo na mateso ya Gwantanamo. Mzee mmoja
alituelezea kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW;">“</span><span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Tambiko maalumu
walilolifanya baadhi ya wazee wa mila, wananchi wa Mtwara kwa kushirikisha
viongozi wa dini na makundi ya jamii mara baada ya madhila ya May 23 mwaka huu
ni kiashiria cha kutokukubaliana na mazingira ya utekelezaji wa mradi wa Gesi
licha ya manufaa kwa taifa yanayoelezwa na viongozi”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Mzee huyu aliyekuwa anazungumza kwa
kujiamini, aliendelea kutuelimisha juu ya vurugu zilizojitokeza Mtwara, kwa kauli
mbiu ya “ Haitoki”, kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Kwa namna yoyote ile ridhaa ya
wananchi katika utekelezaji wa miradi inayolenga kutumia raslimali iliyolindwa
kwa miongo kadhaa na vizazi vya jamii ya eneo ambapo mradi unakusudiwa
kutekelezwa ni muhimu na vyema kuheshimiwa ili kuhakikisha kwamba laana za vizazi
hivyo hazijengwi katika kizazi kinachofuata ndivyo imani za asili
zinavyotambuliwa</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Hii inadhihirishwa na hatua
zinazochukuliwa na jamii hizo hasa katika kutekeleza matambiko ambapo heshima
maalumu kwa wafu waliotangulia mbele za haki na kuzikwa kwenye maeneo ambako
miradi inafanyika hupewa nafasi ya kuhamisha makaburi kama sehemu muhimu ya
kutekeleza imani na matambiko.”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Ikumbukwe awali lilishatolewa tamko
kutoka Msimbati kwa bibi Samoe Mtiti (106) kuwa ikiwa serikali itaendelea
kulazimisha mchakato wa gesi bila kusikiliza hoja za wananchi angegeuza gesi
kuwa maji, hatua ambayo ililazimu mbinu mbalimbali za kumshawishi bi Samoe
zifanyike ili hali hiyo isijitokeze. Wakazi wa Mtwara, wanaamini nguvu za<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Bibi Mtiti, kwamba ana uwezo wa kubadili gesi
kuwa maji, na akitaka gesi isitoke, haiwezi kutoka!</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Imani hii kwa Bibi Samoe Mtiti,
inaonyesha wazi jinsi suala zima la Gesi, halijaelezwa vizuri. Watu hawana
elimu juu ya Gesi na matumizi yake. Kama bado wanaamini Gesi inaweza kubadilika
kwa nguvu za miujiza ikawa maji, bado kuna kazi kubwa. Serikali ina wajibu
mkubwa wa kuwaelimisha watu wa Mtwara. Kutumia jeshi kuwapiga na kuwanyamazisha
si njia sahihi ya kuleta mabadiliko na maendeleo. Kinachohitajika ni
kuwasiliza, kujadiliana nao, kuwashirikisha na kuwaelimisha.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Kuna habari za kuaminika kwamba Januari
24, 2013 gari lenye namba za usajili T609 BXG la mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni
ofisa wa idara nyeti liliteketezwa kwa moto na wananchi wa Msimbati kwa kile
kinachoelezwa kuwa lilifika kumteka bi Somoe ambaye kijijini hapo anajulikana
kama mkuu wa kaya. Wako tayari kumlinda bibi huyu kwa gharama yoyote ile, kwa
vile wanaamini ana nguvu za kutenda miujiza.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Mzee, tuliyeongea naye, alikuwa
anajaribu kutufafanulia umuhimu wa ushirikishwaji. Kwamba serikali
haikuzingatia hili, na watu wa Mtwara hawakushirikishwa juu ya uchimbaji wa
gesi, kwani raslimali gesi sasa inazungumzwa kama bidhaa haramu kama ilivyo
bangi kwenye vyombo vya dola! Ukitamka suala la gesi kwa wanamtwara wanakuona
kama vile umetumwa kuwadodosa ili uwachomee utambi kwenye jeshi na hatimaye
wapelekwe Gwantanamo kuteswa; hiki ni kituo cha Jeshi cha Nalyendele, ambacho
kimebatizwa jina la Gwantanamo, kutokana na vitendo vya mateso vinavyoendelea
kwenye kituo hicho.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Wananchi wanaolizungumzia suala la
gesi<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>kwa tahadhari wanatamka bayana kuwa
vyombo vya usalama vinavyoshughulikia ukusanyaji wa taarifa
havikujipa kazi ngumu kujua hasa kwa nini wananchi wanashinikiza gesi
haitoki bila kujali imani, vyama na hali zao. Kiongozi wa serikali za mtaa
tuliyeongea naye wakti wa utafiti huu alituelezea kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Hili lilichukuliwa kama ajenda ya
kisiasa na watoa taarifa ngazi za juu na ndiyo sababu katika mazungumzo ya
viongozi wa ngazi ya kitaifa wanaliona kama lilikuwa la kisiasa kumbe hii ni
ajenda ya wana-Mtwara imezingatia zaidi maslahi na ustawi wa wana Mtwara na ni matokeo
ya maumivu ya muda mrefu kucheleweshwa kwenye safari ya kufikia maendeleo ya
kweli”. Na kuongezea kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Hivyo maamuzi ya matumizi ya nguvu
ndiyo yakachochea zaidi ufa wa mahusiano baina ya serikali na wananchi
hadi sasa ambapo kama mtu anafanya utafiti atabaini kuwa kati ya watu kumi
unaokutana nao ni nadra kukutana na mtu anayesifia matunda tarajiwa ya miradi
ya gesi kwa Mkoa wa Mtwara huku wengi zaidi wakilaumu mazingira ya utekelezaji
mradi huo”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Serikali
bado inatumia nguvu kubwa kuhakikisha inazima sauti za watu wa Mtwara. Hii
inadhihirishwa na tukio la Septemba 12,2013 katika Kijiji cha Shole –Mtwara.
Wanajeshi walitembeza kipigo kwenye kijiji hicho na baadhi ya watu waliumizwa
vibaya kwa<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>taarifa kwamba kulikuwa na
vipeperushi vya kuwazuia watu kushiriki mapokezi ya Mwenge wa uhuru. </span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Mapokezi mabaya ya mwenge katika wilaya
ya Mtwara yanadhihirisha kuwepo kinyongo miongoni mwa wananchi ambapo ililazimu
kutumika mbinu za kuwaruhusu wanafunzi kuvaa nguo za nyumbani ili isionekane
kwamba Mwenge unapokelewa na wanafunzi<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>peke yao, hata hivyo mbinu hii <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>haikusaidia kuficha hasira za wananchi.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Baada ya kichapo cha Kijiji cha Shole,
diwani mmoja wa CCM alitwambia kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Matumizi ya nguvu kubwa za dola katika
masuala yanayohitaji utashi wa watu ni kiashiria kuwa kuna pengo la mahusiano
baina ya serikali na wananchi na hivyo kuhitaji chombo kingine kuunganisha
makundi yanayotofautiana ”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Kulingana na maelezo ya wananchi, kwa sasa
chombo kinachopewa nafasi katika kuunganisha mahusiano baina ya wananchi na
mamlaka ya serikali ni mijadala ya pamoja ikihusisha asasi za kiraia ili
kurejesha mawasiliano na kuaminiana ambako kumetoweka.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Wananchi wa Mtwara wanasema ukimya
uliopo sasa si kwamba ni utulivu na amani bali ni utulivu pasipo amani, na
wananchi wanafanya hivi kupisha udhalilishaji na manyanyaso ya matumizi makubwa
ya nguvu za dola. </span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Kimsingi tangu kutolewa agizo la
kutoitishwa mikutano ya wazi inayojumuisha watu kwenye maeneo ya wazi, Mtwara
imekuwa kisiwa kwa muda sasa kutokana na wananchi kutopata fursa ya kukutanika
kujadili maendeleo ya mkoa wao.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“Hivi sasa <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>msimu wa korosho umeanza lakini hatuwezi
kukubaliwa kuitisha mikutano ya kujadiliana juu ya maslahi ya wakulima wa korosho
kutokana na agizo hilo na kwamba ukifanya mkusanyiko wowote utakuwa umevunja
amri halali ya serikali” . Alituelezea kiongozi mmoja wa serikali za
mitaa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Utekelezaji wa kamata kamata ya
watuhumiwa wa vurugu za Mei 23 ulioendeshwa kwa usiri mkubwa na nyakati za
usiku kwa kutumia wanajeshi, umetajwa pia kufanywa kwa uonevu mkubwa <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>kwa sababu hata wale <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>ambao hawakuwepo mazingira ya tukio kubebwa
kwa chuki na tofauti zilizokuwepo baina ya baadhi ya viongozi wa mitaa na
wananchi wao.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">“ Nilibambikizwa shtaka polisi la
kuchoma nyumba ya waziri wakati hata nyumba yenyewe siifahamu ipo wapi na zaidi
ya yote sehemu ya tukio <span style="mso-spacerun: yes;"> </span><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>ni mwendo wa siku nzima sasa nilishirikije na
wakati mimi <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>nilishinda kwenye kibanda
changu sokoni hapa ambapo nilishuhudiwa kikiharibiwa na polisi”. Alituelezea
mama mmoja ambaye ana kesi ya kuichoma moto nyumba ya waziri Fulani wa Mtwara.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Pia tume ya haki za binadamu ambayo
ilifanya ziara wilayani humo kufuatilia ukiukwaji wa haki za binadamu
inalaumiwa kwa kuchukua muda mrefu kutoa taarifa ya kasoro zilizojitokeza kwa
upande wa serikali katika udhibiti wa vurugu hizo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>“Vyombo
kama tume ya haki za binadamu ndivyo vinavyojenga imani mbele ya jamii na
kuisaidia serikali kujikosoa lakini kuchelewa kwa taarifa za tathmini yao
kuhusiana na zoezi zima vinafanya tukose imani nacho na kuonekana ni mkono
mwingine wa serikali kukusanya taarifa juu wananchi wanasema nini”. Alilalamika
mama aliyebambikizwa kesi na polisi.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Dhamana zilizotakiwa kutolewa
mahakamani ni kiashiria kingine cha kuwafanya wananchi waliokuwa kwenye tukio
hilo wakose haki mbele ya chombo hicho ambapo kesi mojawapo kila mtu alipaswa
kudhaminiwa kwa Tshs 107 Milioni taslimu! Hiki ni kiasi kikubwa kwa watu ambao
kipato chao ni kidogo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Viwango hivi ni dhahiri vililenga kuwakatisha
tama wananchi katika mchakato mzima wa kupata haki kwa watuhumiwa wa tukio
hilo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Mwanaharakati mmoja anaeleza kuwa kwa
ujumla kuna ukandamizaji mkubwa katika suala la tangu ukamataji hadi ufikishaji
wa watuhumiwa mahakamani na hata uendeshaji wa mashauri yao na kuomba msaada wa
kisheria kwa watuhumiwa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Vyovyote vile<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>suala la Mtwara, linahitaji busara na hasa
kutoa nafasi watu hawa wakasilizwa. Kuendelea kutumia nguvu za dola na kuwanyamazisha
ni kuweka kiporo cha maswali yatakayoulizwa kesho na keshokutwa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Na,</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: "Times New Roman";">+255 754 6331 22</span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<br /></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-61214987660689059842013-12-09T23:55:00.002-08:002013-12-09T23:55:32.596-08:00GESI HAITOKI<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31130" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31132" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">GESI HAITOKI! IKITOKA ITABADILIKA KUWA
MAJI: KINJEKITILE NAMBA 2</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31128" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"><br /></span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30939" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30938" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ikumbukwe awali lilishatolewa tamko
kutoka Msimbati kwa bibi Samoe Mtiti (106) kuwa ikiwa serikali itaendelea
kulazimisha mchakato wa gesi bila kusikiliza hoja za wananchi angegeuza gesi
kuwa maji, hatua ambayo ililazimu mbinu mbalimbali za kumshawishi bi Samoe
zifanyike ili hali hiyo isijitokeze. Wakazi wa Mtwara, wanaamini nguvu za<span> </span>Bibi Mtiti, kwamba ana uwezo wa kubadili gesi
kuwa maji, na akitaka gesi isitoke, haiwezi kutoka!</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31135" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31134" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Ni yale yale ya Kinjekitile, ya
kubadilisha risasi kuwa maji. Kwa haraka na kwa tabia ya kuangalia mambo juu
juu unaweza kusema kwamba huu ni upuuzi. Lakini hapa kuna kitu cha kujifunza.
Ule muujiza wa Kinjekitile, wa kugeuza risasi kuwa maji uliwapatia wapiganaji
hamasa na nguvu za kupambana na wavamizi. Hata kama walishindwa, walikufa kwa
heshima kubwa wa kipambana na silaha za kisasa kutetea nchi yao. Historia inawatambua
na kuwaheshimu. Hivyo si lazima miujiza hii iwe upuuzi wakati wote.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31138" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31137" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kuna habari za kuaminika kwamba Januari
24, 2013 gari lenye namba za usajili T609 BXG la mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni
ofisa wa idara nyeti liliteketezwa kwa moto na wananchi wa Msimbati kwa kile
kinachoelezwa kuwa lilifika kumteka bi Somoe ambaye kijijini hapo anajulikana
kama mkuu wa kaya. Wako tayari kumlinda bibi huyu kwa gharama yoyote ile, kwa
vile wanaamini ana nguvu za kutenda miujiza.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31142" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31141" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Imani hii kwa Bibi Samoe Mtiti,
inaonyesha wazi jinsi suala zima la Gesi, halijaelezwa vizuri. Watu hawana
elimu juu ya Gesi na matumizi yake. Kama bado wanaamini Gesi inaweza kubadilika
kwa nguvu za miujiza ikawa maji, bado kuna kazi kubwa. Serikali ina wajibu
mkubwa wa kuwaelimisha watu wa Mtwara. Kutumia jeshi kuwapiga na kuwanyamazisha
si njia sahihi ya kuleta mabadiliko na maendeleo. Kinachohitajika ni kuwasikiliza,
kujadiliana nao, kuwashirikisha na kuwaelimisha.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31145" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31144" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Vinginevyo watasimama kidete na miujiza
ya Bibi Samoe Mtiti, itawatia hamasa kupigania haki yao na kukubali kufa, ili
historia isiwacheke baadaye. Kama nilivyosema hapo juu si lazima miujiza iwe
upuuzi wakati wote. Ni wazi hakuna muujiza wa kuibadilisha gesi kuwa maji na
wala risasi kugeuka na kuwa maji. Lakini muujiza wa kubadilisha akili za mtu,
akaacha kufikiri na kutenda kama wanyama wengine upo; tunashuhudia vitendo vya
kujitoa muhanga kwa matumaini kwamba kule “Mbinguni” watakuta maisha mazuri na
dhawabu kubwa.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31148" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31147" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Hivyo kiongozi yeyote mwenye busara,
anaposhughulika na watu wenye Imani aina ya Bibi Samoe Mtiti, ni lazima awe
makini kutotumia nguvu. Maana imani ikikolea, mtu anaacha kufikiri na kuyaweka
maamuzi yake mikononi mwa watu wengine. Wanachosema anafuata kwa kuogopa
kuambiwa hana imani! Au kuambiwa yeye ni msaliti! Ni vigumu kupambana na mtu wa
namna hii, hata kama serikali ina nguvu za kutisha.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31152" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31151" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mzee, aliyetuelezea habari hizi za Bibi
Samoe Mtiti, wakati tukifanya utafiti juu ya vurugu za Mtwara, alikuwa <span> </span>akijaribu kutufafanulia umuhimu wa
ushirikishwaji. Kwamba serikali haikuzingatia hili, na watu wa Mtwara
hawakushirikishwa juu ya uchimbaji wa gesi, kwani raslimali gesi sasa
inazungumzwa kama bidhaa haramu kama ilivyo bangi kwenye vyombo vya dola!
Ukitamka suala la gesi kwa wanamtwara wanakuona kama vile umetumwa kuwadodosa
ili uwachomee utambi kwenye jeshi na hatimaye wapelekwe Gwantanamo kuteswa;
hiki ni kituo cha Jeshi cha Nalyendele, ambacho kimebatizwa jina la Gwantanamo,
kutokana na vitendo vya mateso vinavyoendelea kwenye kituo hicho.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31155" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31154" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa maoni ya mzee huyo ni kwamba kwa
namna yoyote ile ridhaa ya wananchi katika utekelezaji wa miradi inayolenga
kutumia raslimali iliyolindwa kwa miongo kadhaa na vizazi vya jamii ya eneo
ambapo mradi unakusudiwa kutekelezwa ni muhimu na vyema kuheshimiwa ili
kuhakikisha kwamba laana za vizazi hivyo hazijengwi katika kizazi kinachofuata
ndivyo imani za asili zinavyotambuliwa.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31158" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31157" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wananchi wanaolizungumzia suala la
gesi<span> </span>kwa tahadhari wanatamka bayana kuwa
vyombo vya usalama vinavyoshughulikia ukusanyaji wa taarifa
havikujipa kazi ngumu kujua hasa kwa nini wananchi wanashinikiza gesi
haitoki bila kujali imani, vyama na hali zao. Hili lilichukuliwa kama ajenda ya
kisiasa na watoa taarifa ngazi za juu na ndiyo sababu katika mazungumzo ya
viongozi wa ngazi ya kitaifa wanaliona kama lilikuwa la kisiasa kumbe hii ni
ajenda ya wana-Mtwara imezingatia zaidi maslahi na ustawi wa wana Mtwara na ni matokeo
ya maumivu ya muda mrefu kucheleweshwa kwenye safari ya kufikia maendeleo ya
kweli. </span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31160" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31159" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Hivyo maamuzi ya matumizi ya nguvu
ndiyo yakachochea zaidi ufa wa mahusiano baina ya serikali na wananchi
hadi sasa ambapo kama mtu anafanya utafiti atabaini kuwa kati ya watu kumi
unaokutana nao ni nadra kukutana na mtu anayesifia matunda tarajiwa ya miradi
ya gesi kwa Mkoa wa Mtwara huku wengi zaidi wakilaumu mazingira ya utekelezaji
mradi huo.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Matumizi ya nguvu kubwa za dola katika
masuala yanayohitaji utashi wa watu ni kiashiria kuwa kuna pengo la mahusiano
baina ya serikali na wananchi na hivyo kuhitaji chombo kingine kuunganisha
makundi yanayotofautiana.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wananchi wa Mtwara wanasema ukimya
uliopo sasa si kwamba ni utulivu na amani bali ni utulivu pasipo amani, na
wananchi wanafanya hivi kupisha udhalilishaji na manyanyaso ya matumizi makubwa
ya nguvu za dola. </span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kimsingi tangu kutolewa agizo la
kutoitishwa mikutano ya wazi inayojumuisha watu kwenye maeneo ya wazi, Mtwara
imekuwa kisiwa kwa muda sasa kutokana na wananchi kutopata fursa ya kukutanika
kujadili maendeleo ya mkoa wao.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Hivi sasa <span> </span>msimu wa korosho umeanza lakini hawawezi
kukubaliwa kuitisha mikutano ya kujadiliana juu ya maslahi ya wakulima wa korosho
kutokana na agizo hilo na kwamba ukifanya mkusanyiko wowote utakuwa umevunja
amri halali ya serikali.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Utekelezaji wa kamata kamata ya
watuhumiwa wa vurugu za Mei 23 ulioendeshwa kwa usiri mkubwa na nyakati za
usiku kwa kutumia wanajeshi, umetajwa pia kufanywa kwa uonevu mkubwa <span> </span>kwa sababu hata wale <span> </span>ambao hawakuwepo mazingira ya tukio kubebwa
kwa chuki na tofauti zilizokuwepo baina ya baadhi ya viongozi wa mitaa na
wananchi wao.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31194" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31193" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa ujumla kuna ukandamizaji mkubwa katika
suala la tangu ukamataji hadi ufikishaji wa watuhumiwa mahakamani na hata
uendeshaji wa mashauri yao na kuomba msaada wa kisheria kwa watuhumiwa. Dhamana
zilizotakiwa kutolewa mahakamani ni kiashiria kingine cha kuwafanya wananchi
waliokuwa kwenye tukio hilo wakose haki mbele ya chombo hicho ambapo kesi
mojawapo kila mtu alipaswa kudhaminiwa kwa Tshs 107 Milioni taslimu! Hiki ni
kiasi kikubwa kwa watu ambao kipato chao ni kidogo.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31191" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31190" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Viwango hivi ni dhahiri vililenga kuwakatisha
tama wananchi katika mchakato mzima wa kupata haki kwa watuhumiwa wa tukio
hilo.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31188" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31187" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kulingana na maelezo ya wananchi, kwa sasa
chombo kinachopewa nafasi katika kuunganisha mahusiano baina ya wananchi na
mamlaka ya serikali ni mijadala ya pamoja ikihusisha asasi za kiraia ili
kurejesha mawasiliano na kuaminiana ambako kumetoweka.</span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31184" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31183" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31182"> </span></span></div>
<div class="yiv9073248315MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31163" style="line-height: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_31162" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus Karugendo</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-4721121696901810682013-12-09T23:53:00.001-08:002013-12-09T23:53:29.962-08:00AGPAHI 3<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30370" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30369" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA: USHUHUDA KUTOKA GEITA NA SHINYANGA.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30367" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30200" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30199" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tarehe 26 Septemba,2013 Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mheshimiwa Magalula S.
Magalula, alifungua jengo la kliniki ya huduma na matunzo kwa watu wanaoishi na
virusi vya Ukimwi (VVU), katika kituo cha Afya Masumbwe wilaya mpya ya Mbogwe –
Mkoa wa Geita. Na tarehe 27 Septemba 2013 Mheshimiwa AnnaRose Nyamubi, Mkuu wa
Wilaya ya Shinyanga, akafungua jengo jingine la Kliniki ya tiba na matunzo kwa
watu wenye VVU, katika kituo cha Afya Kambarage – Shinyanga mjini.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30374" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30373" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Majengo haya mawili, la Masumbwe na la Shinyanga, yamejengwa na Shirika la Kitanzania
AGPAHI(Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative) kwa msaada wa watu wa
Amerika, kupitia shirika la CDC (Centre for Disease Control).</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30387" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30386" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Shirika la AGPAHI lilianza kazi nchini Tanzania, mwaka wa 2011, (Kwa
kuzaliwa na Shirika la Kimataifa la EGPAF ‘Elizabeth Glaser Pediatric AIDS
Foundation’ na kuendeshwa na watanzania) linafanya kazi zake katika Mikoa ya
Geita, Shinyanga na Simiyu katika jitihada za kupambana na Virusi vya Ukimwi
katika Mikoa hii mitatu kwa msaada wa watu wa Marekani na kwa kusaidiana na Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia<span>
</span>Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala
za Mikoa na Serikali za mitaa yaani TAMISEMI ili kuwezesha upatikanaji wa tiba
na matunzo kwa watu wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi lakini pia
upatikanaji wa huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30389" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30392" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30391" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa kipekee shirika hili la AGPAHI, linakazania huduma hii ya kuzuia virusi
kutoka kwa mama mwenda kwa mtoto. Kwa maoni ya shirika hili jambo hili
linawezekana kabisa, kila mtu akitimiza wajibu wake; wananchi wakapima afya zao
kwa hiari, serikali na wadau wengine wakatoa huduma za uhakika, tunaweza kwa
asilimia 100 kuzuia virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na hatimaye
kutokomeza virusi kwa watoto.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30395" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30394" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Majengo haya mawili yaliyofunguliwa Masumbwe na Shinyanga, ni mazuri na
yamejengwa kisasa. Yana idadi ya vyumba 5 ambavyo ni chumba cha usajili wa
wagonjwa, chumba cha ushauri nasaha, vyumba viwili vya waganga na chumba cha
kutunzia dawa. Pia majengo<span> </span>haya yana
vyoo vizuri na vya kisasa. Ni majengo yanayolenga kupunguza unyanyapaa na watu
wenye virusi kujiona wametelekezwa. Huko nyuma kwenye vituo vya afya huduma hii
ilitolewa kwenye chumba kimoja na msongamano ulikuwa mkubwa kiasi cha
kuwakatisha tama wagonjwa na wengine kuamua kuikimbia huduma hii.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30398" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30397" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na majengo mawili yaliyofunguliwa, AGPAHI, inafanya kazi pamoja na
watendaji wa Mkoa na Halmashauri katika kuboresha huduma kwenye vituo 68
vinayotoa huduma za matunzo na matibabu kwa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI na
vituo 284 vinavyotoa huduma za kukinga maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda
kwa mtoto(PMTCT) katika mikoa hiyo mitatu.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30401" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30400" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kliniki ya Masumbwe ilianza kutoa huduma ya matunzo na matibabu mwaka 2006
kwa kupata msaada kutoka shirika la CDC chini ya uratibu wa Elizabeth Glaser
Pediatric Aids Foundation na baadaye AGPAHI (Tunaweza kusema kwamba AGPAHI ni
mtoto wa Elizabeth Glaser Pediatric Aids Foundation). Hadi kufikia Juni 2013,
kliniki ya Masumbwe imeweza kuhudumia jumla ya wateja 1,437, wanaume wakiwa 538
na wanawake 899.<span> </span>Kati yao <span> </span>ni watoto 106 walio chini ya miaka 15. Katika
kliniki hii, wateja 1,030 wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU na UKIMWI
na kati yao ni watoto 79 walio chini ya umri wa miaka 15. Kufikia Juni 2003
jumla ya wateja 714 walikuwa hai na kati yao watoto 50.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30404" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30403" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kliniki ya Kambarage- Shinyanga nayo ilianza kutoa huduma mwaka 2006. Nayo
kufikia Juni 2013, imeweza kuhudumia jumla ya wateja 1,713 wanaume wakiwa 488
na wanawake 1,225.Kati yao ni watoto 113 walio chini ya umri wa miaka 15.
Katika kliniki hii wateja 854 wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU na
UKIMWI. Kati yao ni watoto 66 walio chini ya umri wa miaka 15. Hadi Juni mwaka
huu jumla ya wateja 553 walikuwa hai na wanaendelea kutumia dawa za kupunguza
makali ya VVU na UKIMWI, na kati yao watoto 9 chini ya miaka 15 wako hai.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30407" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30406" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Takwimu hizi zinaonyesha umuhimu wa kliniki za tiba na matunzo kwa watu
wanaoishi na VVU na UKIMWI, maana idadi ya vifo inapungua sana na hasa
uwezekano wa Mama wenye virusi kuzaa watoto wasiokuwa na virusi. Ushuhuda
uliotolewa na wanawake 16 wa Kliniki ya Masumbwe, ni kwamba jambo hili
linawezekana. Wanawake hawa wanaishi na virusi, lakini kwa vile wanatumia dawa
za kufubaza virusi, wamezaa watoto wasiokuwa na virusi. Tatizo linalojitokeza
ni mwitikio mdogo wa wanawake wajawazito kupima ili kujua hali zao. Mkurugenzi
mtendaji wa shirika la AGPAHI Bwana Laurean Rugambwa, kwenye risala yake kwa
Mgeni Rasmi, wakati wa kufungua jengo la kutoa huduma ya tiba na matunzo kituo
cha Masumbwe, wilaya na Mbogwe, alieleza<span>
</span>tatizo hili: “ Ndugu mgeni rasmi, hatua ya kwanza kabisa katika jitihada
za kuzuia maambukizi ya virusi toka kwa mama kwenda kwa mtoto ni kupima kwa hiari
wajawazito wote. Taarifa zinaonyesha kuwa kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi
Juni mwaka huu, kinamama 2,649 tu kati ya 6,796 (39%) waliopimwa hali zao
katika wilaya ya Bukombe na Mbogwe ikiwamo. Kiwango hiki ni kidogo sana hivyo
ndoto ya kutokomeza maambukizi kwa watoto haitaweza kutimia. Hivyo ni wajibu
wetu sote kuhakikisha tunafanya kila linalowezekana kuwafikia akinamama wengi
zaidi”</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30411" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30410" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na kwa upande wa Shinyanga, Bwana Laurean Rugambwa, alieleza: “.. Taarifa
zinaonyesha kuwa kwa kipindi cha Mwezi Aprili hadi Juni ni kinamama 1857 tu
kati ya 2968(63%) ndio waliopimwa hali zao katika manispaa ya Shinyanga. Vile
vile, katika halmashauri ya wilaya Shinyanga vijijini, kipindi cha Aprili hadi Juni,
akinamama 2,434 tu ndio waliopima hali zao kati ya 4,150 (59%) ya akinamama
ambao waliotakiwa kupima hali zao. <span> </span>Kiwango hiki bado kiko chini hivyo ndoto ya
kutokomeza maambukiki kwa watoto haitaweza kutimia.”</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30414" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30413" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ushuhuda huu wa Bwana Laurean Rugambwa, mkurugenzi mtendaji wa AGPAHI,
unaonyesha kwamba “TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA” kila mwananchi akitimiza
wajibu wake. Jambo hili haliwezi kutimia kwa hotuba tu za majukwaani bila kuhimizana,
kushauriana, kuelekezana na kuwa na mifumo ya utekelezaji. Panahitajika
jitihada za pekee kuhakikisha wanawake wajawazito wote wanapima hali zao ili
kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Ni lazima sote kushiriki <span> </span>kama alivyobainisha Bwana Laurean Rugambwa
kwenye risala yake:</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">“ ...Zaidi ya hayo, wanaume lazima tubadili tabia, na pia tuwe tayari
kupimwa afya zetu tukiwa pamoja na wenzi wetu. Tukifikia hatua hii, tutaweza
kuzuia maambukizi ya VVU kwa watoto wanaozaliwa kwani baba na mama watakuwa
wanajua afya zao kabla ya kuamua kupata mtoto, na mama akipata ujauzito afahamu
kwamba anaweza kupata dawa za kuzuia maambukizi kutoka kwake kwenda kwa mtoto.
Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumezuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda
kwa mtoto”</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mbali na changamoto hii ya idadi ndogo ya wajawazito kupima hali zao, Bwana
Laurean Rugambwa, alielezea changamoto nyingine: “ Ndugu mgeni rasmi,
changamoto kubwa tunazozipata katika manispaa hii ya Shinyanga ni kupotea kwa
wateja walioanza kupata huduma katika kliniki zetu, unyanyapaa wa watu wanaoishi
na virusi vya ukimwi katika jamii na ushiriki mdogo wa wanaume katika huduma za
uzuiaji wa maambukimi ya VVU toka kwa mama kwenda kwa mtoto”.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Changamoto hii ya kupotea kwa wateja, pamoja na jitihada zinazofanywa na
AGPAHI na wadau wengine kuwarudisha, ziko kwenye maeneo yote ambayo AGPHAI, inatoa
huduma hizi; Mkoa wa Shinyanga, Geita na Simiyu. Chanzo cha kupotea kwa wateja
hawa, ni waganga wa jadi na imani za kidini. Kuna waganga wa jadi
wanaowaaminisha watu kwamba wana uwezo wa kutibu UKIMWI, lakini ni ujanja wa
kujipatia fedha. Pia kuna viongozi wa kiroho wanaoamini kwamba UKIMWI utapona
kwa miujiza ya Mungu, matokeo yake ni watu wanaotumia dawa za kufubaza virusi,
kupoteza maisha wanapoacha kutumia dawa na kukimbilia kwa waganga wa jadi na
imani za kidini.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Changamoto nyingine iliyotajwa na Bwana Laurean Rugambwa, katika jitihada
za shirika lake kuhudumia watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi ni “ Mheshimiwa
mgeni rasmi, pamoja na juhudi zetu za kutoa huduma, tunakwamishwa na uhaba wa
watoa huduma katika vituo vilivyo vingi, na wengine kuacha kazi. Hapa inabidi
tuangalie kwa jinsi gani tunaweza kuboresha huduma hizi kwa kutumia rasilimali
watu zilizopo”</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30417" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30416" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Akijibu risala ya Mkurugenzi mtendaji wa AGPAHI, Mkuu wa Mkoa wa Geita,
alisema: “ Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo AGPHAI
katika kuendelea kutatua changamoto hizi. Naomba nitumie nafasi hii kuwataka
viongozi wote hasa timu za uendeshaji wa afya na Halmashauri zote kuhakikisha
kuwa wanatengeneza mpango wakuwezesha vituo vingi vya afya kuwa na uwezo wa
kutoa huduma za tiba na matunzo na hivyo kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma
hizo kwa urahisi.<span> </span>Halikadhalika,
halmashauri kupitia idara zake mbalimbali zitengeneze utaratibu unaozihusisha
idara mbalimbali nje ya idara ya afya kuhakikisha kuwa wale wote waliokwisha
andikishwa kwenye huduma za tiba na matunzo wanaendelea kubaki kwenye huduma.
Na ni muhimu zaidi kutengeneza utaratibu utakaowezesha kuwafuatilia na
kuwarudisha kwenye huduma wale wote walioacha kuhudhuria kwenye kliniki zao”.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30429" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30428" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Msimamo huu wa Mkuu wa Mkoa wa Geita, ndio uliokuwa Msimamo wa Mkuu wa
Wilaya ya Shinyanga, hivyo msimamo wa Serikali. Tuna imani kwamba Serikali
ikitekeleza msimamo huu na kuhakikisha kuna mifumo ya kuwadhibiti waganga wa jadi
wenye ujanja wa kutaka kujipatia fedha kwa ulaghai, imani za kidini ambazo
zinawapumbaza watu wenye virusi kuamini kupona kwa miujiza, kuzuia watu
kutoroka huduma na tiba kwenye kliniki hizi za watu wanaoishi na Virusi, mifumo
ya kuhakikisha wajawazito wote wanapima hali zao, wanaume nao wanashiriki
kwenye zoezi la upimaji, wahudumu wa afya wanapatikana, unyanyapaa unapungua na
kila mwananchi anatimiza wajibu wake katika zoezi zima la kutokomeza UKIMWI,
hapana shaka kwamba Tanzania bila UKIMWI inawezekena.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30426" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30424" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv4680100086MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_30422" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 6331 22</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-50390283125538360202013-12-09T23:50:00.003-08:002013-12-09T23:50:36.452-08:00MWALIMU NA WATOTO WAKE<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29057" style="text-align: justify;">
<b id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29061"><u id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29060"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29059" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">MWALIMU
NA WATOTO WAKE</span></u></b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"></span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29071" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28976" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28975" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nilikuwa sikupanga kuandika makala hii. Nimekuwa
nikijizuia kuandika juu ya Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Ninaogopa
kuwekwa kwenye kundi la wanafiki, wanaoandika kumlilia na kumkumbuka Mwalimu,
lakini matendo yao ni tofauti kabisa na ya Mwalimu. Wanamlilia Mwalimu wakati
wanakataa Shirikisho la Afrika ya Mashariki. Wanamlilia Mwalimu wakati
wanawafukuza wakimbizi na wahamiaji haramu. Wanamlilia Mwalimu<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29053"> </span>wakati wanawagawa watanzania katika makundi
ya vyama, makabila na dini. Wanamlilia Mwalimu wakati wanayashibisha matumbo
yao na kulitelekeza taifa. Wanamlilia mwalimu wakati wana ukumbatia ubepari na
kuabudu fedha. Wanamlilia mwalimu wakati wanashindwa kuitetea na kuilinda
Katiba ya Taifa letu. Wanamlilia Mwalimu wakati wanaitelekeza lugha yetu ya
Kiswahili na kutupilia mbali utamaduni wa taifa letu. Mwalimu, alikuwa Mjamaa,
alikuwa mtetezi wa haki za binadamu, alikuwa msomi na mchambuzi, alikuwa
mwandishi, alikuwa na hekima na busara. Alikuwa na upendo na huruma, zaidi ya
yote alikuwa na “vision”. Mwalimu hakutawaliwa na ushabiki wa kisiasa.
Alikwenda kwa hoja, ukimshinda kwa hoja anakuunga mkono. Hakuna anayeyafuata ya
Mwalimu. Wengi wanaojifanya kumkumbuka ni wanafiki wakubwa. Mifano mingi ya
wanafiki. Sikupenda nichanganywe na wanafiki hao, hivyo niliamua kukaa kimya
kuandika juu ya mwalimu.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29086" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29089" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29088" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Leo nimeamua kuandika kwa vile mhariri wa Raia
mwema, amenitumia ujumbe na kuniomba kuandika kitu juu ya mwalimu, maana Jumatatu
ni Nyerere Day. Na kwamba siku hiyo litakuwepo toleo maalumu la Mwalimu, hivyo
nina uhuru kuandika maneno mengi kiasi nitakacho. Juu ya mwalimu ni vigumu
kuandika maneno yaliyo chini ya elfu moja! Kwa wale wasiomfahamu Mwalimu,
vizuri watashindwa kuandika hata maneno mawili. Lakini wale wanaomfahamu, wale
wanaofahamu uwazi wake, wema wake, uzalendo wake, umaskini wake, ni lazima
washawishike kama mimi kuandika mengi. Kwa vile Nyerere Day, ni mara mmoja kwa
mwaka hakuna hatari ya watu kuzichoka makala ndefu.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29091" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29094" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29093" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Lakini la msingi lililonisukuma kuandika makala
hii ni kitendo cha kukutana na Mtoto wa Mwalimu kwenye Daladala. Nilipanda daladala
ya Posta-Mwenge. Tulipofika kituo cha Palm Beach, mtoto wa Mwalimu Nyerere,
ambaye nilitokea kufahamiana naye siku za nyumba, alipanda kwenye Daladala. Sikushangaa,
ila kusema kweli si jambo la kawaida na hasa kwenye nchi za Afrika; mtoto wa aliyekuwa
Rais wa nchi, tena rais wa kwanza na Baba wa taifa kupanda daladala si jambo la
kawaida. Huyu angekuwa na gari lake, na dreva wa kumwendesha. Huyu angekuwa na
ulinzi mkali nk. Lakini Mtoto wa Mwalimu, aliingia kwenye<span> </span>daladala kama msafiri yeyote yule. Nina imani
ndani ya daladala ile ni wachache au labda hakuna mwingine zaidi yangu mimi
aliyetambua kwamba huyo alikuwa mtoto wa Baba wa Taifa.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29097" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29096" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Siku nzima nilitafakari juu ya Mwalimu.
Nilitafakari juu ya upekee wake. Nilitafakari juu ya uongozi wake, juu ya
uzalendo wake, juu ya mapenzi yake kwa taifa la Tanzania na watu wake. Lakini
zaidi nilitafakari juu malezi ya watoto wake: Mwalimu aliwapatia watoto wake
malezi ambayo <span> </span>watoto wote watanzania waliyapata.
Watoto wake walisomea shule zile walikosomea watoto wote wa Tanzania. Mwalimu
aliamua kutoa elimu ya bure si kwa watoto wake, bali kwa watoto wote wa
Tanzania. Kama si mpango wa Mwalimu, wa kutoa Elimu ya bure watu wengi leo hii
wasingekuwa na elimu waliyonayo.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29099" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29102" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29101" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Makongoro Nyerere, alipokuwa anasoma Tabora Boys,
nilikuwa Seminari Kuu ya Kipalapala Tabora. Nilitokea kumfahamu kwa karibu.
Alikuwa anakuja kutembea Kipalapala na kula mapera kama<span> </span>watoto wengine. Alikuwa anapenda muziki na
kuimba – pale Kipalapala tulikuwa na bendi ya muziki, hivyo alikuwa akijichanganya
kwenye bendi hiyo na kupiga gita na kuimba. Alikuwa akitembea kutoka Tabora
Boys hadi Kipalapala kwa miguu kama<span>
</span>watoto wengine. Bila kuambiwa kwamba ni mtoto wa Rais, ilikuwa vigumu
kutambua. Alikuwa hana majivuno, kwa sababu alikuwa amelelewa katika mazingira
ya kujitambua kwamba yeye hana tofauti na watoto wengine.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29105" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29107" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29109" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwalimu hakumpatia mtoto wake yeyote yule cheo cha
upendeleo ndani ya serikali yake na wala hakuwashawishi watoto wake kuingia
kwenye siasa. Sote tulishuhudia Makongoro, alivyojiingiza kwenye siasa – badala
ya kuiingia kwenye chama cha Baba yake, akajiunga na upinzani. </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29111" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29114" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29113" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Rose Nyerere, aliingia Bungeni, baada ya kifo cha Baba
yake. Historia haituonyeshi mtoto wa Mwalimu, aliyependelewa kwa aina yoyote
ile. Kila mmoja mahali alipo, amepambana kama watoto wengine wote
wanavyopambana na maisha na kufanikiwa.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29116" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29119" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29118" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mwalimu , hakuwapendelea watoto wake. Aliwapenda
watoto wote wa Tanzania. Alijenga shule za watoto wote<span> </span>wa Tanzania, alijenga vyuo vya watoto wote wa
Tanzania. Lengo lake kubwa lilikuwa kuiandaa Tanzania<span> </span>yenye neema kwa<span> </span>vizazi vijavyo . Mwalimu, hakuwapeleka watoto
wake kusoma nje ya Tanzania. Kama kuna mtoto wake aliyefanikiwa kusoma nje,
atakuwa alisaidiwa na Wamisionari. Ninakumbuka Mwalimu mwenyewe akiwa hai,
alisema kwamba mmoja wa watoto wake alipata msaada kusoma Canada, na kwamba
msaada huo ulitolewa na wamisionari.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29122" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29125" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29124" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Nina imani kama Mwalimu angekuwa hai bado, wajukuu
zake wangesoma kwenye sekondari za kata! Mwalimu, hakupenda kuwatenga watoto
wake na jamii. Watoto wake<span> </span>walijiunga na
Jeshi la Kujenga taifa kama watoto wengine. Na kule waliishi na kufanya kila
kitu kama watoto wengine wote walivyokuwa wakifanya.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29128" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29131" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29130" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Leo hii wale wote wanaojifanya wanamlilia Mwalimu,
ni nani anafuata mifano yake? Ni mtoto gani wa kiongozi anapamba daladala? Ni
mtoto gani wa kiongozi anasoma kwenye sekondari za kata? Ni mtoto gani wa
kiongozi asiyesoma nje ya nchi? Tumesikia habari za<span> </span>baadhi ya watoto wa viongozi kuwashikia watu
bastola, lakini hawafikishwi mbele ya sheria. Tumeshuhudia watoto wa viongozi
wakiingizwa kwenye siasa na kupata nafasi za juu. Tumeshuhudia watoto wa
viongozi wakifanya biashara na kupata upendeleo.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29133" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29135" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29137" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Wapo baadhi ya watu wanaomlaumu sana mwalimu kwa
siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea. Wengine wanamlaumu Mwalimu kwa kile
wanachokiita “Kuitelekeza” familia yake, kwamba hakuwatafutia watoto wake
nafasi nzuri katika mfumo wa serikali. Wanasema mwalimu alikosea, wanasema
mwalimu alidumaza uchumi wetu. Ukweli ni kwamba Mwalimu, aliona mbali zaidi <span> </span>yetu. Siasa ya Ujamaa na Kujigemea, ilikuwa
silaha kubwa ya kupambana na Ukoloni mambo leo. Mwalimu, alijua wazi kabisa,
kwamba utafika wakati tuzidiwe nguvu na Ukoloni Mambo leo, alijua wazi kwamba
tutafikia mahali tuvamiwe na wawekezaji kwa mgongo wa Utandawazi. Hivyo alitaka
kulijengea Taifa misingi ya kujilinda. Kama <span> </span>tungefanikiwa kujenga Taifa la Ujamaa na Kujitegemea,
kamwe tusingemezwa na Utandawazi, bali tungeshiriki kwenye utandawazi. Sasa,
hakuna cha kushiriki ni kumezwa kabisa. Hakuna cha kushiriki bali ni utajiri
wetu kuporwa na wageni. Badala ya kujenga uchumi wa taifa letu, tunajenga na
kukuza uchumi wa mataifa mengine. Badala ya kuulinda Uhuru wetu, tunakubali
kuwa “watumwa”!</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29140" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29139" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kwa mtazamo wangu, ni kwamba Mwalimu alifanya
makosa mawili katika maisha yake: Kosa la kwanza, ambalo limemgharimu sana, ni
kuwaamini sana watu. Mwalimu, aliwaamini watu. Watu hawa aliowaamini mwalimu,
ndio wale wale walioangusha na kuzika Vision yake. Wale aliowaamini ndio
waliolizika Azimio la Arusha kule Zanzibar. Ni<span>
</span>watu wachache wa aina ya Mzee Kawawa, walibaki waaminifu kwa Mwalimu.
Wengine walikuwa wanafiki, walitaka vyeo na utajiri wa haraka. Walionyesha
unyenyekevu kwa Mwalimu, walizungumza kama Mwalimu na kuvaa nguo kama za
Mwalimu. Baada ya Mwalimu, kutoka madarakani, watu hawa walibadilika haraka,
walianza kuongea lugha nyingine na kuvaa nguo za Kizungu. Kosa <span> </span>la pili la Mwalimu, ni kwenda Haraka. Mfano,
hakujipatia nafasi kufanya maandalizi ya kutosha kabla ya kufanya uamuzi wa
Azimio la Arusha. Hakuwaandaa watu kupokea Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.
Alifanya haraka ya kutaifisha, viwanda, mashule na mahospitali. Uharaka huu,
ambao haushangazi kwa Mwanamapinduzi, kama alivyokuwa Mwalimu, ndiyo sababu
kubwa ya kuanguka kwa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29142" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29145" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29144" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Mimi ni kati ya watu wanaomlaumu Mwalimu kwa
uharaka wake. Mimi ni kati ya watu wanaoamini kwamba labda kama Mwalimu,
angefanya maandalizi ya zaidi ya miaka 20 – watu wakajadili, wakatafakari na
kutafuta uzoefu wa ujamaa katika nchi za ujamaa za wakati ule, labda Ujamaa
wetu usingekufa. Lakini pia mimi ni miongoni mwa watu wanaotetea Uharaka wa
Mwalimu. Ni kweli kwamba aliona mbali. Alifikiri kwamba bila kujenga Ujamaa kwa
haraka, tungemezwa bila maandalizi.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29147" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29150" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29149" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Baada ya Uhuru, Mwalimu Nyerere alitangaza maadui
wa Taifa letu kwamba ni Maradhi, Ujinga na Umaskini. Na kwamba silaha pekee ya
kupamba na maadui hawa ni: Ardhi, Siasa safi, Uongozi bora na<span> </span>watu. Aliamini pia kwamba ili haya yote yafanyike
ni lazima tuwe na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Siasa hii, ililinda utajiri
wa Taifa letu. Hatukusikia malalamiko ya madini kusombwa na kupelekwa nje,
hatukusikia wizi wa magogo, hatukuzikia vitalu vya wawindaji. Tulisikia Kisomo cha
watu wazima, tulisikia Siasa ni Kilimo, tulisikia mvua za kwanza ni za kupandia
n.k</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29152" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29154" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29156" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Kama nilivyosema hapo juu, ni kwamba Mwalimu
hakuwapendelea watoto wake, bali aliwapenda watoto wote wa Tanzania. Wimbo wetu
wa Taifa, unaonyesha wazi jinsi Mwalimu alivyokuwa na upendo kwa watoto kama
taifa la Kesho. Watoto wanatajwa na kuombewa baraka nyingi katika wimbo huu wa
Taifa. Lakini upendo wake kwa watoto haukuishia hapo, ulivuka mipaka ya
Tanzania, na kuenea kwenye bara lote la Afrika. Vituo kama kile cha Mazimbu,
kule Morogoro, vilianzishwa ili kuwapatia Elimu ya ukombozi watoto wa wakimbizi
kutoka Msumbiji. Lakini pia nchi nyingine nyingi za Afrika kama Angola, Botswana,
Zimbabwe, Namibia n.k. zilipata Kivuli kizuri sana<span> </span>kutoka kwa<span>
</span>Mwalimu.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29159" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29158" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tunaposherehekea Nyerere Day, ni watanzania
wangapi, ni viongozi wangapi wanawapenda watoto wa Tanzania, kama alivyowapenda
Mwalimu Nyerere? Ni nani anahakikisha watoto wetu wanapata malezi bora, elimu
bora na afya njema? Ni nani anawaandalia watoto wetu Tanzania ya kesho yenye
neema? Hadi leo hii Taifa letu limeshindwa kusimamia usafiri salama wa watoto
wetu kwenda shule. Watoto wanasukumwa na kunyimwa nafasi kwenye daladala.
Wasomi wa vyuo vikuu wanasumbuka kupata mikopo. Maadili ya watoto wetu
yanakwenda ovyo, watoto wameachwa bila mtu wa kuwaelekeza. Tunachimba madini na
kuwaachia watoto wetu mashimo, tunakata miti kwa fujo na kuuza magogo nchi za
nje na kutunza pesa hizo kwenye uchumi wa nchi za nje. Viongozi wanawapendelea
watoto wao, wanawasomesha nchi za nje kwenye vyuo vizuri. Watoto wengi
wanaobaki wanajengewa Sekondari za kata!</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29182" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29163" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29162" lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Tumkumbuke Mwalimu Nyerere, kwa kujiwekea mkakati
wa kuongeza mapenzi kwa watoto wetu. Tuwapatie watoto wetu elimu bora, mazingira
bora na yenye kuvutia, afya njema na kuwajengea Tanzania ya kesho yenye Neema.
Mwenye Mungu, amlaze mahali pema peponi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba
yetu wa Taifa!</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29165" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Na,</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29167" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29179" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv7125574303MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_29177" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-11223263209820072232013-12-09T23:38:00.002-08:002013-12-09T23:38:43.827-08:00GRACE AIKAELI MBOWE<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28299" style="text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28298"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28297" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">MWANA MAMA
MAREHEMU GRACE AIKAELI MBOWE</span></strong></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28295" style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;"><br /></span></strong></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28292" style="background-color: transparent; color: black; font-family: HelveticaNeue, Helvetica Neue, Helvetica, Arial, Lucida Grande, sans-serif; font-size: 18.6667px; font-style: normal; font-weight: bold; text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28291"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28290" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Mungu ailaze
mahali pema peponi roho ya Marehemu Grace Aikaeli Mbowe! Pia Mungu awafute
machozi watoto wake, mme wake na ndugu na jamaa wote! Siandiki tanzia hii kwa
vile Grace, alikuwa dada wa rafiki yangu Mheshimiwa Freeman, wala siandiki
tanzia hii kwa vile marehemu alikuwa ni dada wa Mwenyekiti wa Chadema, na wala
siadiki tanzia hii kwa vile Grace, alizikwa na Askofu na viongozi wa Serikali
na vyama siasa.</span></strong></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28205" style="text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28204"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28203" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Na wala
siandiki tanzia kumsifia dada Grace, kuwa ni mtu mwema, mwenye huruma, mwenye
upendo, mvumilivu na mnyenyekevu, maana kila mtu akifikia hatua hiyo ya kulala
milele, hizo ndizo sifa zinazomsindikiza. Labda mchawi! Lakini katika hali ya
kawaida; unyenyekevu, upendo, uvumilivu na huruma, ni sifa za kila binadamu
anapoiacha dunia yetu na kujiunga na muumba wake.</span></strong></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28307" style="text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28306"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28305" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Na wala sina
lengo la kumpamba Grace kwa sifa nyingi, maana mimi ni nani? Mwenye uwezo wa
kumsifu ni Muumba wake aliye Mbinguni. Hata hivyo ni imani yangu kwamba sifa
zake zimeimbwa na wanasiasa ambao wameteka nyara wasifu wa marehemu na kuugeuza
kuwa mtaji wa siasa zao.</span></strong></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28311" style="text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28310"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28309" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Hata hivyo
siwezi kuukataa ukweli kwamba ninalia na wanaolia na kusikitika na
wanaosikitika. Msiba wa ndugu yako ni msiba wako pia, msiba wa rafiki yako ni
msiba wako pia. Pamoja na kwamba natafuta maneno ya kuwatuliza wafiwa na
kuonyesha kushiriki msiba huu, halikuwa lengo langu kubwa:</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Naandika
tanzia hii kuendeleza kusudio la kuanzisha safu hii ya Mwana Mama. Hii ni
nafasi ya kuandika Mwana mama ambaye ametoa mchango mkubwa katika taifa letu,
lakini hasikiki na wala hakuna kilichoandikwa juu yake. Na<span> </span>marehemu Grace, ni miongoni mwa akina mama
hao.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Ni bahati
mbaya kwamba dada yetu Grace, amesindikizwa na malumbano ya kisiasa! Vyombo
vyote vya habari, mitandao ya kijamii, imeamua kuweka pembeni mchango wake
katika taifa letu na kuelekekeza nguvu zote kwenye siasa. Ni jambo la
kusikitisha sana kwamba Tanzania tunapoteza mwelekeo na uandishi wetu umekuwa
ni <span> </span>wa kuongozwa na kuelekezwa na
wanasiasa.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Chadema na
CCM, ni vyama vya siasa ambavyo vimetekea nyara wasifu wa dada yetu Grace.
Badala ya kutuelezea mchango wake katika maisha yake ya miaka hamsini kasoro,
tunaletewa siasa na mambo mengi ya kuzusha kwa faida ya siasa na wanasiasa.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Grace
alifariki katika ajali ya gari <span> </span>katika
eneo la Kabuku, Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga wakati akielekea jijini Dar es
Salaam. Watu wengine walipoteza uhai katika ajali hiyo. Hivyo<span> </span>ni kifo kama vifo vingine.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Bahati mbaya
hadi sasa hivi hakuna anayetwambia kwamba dada yetu Grace</span></strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt;"> <strong><span style="font-weight: normal;">alikuwa mwanamke wa pili
kusajiliwa na bodi ya wahandisi nchini akiwa kama Ofisa mpimaji (Quantity
Surveyer) baada ya kuhitimu elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kitengo
ardhi (ARU).</span></strong></span></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Hii ni sifa
kubwa kwa marehemu. Ni wazi kwa ujuzi huo na kisomo chake ametoa mchango mkubwa
katika taifa letu. Hapana shaka kwamba kwa kifo chake, pengo kubwa limetokea
katika fani yake ya uhandisi. Haya ndiyo tunataka tuyasikie, na haya ndiyo
yanatusukuma kuandika tanzia hii, ili kumlilia huyu dada yetu ambaye kifo
kimemchukua mapema.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Kuiacha sifa
hii kubwa na kuendeleza nyimbo za siasa, ni kumkosea haki marehemu. Kila
binadamu ana uhuru wa kufanya mambo yake binafsi. Suala la mapenzi ya siasa ni
suala la mtu binafsi, lakini huduma kwa jamii, kama hii ya(Quantity Surveyer)
ambayo dada yetu alikuwa amesomea, si suala binafsi. Hili ni suala la kijamii
na ni suala la kitaifa. Kwa kujenga sifa ya mtu ndani ya jamii, masuala ya
kijamii yanashika nafasi ya kwanza mbele ya masuala ya binafsi. Hata kama
Grace, alihama chama cha Chadema, chama ambacho kaka yake ni Mwenyekiti, hili
ni suala binafsi ambalo si muhimu sana ukilinganisha na mchango wa dada Grace
katika jamii kubwa ya watanzania.</span></strong></div>
<div style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal;">Kama Grace,
alifika chuo kikuu na kusoma masomo hayo ya sayansi, ni wazi huko nyuma
alifanya vizuri. Tunataka tusikie wasifu wake katika shule za sekondari.
Tungependa kusikia na kufahamu alikuwa ni mtoto wa namna gani wakati akisoma.
Huo ndio wasifu wa Grace na wala si huu wa Chadema na CCM.</span></strong></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" style="text-align: justify;">
<strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal; line-height: 115%;">Nina imani kuna mambo mengine mengi aliyoyatenda </span></strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">dada Grace, zaidi ya haya ya Chadema na CCM. Hivyo
ninategemea, baada ya wasifu huu wa uchokozi, wengine watajitokeza na kutuimbia
wasifu chanya wa dada yetu.<strong><span style="font-weight: normal;"></span></strong></span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28315" style="text-align: justify;">
<strong id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28314"><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28313" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; font-weight: normal; line-height: 115%;">Mpaka mazishi yake yakaongozwa na Askofu, ina maana
huyu alikuwa mtu wa sala, alikuwa mtu wa kanisa. Tusikie wasifu wake wa
kumpenda Mungu wake na watu wake. Huu ndiyo wasifu <span> </span>wa </span></strong><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">dada yetu Grace na wala si huu wasifu wa CCM na Chadema.</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28318" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28317" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Dada Grace alikuwa na watoto. Huyu alikuwa mama wa namna gani? Tunataka
kusikia watoto wake wakiimba wasifu wake. Lakini vyombo vya habari na mitandao ya
kijamii, imewanyamazisha watoto wa marehemu na kuteka nyara wasifu wa mama yao
mpenzi.</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28321" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28320" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Grace, ni mtu aliyesimama kama mtu, kama mama wa familia. Kuunganisha
wasifu wake na wa ndugu zake, ni kumkosea haki kama binadamu. Hata hivyo kama
nilivyodokeza hapo juu, huyu ni mama mhandisi, kuna mengi ya kuandika juu yake
na kumbukuka zaidi ya kumeza wasifu wake makusudi mazima.</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28324" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28323" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pia, watanzania tujifunze kuandika na kuheshimu wasifu wa watu. Tusichanganye
wasifu na vitu vingine ambavyo vinakuja na kupita. Daima wasifu wa mtu ni vitu
vile visivyopita! Ni <span> </span>mchango wa marehemu
katika jamii husika; na mara nyingi tunafikiria mchango chanya!</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28348" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28347" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mungu amlaze mahali pema dada yetu mpendwa Grace Aikaeli Mbowe.</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28345" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28343" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28342" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv2330781652MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_28340" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-40147197898942444202013-12-09T23:37:00.000-08:002013-12-09T23:37:02.265-08:00TEITI 1<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27637" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27639" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">MPANGO WA TEITI UTALETA UWAZI KWENYE MADINI, MAFUTA </span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27625" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"></span><span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27624" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">NA GESI ASILIA AU NI
MSAMIATI KAMA MINGINE?</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27622" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27464" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27463" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tanzania ni mabingwa wa misamiati na kauli mbiu, kama kigezo cha maendeleo
kingekuwa ni hesabu ya misamiati na kauli mbiu, basi tungekuwa mstari wa mbele
katika maendeleo. “Kilimo kwanza”, sasa imemezwa na “Big results now”. MKUKUTA,
MKURABITA, Kasi Mpya, na maisha bora kwa kila Mtanzania ni nyimbo za kumbukizi!</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27642" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27641" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Yawezekana mpango wa TEITI, utajiunga kwenye mlolongo huu wa nyimbo za
kusadikika au ndo tunapiga hatua na kuanza utamaduni mpya? Utamaduni wa uwazi
katika mipango ya matumizi ya rasilimali na kuhakikisha utajiri huu wa
rasilimali unawanufaisha watanzania wote? Wakati watanzania wanalilia usiri
kwenye mikataba ya madini na kilio cha Gesi asilia kule Mtwara, Tanzania
imejiunga na Mpango wa Uhamasishaji Uwazi katika Mapato ya Madini, Gesi asilia
na Mafuta (EITI) (Extractive Industries Transparency Initiative). Hivyo kwa
Tanzania, mpango huu unajulikana kama TEITI( Tanzania Extractive Industries
Transparency Initiative).</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27646" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27645" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mpango wa Uhamasishaji wa uwazi na Uwajibikaji Katika Tasnia ya Uziduaji
(Asasi ya EITI) ulitangazwa mara ya kwanza kwenye Mkutano wa Dunia juu ya
Maendeleo Endelevu uliofanyika Johannesburg, Afrika ya Kusini mnamo Mwaka 2002
na kuzinduliwa rasmi London Uingereza 2003. Nchi wanachama wa asasi hii ya
kimataifa ya EITI hutakiwa kuweka wazi malipo ya kodi kutoka kampuni za
uchimbaji wa madini, gesi asilia na mafuta; na mapato yanayopokelewa
Serikalini. Kupitia taarifa hizi za malipo ya kodi<span> </span>na mapato wananchi hushirikishwa katika
usimamizi wa rasilimali hizi kwa kujadili na kutoa michango yao ili kuboresha
sera na sheria kwa ajili ya kuongeza mapato.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27649" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27648" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Asasi hii ya EITI ilianzishwa kwa kutambua kwamba madini, mafuta na Gesi
asilia vinaweza kuinua kipato na kuleta maendeleo duniani, lakini sehemu ambazo
serikali ni dhaifu utajiri huu unaweza kuleta rushwa, ufisadi machafuko na
kuleta ufukara kwa watu wengi. Hivyo kuwa na mpango wa uhamasishaji uwazi na
uwajibikaji katika tasnia hii ya uziduaji wa madini, mafuta na gesi asilia ni
muhimu sana.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27652" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27651" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mnamo tarehe 18 Novemba, 2008, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ilitoa tamko kwa umma juu ya nia yake ya kujiunga na asasi ya EITI ili kuongeza
uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa sekta za madini, gesi asilia na
mafuta. Katika mkutano wa nne wa EITI wa dunia uliofanyika tarehe 16 Februari,
2009 Doha, Qatar, Bodi ya EITI iliipatia Tanzania uanachama wa awali baada ya kukamilisha
taratibu za kujiandikisha.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27655" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27654" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Utekelezaji wa EITI hapa nchini unasimamiwa na Kamati Tekelezi ambayo
imeundwa na wajumbe 16 kutoka asasi za kiraia, kampuni na Serikali. Wajumbe
watano kwa kila kikundi. Kamati hiyo huongozwa na mwenyekiti ambaye hatoki
katika kundi lolote. Katika utendaji wa shughuli za kila siku, Kamati
inasaidiwa na Sekretarieti.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27658" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27657" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kama mpango huu utatekelezwa vizuri na kukwepa nyimbo za kusadikika,
misamiati na Kauli mbiu nyingine nyingi tulizozizoea, utatusaidia kupiga hatua
kubwa katika kusimamia utajiri wetu rasilimali zetu . Kulingana na kigezo cha
IMF, nchi ambazo mchango wa sekta za madini, mafuta na gesi asilia katika pato
la mwaka au mauzo ya nje hufikia asilimia 25, hutambulika kuwa ni nchi zenye
utajiri wa mali asili. Hapa Tanzania mchango wa sekta ya madini pekee katika
mauzo ya nje ni zaidi ya asilimia 25 ya mapato ya fedha za kigeni. Takwimu za
miaka mitatu iliyopita zinaonesha mapato ya fedha za kigeni kutoka sekta ya
madini ni asilimia 38.2 kwa mwaka 2007,<span>
</span>asilimia 34 kwa mwaka 2008 na asilimia 35 kwa mwaka 2009. Hivyo na sisi
ni miongoni mwa nchi zenye utajiri wa mali asili;</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27661" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27660" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hivyo basi mpango huu wa TEITI unahitajika ili kuhamasisha uwazi na
uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia kwa
kuweka wazi malipo ya kodi kutoka kwenye makampuni ya uziduaji na mapato
yaliyopokelewa serikalini. Kuongeza ufahamu kwa umma kwa kuchapisha malipo na
mapato yatokanayo na madini, mafuta na gesi asilia, hivyo kuongeza ushiriki wao
katika usimamizi wa sekta za madini, mafuta na gesi asilia.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27664" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27663" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mpango huu pia utaisaidia serikali na wadau kupata taarifa sahihi na kwa
wakati za malipo na mapato yanayotokana na shughuli za uchimbaji wa madini,
mafuta na gesi asilia. Uwazi katika taarifa za malipo na mapato ni msingi mzuri
wa kuboresha usimamizi na utawala bora katika tasnia ya uziduaji.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Sasa hivi, watanzania wanalalamika kwamba makampuni ya madini, mafuta na
gesi asilia wanawaibia. Mtwara, kila mwananchi anasema “gesi” haitoki!
Wanalalamika kwamba utajiri wao utaibiwa na kupelekwa sehemu nyingine. Lakini hakuna
anayeweza kusema kwa uhakika ni kiasi gani cha fedha tunaibiwa. Mpango huu wa
TEITI, unawataka makampuni na serikali kuweka malipo wazi; Makampuni yaonyeshe
yamelipa kodi kiasi gani na serikali ionyeshe imepokea kiasi gani. Kwa kufanya
ulinganifu wa mapato na kodi, tunaweza kupata msingi mzuri wa kujenga hoja ya
kuibiwa na wawekezaji au kuibiwa na serikali. Tunaweza kuwa na msingi wa kuiwajibisha
serikali na kuuliza maswali yenye kuhitaji majibu ya uhakika.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hadi leo hii ninapoandika makala hii, TEITI, imetoa taarifa tatu za malipo
ya kodi, mrabaha na tozo kutoka kampuni za uchimbaji madini na gesi asilia.
Katika makala hii nitajadili taarifa ya pili ya mwaka wa fedha 2009/10</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na mambo mengine mengi, taarifa ya ulinganisho ya TEITI, inaonyesha
kwa mwaka wa fedha wa 2009/10 kampuni zililipa kiasi cha shilingi 424 bilioni ikilinganishwa
na mapato ya shilingi 419 bilioni yaliyopokelewa serikalini. Matokeo hayo
yanaonyesha tofauti ya malipo na mapato kwa kiasi cha shilingi bilioni 5. Hii
ni sawa na asilimia 1 ya jumla ya mapato yaliyopokekewa na serikali katika
kipindi hicho.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">La kuzingatia hapa ni kwamba makampuni yaliyofanyiwa ulinganifu, ni yale
yenye uwezo wa kulipa kodi zaidi ya shilingi milioni 200, kwa mwaka wa fedha wa
serikali, makampuni 23, kati ya makampuni zaidi ya 400, ndo yalitimiza kigezo
hicho.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa taarifa hizi za TEITI, tunaweza kufahamu ni makampuni gani yanalipa
kodi na yanalipa kiasi gani. Tunaweza kufahamu serikali inapata kiasi gani.
Mfano taarifa ya pili ya TEITI, inaonyesha makampuni yalilipa kiasi kikubwa,
lakini serikali inaoyesha imepokea pungufu. Nani anasema uongo? Serikali au
makampuni? Tunaweza kujadili kwa uhakika, bila kulalamika tunaibiwa, wakati
hatuna takwimu.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na changamoto nyingine ambazo TEITI, inakumbana nazo ni kwamba kwa
sasa Tanzania haina sheria ya TEITI. Ni vigumu kuwafanya wadau washiriki katika
zoezi la ulinganisho kwa hiari bila kuhimizwa. Kwa Ulinganisho wa taarifa ya
pili kwa mfano,<span> </span>baadhi ya kampuni
hazikuweza kuwasilisha fomu za takwimu walipoombwa kufanya hivyo, na wengine
walioweza kuwasilisha fomu za takwimu walishindwa kukidhi masharti yote. Bila
kuwepo sheria inakuwa vigumu kuwahimiza.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27673" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27675" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Changamoto nyingine kubwa ni mpango huu kufahamika kwa wananchi. Hadi leo
hii ni watanzania wangapi wanafahamu kwamba kuna mpango wa TEITI? Ni watanzania
wangapi wamesikia au kuona taarifa za TEITI juu ya ulinganisho wa kodi na
mapato kutoka kampuni za uchimbaji madini, mafuta na gesi asilia? Kulingana na
umuhimu wa TEITI ni muhimu, wananchi kushiriki kwa kiasi kikubwa. Kamati
tekelezi ambayo ina wajumbe 5 kutoka kwenye asasi za kirai, ni muhimu kuundwa
kwa kufuata ushirikishwaji. Wachaguliwe kidemokrasia na si kuingia kwenye
kamati kwa vile mtu ana asasi. Mara nyingi Asasi za kiraia zinaanzishwa na
baadhi ya watu, bila kuwa na ushirikishwaji mkubwa kwenye jamii. Si mara zote
Asasi kuwakilisha matakwa ya jamii nzima. Suala la utajiri wa madini, mafuta na
gesi asilia ni la jamii nzima, hivyo linahitaji uwakilishi mpana. Ni muhimu
kwenye kamati hii <span> </span>waingie watu
wanaoguswa na maendeleo ya taifa letu. Bila kuwa na Kamati tekelezi yenye upeo
na msimamo imara, mpango wa TEITI, utakuwa ni miongoni mwa nyimbo za kusadikika
tulizozizoea.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27671" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27669" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 6331 22.</span></div>
<div class="yiv3660234737MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_27667" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">pkarugendo@yahoo.com</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-86295761069888690052013-12-09T23:35:00.001-08:002013-12-09T23:35:17.634-08:00AGPAHI - GEITA<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26874" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26873" lang="SW" style="font-size: 12.0pt; line-height: 115%;">KIKUNDI CHA KINAMAMA TUSHIKAMANE MASUMBWE – GEITA.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26871" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 12.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26869" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26868" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kama kawaida ya safu hii, ni kukuletea habari za Mwana mama. Tunajitahidi
kukuletea habari za akina mama ambao wako penzoni na habari zao hazisikiki wala
kuandikwa. Na kawaida tumekuwa tukiwaletea habari za mama mmoja mmoja na tutatendelea
kufanya hivyo.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26759" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26758" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Leo imejitokeza tofauti kidogo tu, na tunakuletea Kikundi cha Kinamama
Tushikamane kutoka Wilaya mpya ya Mbogwe mkoa wa Geita. Kikundi hiki
kilianzishwa na wanawake wanaoishi na virusi vya UKIMWI, kwa lengo la
kuelimisha jamii kuhusu maambukizi yaVVU na UKIMWI, kuelimisha jamii juu ya
unyanyapaa na kunyanyapaliwa, kuikumbusha jamii kwamba mtu mwenye virusi vya
ukimwi ana haki ya kuoa na kuolewa na kupata mtoto asiye na maambukizi,
kuelimisha jamii juu ya kuzuia maambukizi mapya wa VVU na la msingi kwao ni
kuelimisha juu ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na
kuhamasisha watu kupima afya zao; maana bila kupima ni vigumu kujua mgonjwa na
mzima na vigumu kuwaanzishia dawa wangojwa na hasa kuzuia maambukizi kutoka kwa
mama kwenda kwa mtoto.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26888" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26887" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Tumeamua tuandike juu ya wanawake hawa kwa pamoja, maana wote wanafanya
kitu kinachofanana. Wote hawa wana sifa ya Mwana Mama, ambaye tunamwandika
kwenye safu hii. Pamoja na mambo mazuri ya kutetea na kuulinda uhai,
wanayoyafanya wanawake hawa, wana sifa moja kubwa ya kushinda vita kubwa ya kujinyanyapaa
wao wenyewe. Hatua hii ni kubwa na ni muhimu sana katika zoezi zima la
kupambana na UKIMWI. Mtu akijinyanyapaa mwenyewe, anapoteza maisha haraka sana.
Mtu akijinyanyapaa mwenyewe, anaufanya ugonjwa huu kuwa wa siri na matokeo yake
hawezi kupata msaada kwa wakati. Wanawake hawa wa Masumbwe, wameshinda mtihani
huu na kuna haja ya kuwapongeza na kuwatolea mfano, ili watu wengine wajifunze
na kuiga mfano wa wanawake hawa wa Masumbwe.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26891" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26890" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Septemba 26 2013, wakati wa kufungua Jengo la Kliniki ya huduma na matunzo
kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi, kituo cha afya cha Masumbwe, wilaya ya
Mbogwe, wanawake hawa walisimama mbele ya umati mkubwa uliokuwa umekusanyika
siku hiyo na kutangaza mafanikio yao; kwamba miongoni mwao zaidi ya
wanawake<span> </span>6, ambao wana virusi
wamefanikiwa kujifungua watoto wasiokuwa na virusi; kwamba wanafuata masharti
ya kumeza dawa za kupunguza makali ya virusi; kwamba wanachangiana fedha za
kusaidiana katika kikundi chao.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26895" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26894" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Wanawake hawa, walisimama na kujitangaza, bila aibu yoyote ile, kwamba wao
walipimwa na kukutwa na virusi, na walifuatilia dawa bila kuchoka na matokeo
yake wameweza kujifungua watoto wasiokuwa na virusi na wenyewe wanaendelea
vizuri na wanaweza kushiriki shughuli zote za kuzalisha mali. Watoto hao
waliozaliwa bila virusi walionyeshwa pia kwenye mkutano huo. <span> </span>Wanawake hawa waliendelea kuwahimiza watu
wengine kujitokeza kupima, ili watakao kutwa na virusi, wapate dawa za
kurefusha maisha na kumkinga mtoto asipate maambukizi.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26899" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26898" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwenye picha hapo chini, wanaonekana wanawake hao wa Masumbwe, wakisoma
risala yao mbele ya mgeni rasmi. Ni moyo wa ushujaa na kujikubali katika jamii
ambayo bado ina unyanyapaa, maana wakati wanawake hao wakisoma risala yao, kuna
maneno yaliyokuwa yakipita miongoni mwa wasikilizaji kwamba hao ni “Wauaji”.
Wanajijua kwamba wao ni wagonjwa, lakini wanaendelea kusambaza. Kuna sauti za
chini chini zilizokuwa zikisikika kwamba “ Hawa ni watu wa kuawa, ili
wasiendelee kusambaza ugonjwa”. Kila mtu alikuwa na la kwake kusema, lakini
sauti ya pamoja, ikiungwa mkono<span> </span>na mgeni
rasmi, shirika la AGPAHI, waandishi wa habari, wageni waalikwa na watu wengine
wenye mapenzi mema, ilikuwa ikiiunga mkono juhudi za wanawake hawa wa Masumbwe.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26902" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26901" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Watu wote wanaopambana na UKIMWI, wamekuwa wakihimiza watu kujitolea kupima
afya zao, ili watakaokutwa na virusi, waanzishiwe dawa za kupunguza makali,
lakini jambo ambalo limesisitizwa kwa nguvu zote ni kukinga maambukizi kutoka
kwa mama kwenda kwa mtoto. Shirika<span> </span>la
AGPAHI ambalo kwa msaada wa watu wa Amerika, limeweza kujenga jengo la Kliniki
ya huduma na matunzo kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI kituo cha
Masumbwe, wamekuwa mstari wa mbele kuhimiza kuzuia virusi kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto.Tunaweza kusema kwamba huo ndiyo utume wa AGPAHI, kupunguza au
kufuta kabisa uwezekano wa virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26905" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26904" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hivyo mafanikio ya akinamama wa Masumbwe ni mafanikio ya AGPHAHI pia. Ni
mafanikio wa watu wa Amerika wanaotoa fedha zao ili zisaidie katika zoezi hili
la kupunguza makali ya virusi vya UKIWMI na kuzuia virusi kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto. Na pia ni mafanikio yetu sote maana tunaimba wimbo wa
Tanzania<span> </span>bila UKIMWI inawezekana;
iwezekane kwa vitendo na kupiga hatua!</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26909" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26908" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na mafanikio haya, bado kuna changamoto katika zoezi zima. Akinamama
hawa wa Masumbwe, pamoja na kufurahia kujifungua watoto wasiokuwa na virusi,
bado walielezea changamoto zinazowakabili katika jamii; Changamoto kubwa ni ya
unyanyapaa, ingawa wao wanajitahidi sana kutojinyanyapaa, bado huko mtaani wananyoshewa
kidole kwamba wanazaa watoto wakati wao ni wagonjwa, wengine wanawalaumu
kuendelea kufanya tendo la ngono wakati wakijua kwamba wao ni wagonjwa; hivyo
kuna ambao wanawapachika majina ya “Wauaji”; na kwamba watoto wao wanapocheza
na watoto wengine, wanabaguliwa na kunyoshewa kidole kwamba wao ni waathirika
wa UKIMWI na kwamba uchumi ni kikwazo kikubwa, maana wakati mwingine hawapati
matunzo kulingana na afya za zilivyo.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26912" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26911" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ili kupambana na tatizo la ukata, wanawake hao wameamua kufungua akaunti
benki na kujiwekea sheria ya kuchanga shilingi 500, kila mwezi. Wakati wa
kufungua kituo chao hapo Masumbwe, walikuwa na shilingi 30,000 kwenye akaunti
yao. Kwa kuguswa na moyo wa wanawake hao, Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe
akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Geita, walianzisha harambee ya kuchangia mfuko
huo wa akina mama wa tushikamane na kuweza kuutunisha.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26916" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26915" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Vyo vyote vile hawa ni wanawake wenye sifa zote<span> </span>za kuandikwa kwenye safu hii ya Mwana Mama.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26919" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26921" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv9761209408MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26923" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-1118698703675401122013-12-09T23:32:00.004-08:002013-12-09T23:32:47.345-08:00TEITI<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26139" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26138" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">MPANGO WA UHAMASISHAJI UWAZI KATIKA MAPATO YA MADINI,GESI ASILIA NA MAFUTA
UENDE MBALI<span> </span>ZAIDI!</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26136" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_25993" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_25992" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Makala iliyopita katika safu hii, tuliwaelezea mpango wa TEITI hapa
Tanzania na faida zake. Maswali<span>
</span>yanayokuja kutoka kwa baadhi ya wasomaji wa gazeti hili, yanaonyesha
wazi kwamba mpango huu bado haujafahamika vizuri na wengi wanaonyesha
hawakufahamu kabisa kwamba kuna mpango kama huu napa kwetu Tanzania. Ni wazi
TEITI wana kazi ya ziada ya kuhakikisha taarifa zao zinasambazwa na
kufafanuliwa kwa wananchi. <span> </span>Ni jambo la
kujipongeza kwamba sasa kupitia mpango huu, kwa yeyote anayejali na kufuatilia
masuala ya mapato katika<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26144"> </span>taifa letu,
anaweza kupata takwimu za uhakika juu ya mapato yanayotokana na madini, mafuta
na gesi asilia.</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26147" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26146" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ni wazi si kazi ya TEITI<span> </span>kufuatilia
fedha hizi zinazolipwa na makampuni ya uziduaji wa madini, mafuta na gesi
asilia zinatumika vipi? Zinanunua mashangingi na kulipia safari za viongozi nje
ya nchi? Zinatumika kulipia matibabu ya viongozi na vigogo wengine nje ya nchi?
Zinatumika kulipa posho za wabunge na viongozi wengine serikalini au zinatumika
kwa lengo la “Maisha bora kwa kila Mtanzania” na “Big results now”? Hii ni kazi
ya wabunge wetu, kufuatilia na kupiga kelele juu ya matumizi ya fedha hizi.
Hata na wananchi wenyewe baada ya kusoma na kuelewa taarifa hizi za<span> </span>TEITI wanaweza kuhoji na kuwashinikiza
wawakilishi wao, madiwani na wabunge kufuatilia kwa karibu matumizi ya mapato
haya yanayotokana na madini, mafuta na gesi asilia. <span> </span>Fedha hizi zitakuwa ninaingizwa kwenye mfuko
wa maendeleo kwa malengo ya kujenga barabara, kununua dawa, kulipia elimu ya
juu ya vijana wetu na kazi nyingine nyingi za kijamii. Je fedha hizi zinafika
kweli na kufanya kazi hizi? Pamoja na ukweli kwamba makampuni haya ya uziduaji yanatuibia
bado kuna ulazima wa kuhakikisha ukweli huu<span>
</span>na kuuelezea bila kuacha utata wa aina yoyote nyuma yake.</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ingawa bado kuna utata kwenye takwimu hizi ambazo TEITI wanatoa;<span> </span>makampuni yakionyesha kulipa zaidi, na
serikali ikionyesha kupokea pungufu, ni<span>
</span>masuala ambayo kwa ufuatiliaji wa karibu yanaweza kupata maelezo. Pia
utata mwingine, kwamba asilimia 99 ya mapato yote yatokanayo na madini, mafuta
na gesi asilia yanalipwa na makampuni 23, ni jambo ambalo bado linahitaji
maelezo ya kina. Ni kitu gani kinatokea kwa makampuni mengine zaidi ya 400
yaliyosajiliwa <span> </span>na yanafanya kazi ? Ni
kwamba hayapati faidia kabisa kiasi cha kushindwa kulipa kodi, au hayazalishi chochote?
Na kama hayazalishi chochote ni kwa nini yaendelee kuwepo?</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Pamoja na mwanga unaotolewa na mpango huu wa TEITI ,bado kuna hoja kwamba
mpango huu ungeweza kwenda mbali zaidi. Hoja yenyewe ni kwamba, kwa nini
usifanywe ulinganifu wa <span> </span>faida wanayoipata
makampuni na kodi<span> </span>wanazozilipa? Madini,
mafuta na gesi asilia vinauzwa kwenye soko la dunia. Hivyo si kazi ngumu
kufahamu makampuni haya yanapata faida kiasi gani. Mfano ukiangalia bei ya
dhahabu kwenye soko la dunia, na ukaangalia kiasi cha dhahabu ambacho makampuni
haya yanaripoti kuchimba na kuuza nje ya nchi utapata takwimu kubwa ambayo bila
maelezo ya kina ni kana kwamba taifa letu linayapatia makampuni haya zawadi! Ukifanya
ulinganifu wa faida wanayoipata, baada ya kuondoa fedha za uendeshaji, ni kweli
inawiana na kile wanachokilipa?</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mfano sasa hivi ulinganifu uliofanyika kwenye taarifa tatu za TEITI,
unaonyesha wazi kabisa kiasi ambacho makampuni yanalipa. Na hii imewezekana kwa
makampuni na serikali kuonyesha risiti za malipo na vielelezo vingine. Hivyo
mawazo yaliyokuwepo kwamba makampuni haya hayalipi kabisa sasa haipo.
Kinachotakiwa sasa ni makampuni kuonyesha risiti za mauzo, risiti za uendeshaji
ili kubaini faida wanayoipata mwishoni ili kufanya ulinganifu wa kodi
zinazotolewa na faida inayopatikana. Ulinganifu huu ndio wenye tija kwa taifa
letu. Yawezekana pamoja na makampuni haya kulipa kodi, wanapata faida kubwa na
kutuachia mashimo na uharibifu wa mazingira.</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26150" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26149" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mpango huu wa kuhamasisha uwazi una uwajibikaji, unaweza kwenda mbali kiasi
cha kuwezesha mikataba ya<span> </span>uchimbaji
madini na uzinduaji wa mafuta na gesi asilia kuwekwa wazi? Maana swali la
kujiuliza ni lini makampuni haya yanapoanza kulipa kodi hizi serikalini? Kuna
taarifa kwamba kuna Resolute kule Nzega, ambao umekuwa ukichimba dhahabu kwa
kipindi cha miaka 16, <span> </span>ulianza kulipa
kodi miaka miwili ya mwisho. Pia kuna taarifa za kuaminika kwamba kuna migodi
ya kuchimba dhahabu ambayo itafikia mwisho wa kuchimba dhahabu bila kulipa
kodi, kwa kisingizio kwamba kwa miaka yote hiyo wamekuwa wakifanya hasara? Inashangaza
kuona kampuni inapata hasara na inaendelea kuwepo na kuchimba madini zaidi ya
miaka 16?</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26164" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26166" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kama hili ni kweli, kwa nini basi mango huu wa TEITI, usifanye utafiti ili
kubaini ukweli huu? Maana kama mtu anapata hasara kila mwaka, kwa nini aendelee
kuchimba au kutafuta<span> </span>mafuta na gesi
asilia kwa kipindi<span> </span>cha miaka<span> </span>kumi? Haya ni maswali ambayo watu wanajiuliza
kama ambavyo huko nyuma walikuwa wakilalamika kwamba tunaachiwa mashimo, wakati
makampuni yanalipa kodi. Ukweli huu umewekwa wazi na mpango wa TEITI. Hata kama
taarifa hii ya TEITI haijasambazwa kiasi cha kutosha, ukweli umejulikana na
hasa kwa wale walio kwenye ngazi ya kutoa maamuzi. <span> </span>Ndio maana ni muhimu pia kwa TEITI kutuweka
wazi juu ya hoja hii ya watu kuendelea kuchimba na kuendeleza shughuli za
uziduaji wakati wanafanyia hasara. Tunaposema TEITI waende mbele zaidi ya hapa
walipo tuna maana ya kufanya ulinganifu wa faida ya makampuni na kodi
wanazozilipa. Na pia kuhakikisha taarifa zao zinasambazwa kwa njia mbali mbali;
kwa radio, luninga, magazeti, semina na hata mashuleni.</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26160" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26162" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Uelewa mpana, uwazi na uwajibikaji katika miradi ya madini, mafuta na gesi <span> </span>asilia utaliepushia taifa letu na balaa
itokanayo na miradi hii kama tunavyosikia kwenye nchi nyingine za Afrika.
Vurugu za gesi kule Mtwara ni dalili za balaa kubwa linaloweza kulikumba taifa
letu. Dawa pekee ni uwazi na uwajibikaji; hivyo mpango huu wa TEITI uwezeshwe
ili uweze kwenda mbali zaidi.</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na </span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26158" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus<span> </span>Karugendo</span></div>
<div class="yiv3993991148MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_26156" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-68342085498997463062013-12-09T23:27:00.001-08:002013-12-09T23:27:19.420-08:00UKATILI WA KIJINSIA TANZANIA<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:WordDocument>
<w:View>Normal</w:View>
<w:Zoom>0</w:Zoom>
<w:TrackMoves/>
<w:TrackFormatting/>
<w:PunctuationKerning/>
<w:ValidateAgainstSchemas/>
<w:SaveIfXMLInvalid>false</w:SaveIfXMLInvalid>
<w:IgnoreMixedContent>false</w:IgnoreMixedContent>
<w:AlwaysShowPlaceholderText>false</w:AlwaysShowPlaceholderText>
<w:DoNotPromoteQF/>
<w:LidThemeOther>EN-US</w:LidThemeOther>
<w:LidThemeAsian>X-NONE</w:LidThemeAsian>
<w:LidThemeComplexScript>X-NONE</w:LidThemeComplexScript>
<w:Compatibility>
<w:BreakWrappedTables/>
<w:SnapToGridInCell/>
<w:WrapTextWithPunct/>
<w:UseAsianBreakRules/>
<w:DontGrowAutofit/>
<w:SplitPgBreakAndParaMark/>
<w:DontVertAlignCellWithSp/>
<w:DontBreakConstrainedForcedTables/>
<w:DontVertAlignInTxbx/>
<w:Word11KerningPairs/>
<w:CachedColBalance/>
</w:Compatibility>
<m:mathPr>
<m:mathFont m:val="Cambria Math"/>
<m:brkBin m:val="before"/>
<m:brkBinSub m:val="--"/>
<m:smallFrac m:val="off"/>
<m:dispDef/>
<m:lMargin m:val="0"/>
<m:rMargin m:val="0"/>
<m:defJc m:val="centerGroup"/>
<m:wrapIndent m:val="1440"/>
<m:intLim m:val="subSup"/>
<m:naryLim m:val="undOvr"/>
</m:mathPr></w:WordDocument>
</xml><![endif]--><br />
<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:LatentStyles DefLockedState="false" DefUnhideWhenUsed="true"
DefSemiHidden="true" DefQFormat="false" DefPriority="99"
LatentStyleCount="267">
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Normal"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="heading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="35" QFormat="true" Name="caption"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="10" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" Name="Default Paragraph Font"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="11" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtitle"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="22" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Strong"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="20" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="59" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Table Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Placeholder Text"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="No Spacing"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Revision"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="34" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="List Paragraph"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="29" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="30" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="19" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="21" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="31" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="32" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="33" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Book Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="37" Name="Bibliography"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" QFormat="true" Name="TOC Heading"/>
</w:LatentStyles>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 10]>
<style>
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:"Table Normal";
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:"";
mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;
mso-para-margin-top:0in;
mso-para-margin-right:0in;
mso-para-margin-bottom:10.0pt;
mso-para-margin-left:0in;
line-height:115%;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:11.0pt;
font-family:"Calibri","sans-serif";
mso-ascii-font-family:Calibri;
mso-ascii-theme-font:minor-latin;
mso-fareast-font-family:"Times New Roman";
mso-fareast-theme-font:minor-fareast;
mso-hansi-font-family:Calibri;
mso-hansi-theme-font:minor-latin;
mso-bidi-font-family:"Times New Roman";
mso-bidi-theme-font:minor-bidi;}
</style>
<![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapedefaults v:ext="edit" spidmax="1026"/>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapelayout v:ext="edit">
<o:idmap v:ext="edit" data="1"/>
</o:shapelayout></xml><![endif]-->
<br />
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">UKATILI<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>WA
KJINSIA BADO NI KITENDAWILI TANZANIA</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Tarehe 25.11.2013, tunaanza siku 16 za kupinga
ukatili wa kijinsia. Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ni kampeni ya
kimataifa iliyoanzia kwenye mkutano wa kwanza wa Taasisi ya Uongozi wa Wanawake
Duniani (Women’s Global Leadership Institute)<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>uliofadhiliwa na Kituo Cha Uongozi wa Wanawake Duniani (Center for
Women’s Global Leadership ) mwaka 1991. (. Washiriki walichagua tarehe 25 mwezi
Novemba, Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili Dhidi ya Wanawake, na Desemba 10,
Siku ya Haki za Binadamu Duniani, ili kuhusianisha ukatili dhidi ya wanawake na
haki za binadamu na kuhamasisha kuwa ukatili kama huu ni ukiukaji wa haki za
binadamu. Kipindi hiki cha siku 16 pia kinaangalia siku nyingine muhimu,
ikiwemo tarehe 29 Novemba, ambayo ni Siku ya Watetezi wa Haki za Binadamu,
Desemba 1 Siku ya Ukimwi Duniani na Desemba 6, Kumbukumbu ya Mauaji ya Montreal.<span style="mso-spacerun: yes;"> </span><br style="mso-special-character: line-break;" />
<br style="mso-special-character: line-break;" />
</span><span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;"></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Ukatili Dhidi ya Wanawake ni ukiukwaji<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>ulionea wa haki za binadamu , ni janga la
kibinadamu katika jamii, na kikwazo cha kufikia usawa, maendeleo, usalama na
amani. Maneno “ukatili dhidi ya wanawake” na “ukatili wa kijinsia” yanatumika
kumaanisha mlolongo wa unyanyasaji unaofanyika dhidi ya wanawake<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>unaotokana na kutokuwepo na usawa wa kijinsia
na hadhi ya chini wa wanawake katika jamii ukilinganisha na wanaume. Mwaka
1993, Azimio la Umoja wa Mataifa juu ya Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake uliutafsiri
ukatili dhidi ya wanawake kama:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>“kitendo
chochote cha ukatili wa kijinsia kinachosababisha au kinachoweza kusababisha
maumivu au mateso ya kimwili, kingono au kiakili kwa wanawake, ikiwamo vitisho,
kulazimishwa au kunyimwa uhuru, vinavyotokea katika jamii au kwenye maisha
binafsi .” <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Inakadiriwa kuwa mmoja kati
ya wanawake watatu duniani atakumbana na ina Fulani za ukatili wa kijinsia
katika maisha yake. Hivyo ni wazi kabisa kwamba wanaofanyiwa ukatili wa
kijinsia ni wanawake, ingawa si lazima kwamba ukatili huu unafanywa na wanaume
peke yao.</span><span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;"></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Lengo la siku hizi 16 ni kupinga ukatili wa kijinsia,
lakini kwa wengi siku hizi zimechukuliwa kama kupinga ukatili dhidi ya
wanawake. Na kwa mtizamo finyu ni ukatili unaofanywa na wanaume kwa wanawake.
Lakini hali halisi na matukio ya siku kwa siku na hasa hapa Tanzania
yanaonyesha tofauti kabisa, kiasi cha kulifanya suala zima la ukatili wa kijinsia
kuwa ni kitendawili.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Hata ukiiangalia mikataba ya kimataifa ya haki za
binadamu na maazimio yaliyofikiwa ndani ya Umoja wa Mataifa kushughulikia
ukatili dhidi ya wanawake na inayohitaji Serikali kuchukua hatua yote imelenga
ukatili dhidi ya wanawake, ikiwemo Mkataba wa Kutokomeza Aina Zote za Ukatili
Dhidi ya Wanawake<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>(CEDAW, 1979), Mkataba
wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake (DEVAW, 1993),Azimio la<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Beijing na Ulingo wa Hatua(1995), Mkataba wa
Mahakama ya Uhalifu Kimataifa<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>(Mkataba
wa Rome , 1998), Azimio la Milenia<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>(2000) na Azimio la<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Baraza la
Usalama 1325 juu ya<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Wanawake, Amani na
Usalama (2000), na mengineyo. </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Wimbi kubwa la kuwanyanyasa wafanyakazi wa
majumbani ambao asilimia kubwa ni wasichana linabadilisha kwa kiasi fulana
dhana nzima ya ukatili wa kijinsia. Manyanyaso haya kwa kiasi kikubwa
yanatekelezwa na wanawake. Ingawa kwa kiasi Fulani wafanyakazi hawa wa majumbani
wananyanyaswa na kudhalilishwa na wanaume, kama kuwabaka au kuwageuza nyumba ndogo,
lakini mateso makubwa dhidi ya utu wao na uhuru wao yanatendwa na wanawake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Biashara ya ngono, kwa kiasi Fulani inaendeshwa
na wanawake. Wanawakusanya wasichana wadogo sehemu mmoja, na hasa kwenye miji
mikubwa na kuwatumikisha kingono,<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>ni
aina Fulani ya utamaduni wa kule mkoa wa Mara, ambako wanawake wanao kwa lengo
la kuwa na wasichana wa kuwatumikisha kingono na kujipatia watoto. Utamaduni
huu unajulikana kama “Nyumbantobu”. Katika utamaduni huu, msichana anayeolewa
na mwanamke, anakuwa hana uhuru wa aina yoyote na mwili wake au na watoto
anaowazaa. Hii ni aina ya ukatili wa kijinsia, ambao ingawa wanatendewa
wanawake, lakini si ukatili wa wanaume. </span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">“Idadi ya wanaume wanaofika kwenye kituo cha
polisi kulalamika kupigwa na wake zao imeanza kuongezeka kwa kasi katika Jiji
la Dar-es-Salaam” Hayo yalisemwa na <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Kaimu Kamishana wa Polisi, Adolphina Chialo,
alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga
ukatili wa kijinsia, ulioratibiwa na Shirika la wanawake katika Sheria na Maendeleo
(WiLDAF).</span><span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW;"></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Utafiti uliofanywa tarehe 22.11.2013 kwenye Bar
ya Kisuma- Mwembeyanga-Temeke- Dar-es-alaam, umeongeza giza nene kwenye suala
zima la ukatili wa kijinsia. Wanawake sita ambao ni miongoni mwa wanawake wengi
wanaohudumia kwenye Bar hiyo walikuwa na maoni tofauti na yanayopingana juu ya
ukatili wa kijinsia. Wakati wanawake watatu<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>walikataa kushuhudia aina yoyote ile ya<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>ukatili na udhalilishaji wa wahudumu kwenye baa hiyo, wanawake wengine
watatu walilalamikia manyanyaso na udhalilishaji wa hali ya juu kwenye baa hiyo
ya Kisuma.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Utafiti ulifanywa Kisuma, baada ya kuwepo na
taarifa za unyanyasaji wa kijinsia kwenye baa nyingi za Dar-es-Salaam. Wahudumu
kulazimishwa kuvaa nguo fupi, kuonyesha sehemu kubwa ya matiti yao,
kulazimishwa kushikwa shikwa na wateja, kufanyishwa kazi masaa mengi kwa malipo
kidogo na matendo mengi <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>ambayo ni
kinyume na haki za Binadamu.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Adela Joseph (jina la kubuni), mhudumu wa Baa ya
Kisuma, alilalamika “ Tunafanya kazi masaa mengi, mshahara kidogo. Tunashikwa
shikwa na wanaume, ukilalamika unafukuzwa au unaambiwa hii si hoteli ya chai,
hivyo ni lazima kuvumilia… ukibeba mimba, unakuwa umejifuta kazi, maana ukienda
kujifungua, ndo mwisho wa kazi yako… hakuna haki hapa, tunanyanyaswa na
kudhalilishwa”</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Meneja wa Bar ya Kisuma, bwana Peter Jackob (jina
la kubuni), aliungana na wale wanawake watatu waliosema Kisuma hakuna
udhalilishaji. “ Mtu akimshika shika mhudumu bila ridhaa yake, sheria inachukua
mkondo wake. Tunatenda haki na kuhakikisha kila mhudumu anapata haki yake,
mishahara yetu ni mizuri na wana marupurupu mengi.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Bwana Kafana Mbyango (Jina la kubuni) mteja wa
Kisuma, aliyefuatilia maongezi yetu kwa karibu alisaidia kufumbua kitendawili cha
Kisuma; wanawake watatu na meneja wanasema mambo safi, wakati wanawake wengine
wanasema Kisuma kuna unyanyasaji wa kijinsia. “ Unajua wale wanaotetea, ni wale
wenye mishahara mikubwa, ni wale wenye mahusiano ya karibu sana na Meneja au
mwenye Bar, ni wale wakivunja gilasi, mishahara yao haikatwi. Kusema kweli hapa
Kisuma kuna unyanyasaji wa hali ya juu, nimeshuhudia mara nyingi wahudumu
wakidhalilishwa..”.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">“Kisuma, kuna udhalilishaji wa hali ya juu.
Kwanza, kwa maoni yangu mimi wanawake wote wa Kisuma, ni Malaya tu! Ukifanya
kazi kwenye Baa, wewe ni Malaya..” Alichangia kijana mmoja aliyeonekana kuwa ni
mteja wa kila siku pale Kisuma.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Ina maana pale Kisuma, wahudumu wanawake wenye
hali nzuri kimaslahi, wanabariki unyanyaswaji na udhalilishwaji wa wanawake
wenzao? Kwa maneno mengine, huu ni unyanyasaji wa wanawake unaoendeshwa na
wanawake wenyewe! Hiki ndicho tunachokiita kitendawili. Kazi kubwa iliyo mbele
ya wanaharakati na wale wote wenye mapenzi mema ya kutaka kuona ukatili wa
kijinsia unakomeshwa, wajitahidi kutegua kitendawili hiki. Tusipumbazwe na
utamaduni wa wanaume kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wanawake, tuliangalie na
kulishughulikia suala zima la unyanyasaji wa kijinsia: Wanaume wanawanyanyasa
wanawake, lakini pia kuna wanawake wanaonyanyasa na kuwadhalilisha wanawake
wenzao na wakati mwingine kuwanyanyasa na kuwadhalilisha wanaume.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Ukatili wa kijinsia, uzingatie suala zima la haki
za watoto: Wasichana kwa wavulana, haki za wanawake na haki za wanaume.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Na,</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-family: "Times New Roman","serif"; font-size: 14.0pt; line-height: 115%; mso-ansi-language: SW; mso-fareast-font-family: Calibri;">+255 754 633122</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-64215582275477214772013-12-09T23:25:00.001-08:002013-12-09T23:25:17.078-08:00GBV IN TANZANIA<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20433" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20441" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt;">GBV IN TANZANIA, A RIDDLE YET TO BE RESOLVED?</span></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20435" style="text-align: justify;">
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20437" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20439" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt;">When this week we start commemorating 16 days of
fighting Gender Based violence, In Tanzania the riddle needs expert to resolve
it. It is mostly believed that men commit GBV. Research from the Ministry for Health
and Social Welfare has revealed that 45 per cent of women aged 15 to 49 have
been victims of domestic violence. In addition, 75 per cent of children
experience physical abuse at the hands of family or authority figures before
they are 18 years old. Yet only 40 per cent of victims report the violence. Not
reporting the violence can be a part of the riddle, but here we are directing
our argument to something else.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20443" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20445" style="font-size: 14.0pt;">Some efforts
have been done in Tanzania to fight GBV For example, </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20447" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20449" style="font-size: 14.0pt;">President
Kikwete has publicly stated that gender-based violence should be included as
one of the Millennium Development Goals.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20451" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20454" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20453" style="font-size: 14.0pt;">Furthermore,
Tanzania’s Poverty Reduction Strategy Papers (PRSP), the National Strategy for
Growth and Poverty Reduction, lists violence against women as one of its
indicators of poverty—a feature that is rare among PRSPs in other countries. </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14.0pt;"> </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20457" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20456" style="font-size: 14.0pt;">Tanzanian
law has shown some progress in preventing and punishing GBV crimes. For
example, the Sexual Offence Special Provisions Act of 1998 poses harsh penalties
for perpetrators of sexual violence. However, gaps remain in the legal system.
In particular, domestic violence is only minimally and vaguely addressed in The
Law of Marriage Act—although without specified penalties—and through the penal
codes on general violence and assault. There is no law against domestic
violence, specifically. </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20460" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20459" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">House girls are facing Gender based violence,
which in most cases, women are involved than men. There are cases of rape among
house girls, but women fuel mostly the mistreatment they face. While the whole
world is blaming men in Afrika to<span> </span>be on
the read in GBV, women are also a apart of it.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20463" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20462" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">It is believed that in Tanzania, some women
are involved in human trafficking for commercial sex work; they transport girls
from different pats of Tanzania and bring them in big cities for commercial sex
work. It is a kind of slavery, where girls sell sex and handover money they
receive to their bosses who in most cases are women. This is one of the worst
GBV being practised in Tanzania. Even in villages in Tanzania, this practice is
there, a good example is “Nyumbatobu” culture practised in Mara region, where
women pay dowry to marry girls! It is believed that, one woman can marry up to
four or five girls. These girls are not free, they follow orders from their
bosses who are women. They sex with men chosen by<span> </span>their bosses and if it happens to have a
baby,<span> </span>the mother is always the bosses
who are women.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20466" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20465" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Recently the Assistant Police commissioner
Adolhina Chialo, said that “The number of men coming to police station to report
being beaten by their wives is increasing everyday in Dar-es-salaam. Even in
other places in Tanzania, there is this kind of report. Before, it was shameful
a man to report being beaten by their wives, but now things is changing”.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20469" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20468" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">A resent research carried on 22nd November
2013 at Kisuma Bar, Mwembeyanga, Temeke, Dar-es-salaam confirmed the GBV riddle
in Tanzania. Six women among many women working at this Bar were interviewed on
the GBV behaviour believed to be a culture of this Bar. Surprisingly, three
women responded positively, insisting not<span>
</span>to have experienced an kind of GBV at their working place. “ I am
enjoying my work, I have three children and they are all attending school, I am
able to pay for their school fees from the salary I receive from my work here
at Kisuma Bar” Mary Kaisi (pseudo name) commented during the interview. Even
the manager of Kisuma Bar supported their opinion, saying, “Kisuma Bar, is a
non GBV zone”. Other three women responded negatively, saying that Kisuma Bar,
is a place of GBV; they work long hours with a little pay, when a worker gets
pregnant, that is a self termination, they are exposed to sexual harassment to
attract the customers; when they complain of mistreatment their work is
terminated.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20472" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20471" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mr Kafana Mbyango (Pseudo name) a regular
customer of Kisuma Bar, was an eye opener of the GBV riddle at Kisuma Bar where
three bar maid supported the opinion of having GBV at<span> </span>the Bar and the other three were completely
against this opinion. “You know those who are against the opinion are being
paid well than the other three,<span> </span>they
have an intimate relationship with the manager and the proprietor. As longer
as<span> </span>they have good working conditions,
they seem not to consider gender based violence other workers are facing. In
other words these women are a part and parcel of GBV”</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20500" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20499" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Other customer Kafunje Kayoza (Pseudo name),
used GBV language “ My opinion is that all women working here at Kisuma Bar are
prostitutes! As longer us they are selling beer not tea, and they are working
for money, what do you aspect? They are abused morning till evening, at the end
of the day they end up in bed”</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20497" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20496" lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">The riddle is, while we are used to blame men committing
GBV, it seems in Tanzania women are also committing GBV. We need to direct our
efforts no only fighting violence against women, but Gender based violence in
the real sense. Is this riddle hiding only in Tanzania or it is in other
African countries?</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20494" style="text-align: justify;">
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">By,</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20492" style="text-align: justify;">
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Fr. Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="yiv3220367808MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_20490" style="text-align: justify;">
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 633122</span></div>
<span lang="EN-GB" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">pkarugendo@yahoo.com</span>pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-49390885259580180502013-12-09T23:22:00.005-08:002013-12-09T23:22:53.246-08:00MWALIMU THEOPHILDA TINKASIMIRE TIKAWA<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19242" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19241" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">MWANA MAMA MWALIMU THEOPHILDA TINKASIMIRE TIKAWA.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19244" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"> </span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19119" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19118" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Leo hii katika safu yetu ya Mwana mama tunawaletea Mwalimu Theophilda
Tinkasimire Tikawa. Maarufu kama Mwalimu Tinka. Mama mwenye tabasamu na
uchangamfu kila wakati, mwenye kuwapenda watu wote bila ubaguzi, mwenye
kuipenda kazi yake ya ualimu na roho ya kuwasaidia watu wanaomzunguka na hasa
wasiojiweza. Inawezekana sifa hizi zikawa zinapwaya kwa wale wanaomfahamu Mwana
mama huyu kwa karibu, lakini safu hii imejitahidi kiasi cha kuzidi nusu ya sifa
zake. <span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19388"> </span>Mwalimu huyu wa miaka mingi
anastaafu kazi ya ualimu mwezi huu baada ya kufikisha miaka 60 ya kuzaliwa. <span> </span>Bila kuona mvi zinazokipamba kichwa chake,
utafikiri ni binti mdogo wa miaka 30, yeye anajivunia mvi zake na hapotezi muda
wake kuweka rangi za kubadilisha rangi ya nywele zake kama wafanyavyo wengine
wanaogopa kuitwa “Bibi” au “Babu” kwa upande wa wanaume.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19248" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19231" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19230" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mwalimu Tinka, ni mama wa watoto 4, wajukuu 12 na watoto wengine wengi
aliowafundisha sehemu mbali mbali za Tanzania; Tanga, Tabora, Dar-es-Salaam,
Mbeya na Karagwe. Mama huyu ambaye kauli mbiu ya maisha yake imekuwa “ Kukata tama
ni dhambi” ni mfano wa kuigwa. Safu hii ilipoongea na mama huyu kwa nyakati
tofauti, amekuwa akisisitiza kauli mbiu yake: “Unajua nilipofiwa na mme wangu,
mnamo mwaka wa 1990, ningekata tama, nisingekuwa hivi nilivyo. Nisingeweza
kuwasomesha watoto wangu na kuhakikisha wanakua vizuri na<span> </span><span> </span>kuweza
kujitegemea. Sikukata tama, nilipambana na maisha na kumtegemea Mwenyezi Mungu,
sikufikiria kuolewa tena, bali niliweka nguvu zangu zote kulijenga taifa langu
la Tanzania kwa kufundisha watoto<span> </span>na
kuhakikisha ninawatunza watoto wangu” Alisema Mwalimu Tinka, akiongea na safu
hii.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19250" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19253" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19252" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Wakati anapostaafu na bado ana nguvu, Mwalimu Tinka anatamani “ Kuzunguka
Tanzania yote, nikitoa ushauri kwa wajane. Nimeishi maisha ya ujane, nafahamu
matatizo<span> </span>na uchungu wa kuwa mjane. Kama
kuna kita ambacho siwezi kukisahau hadi naingia kaburini ni tukio na kufiwa na
mme wangu. Hivyo natamani nieleze uzoefu wangu na kuwashauri wajane wenzangu
wazikate tama, maana kukata tama ni dhambi. Tatizo lililo mbele yangu ni
kutokuwa na uwezo wa fedha za kuizunguka Tanzania yote..” Anayasema haya kwa
uchungu mkubwa, maana anaonyesha hamu na nia yake ya kutaka kuizunguka Tanzania
nzima akiwashauri wajane.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19255" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19258" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19257" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa vile ana wasiwasi wa kutoweza kupata fedha za kuizunguka Tanzania,
nzima Mwalimu Tinka, ameaanza kuandika kitabu cha maisha yake. Anaamini, wajane
na watu wengine wakikisoma watapata la kujifunza.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19261" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19260" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mwalimu Theophilda TinkasimireTikawa, alizaliwa mnamo mwaka 1952 kijiji cha
Kasheshe – Nyaishozi –Karagwe. Ni mtoto pekee wa Baba Paul Koliko na Mama Agnes
Paul. Kati ya mwaka 1962 na 1968, alipata elimu ya msingi shule za Katoju na
Nyaishozi –Karagwe. Hakuweza kuendelea na elimu ya Sekondari, isipokuwa
alijiunga na Hospitali ya Nyakahanga –Karagwe, ambako alichukua mafunzo ya
kuwasaidia manesi kwa miaka miwili, na baadaye kutoa huduma kama nesi msaidizi.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19364" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19264" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19263" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Wakati akiwa mfanyakazi wa Hospitali ya Nyakahanga, alikutana na mchumba
wake Bwana Joseph Tinkasimile, aliyekuwa akifanya kazi Tanga, kama Afisa
Maliasili wa Mkoa wa Tanga. Walifunga ndoa takatifu kwenye kanisa Katoliki Karagwe
mwaka wa 1970 na kuhamia Tanga. Mungu aliwajalia kumpata Bruno mtoto wao wa
kwanza mnamo mwaka 1971 na mtoto wao pili Felix mwaka 1972. Mnamo mwaka 1974,
walijaliwa kumpata mtoto wao pekee wa kike Leticia Shubira Wamala na mwaka 1979
mtoto wao wa mwisho Victor alizaliwa.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19366" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19268" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19267" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kati ya mwaka 1976 hadi 1977, Mwalimu Tinka, alijiunga na chuo cha Ualimu
Korogwe na kusoma ualimu daraja la C. Katika hatua hii hawezi kumsahau mshauri
wake Mama Mazoko wa Bukoba, ambaye ndiye aliyemshauri asomee ualimu na
kuendelea kumshauri mambo mengi katika maisha yake. Hadi leo hii Mama Mazoko,
bado ni mshauri wa karibu wa Mwalimu Tinka. “ Mama huyu ndiye alitoa ushauri
nisikatwe mguu nilipopata ajali ya pikipiki kwenye miaka ya tisini. Bila
ushauri wa mama Mazoko, leo hii ningekuwa na mguu mmoja. Hivyo Mama huyu siwezi
kumsahau kwenye maisha yangu, alinishauri nisomee ualimu, na umenisaidia kwenye
maisha yangu na kuwasaidia wengi na bado anaendelea kunishauri” . Alieleza
Mwalimu Tinka, wakati alipoongea na safu hii ya Mwana Mama.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19370" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19369" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Baada ya kuhitimu. <span> </span>Mwalimu Tinka,
alianza kazi ya kufundisha Shule ya Msingi Kibasila – Dar-es-Salaam mnamo mwaka
1978. Mnamo mwaka wa 1979, alihamia shule ya<span>
</span>msingi Kitete –Tabora. Akiwa Tabora, aliteuliwa kuwa Afisa Utamaduni wa
michezo wa Manispaa(Mji) wa Tabora. Mwaka 1982 - 1983, Mwalimu Tinka alihamia
shule ya msingi Uyole Mbeya. Na mwishoni mwa mwaka wa 1983, alihamia Wilaya ya
Karagwe na kufundisha shule ya msingi Rwambaizi hadi mwaka2002. Kati ya 2002 na
2003, alifundisha kwenye shule mbili za msingi Nyamilima na Kituntu kule
Karagwe.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19270" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19273" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19272" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mnamo mwaka 2004, Mwalimu Tinka, alihamia tena Dar-es-Salaam na kufundisha
shule ya msingi Kizinga hadi mwaka 2005. Baada ya hapo hadi mwezi huu anapostaafu
alikuwa anafundisha shule ya msingi Toangoma na amejenga makazi yake huko
hukoToangoma.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19276" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19275" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa vile Mwalimu Tinka, hakusoma masomo ya sekondari, kati ya mwaka 1999 na
2000 alisoma na kushinda mitihani ya sekondari na kujipatia cheti cha kidato
cha nne. Pia mwaka 2011, alipata masomo maalumu ya mwaka mmoja ya ualimu wa
Chekechea. Lakini pia amepata fursa ya kusoma nje ya nchi masomo ya Demokrasia
na Uongozi nchi ya Denmark mwaka 1997.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19373" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19376" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19375" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mwalimu Tinka, amekuwa mama mshauri kwa watu wengi. Bwana Kaboko wa Dar-es-Salaam
na Profesa Faustine Kamuzola wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Morogoro, ni miongoni mwa
watu walionufaika na ushauri wa Mwana mama huyu.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19378" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19279" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19278" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Mwana Mama huyu, mbali na ualimu amekuwa kishiriki shughuli mbali mbali
katika jamii kama vile siasa na shughuli za kidini. Amekuwa mwanachama wa UWT
na aligombea nafasi za Ubunge wa viti maalumu, ingawa hakufanikiwa kuchaguliwa.
Hata hivyo aliendelea kujishughulisha na kazi za UWT na CCM.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19392" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19282" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19281" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Kwa upande wa shughuli za kidini, Mwalimu Tinka, alikuwa mwenyekiti wa
WAWATA jimbo katoliki la Rulenge, kwa kipindi cha miaka mitatu. Kazi hii
aliifanya kwa moyo wake wote na kipindi hicho ndipo alipata nafasi ya kusafiri
sana ndani na nje ya nchi.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19284" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19287" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19286" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Ukitoa kichwa chake kuwa na mvi, anaonekana ni kijana! Siri yake ni nini?
Anasema ni matokeo ya kutotunza kinyongo rohoni mwake. Amejaliwa karama ya
kusamehe! Amekumbana na migogoro mingi katika maisha yake na hasa baada ya
kumpoteza mme wake. Waliomsema vibaya, waliomzulia mambo ya uongo, aliwasamehe,
hakuweka kinyongo rohoni mwake. Mfano kuna wakati alisingiziwa kumshitaki
mwalimu mkuu aliyekuwa amevujisha mtihani wa darasa la saba, mgogoro huu
ulikuzwa hadi mtoto wake Victor akapigwa vibaya na kuumizwa na watu
wasiojulikana. Ingawa uchunguzi uliweza kubaini waliotendea kitendo hicho <span> </span>kwa mtoto wake, Mwalimu Tinka, aliwasamehe
watu hao.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19289" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;"><br /></span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19292" style="background-color: transparent; color: black; font-size: 18.6667px; font-style: normal; text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19291" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Hivyo tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa Mwana mama huyu anayestaafu kazi <span> </span>ya ualimu mwezi huu. Amekuwa Mwalimu wa mfano
shule zote alizozifundisha, amekuwa ni Mwalimu anayewapenda watoto, kuwajali na
kuwashauri, amekuwa mama, mzazi wa mfano kwa kuwalea watoto wake kwa maadili
mema, amekuwa ni mjane aliyesimama imara bila kuyumba, kuwakwaza watoto wake na
kuikwaza jamii. Bahati nzuri watoto wake hawakumwangusha, anamshukuru Mungu kwa
Baraka zake.</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19295" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19294" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Safu hii, inamtakia Mwalimu Theophilda Tinkasimire Tikawa, maisha marefu
wakati anapoanza maisha yake ya kustaafu!</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19297" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Na,</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19300" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19299" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">Padri Privatus Karugendo</span></div>
<div class="yiv9369833372MsoNormal" id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19303" style="text-align: justify;">
<span id="yui_3_13_0_ym1_1_1386655616878_19302" lang="SW" style="font-size: 14.0pt; line-height: 115%;">+255 754 6331 22</span></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3822388592381669189.post-44678377745810999972013-12-09T23:18:00.004-08:002013-12-09T23:18:59.365-08:00Uhakiki wa Kitabu - Chamani<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:WordDocument>
<w:View>Normal</w:View>
<w:Zoom>0</w:Zoom>
<w:TrackMoves/>
<w:TrackFormatting/>
<w:PunctuationKerning/>
<w:ValidateAgainstSchemas/>
<w:SaveIfXMLInvalid>false</w:SaveIfXMLInvalid>
<w:IgnoreMixedContent>false</w:IgnoreMixedContent>
<w:AlwaysShowPlaceholderText>false</w:AlwaysShowPlaceholderText>
<w:DoNotPromoteQF/>
<w:LidThemeOther>EN-US</w:LidThemeOther>
<w:LidThemeAsian>X-NONE</w:LidThemeAsian>
<w:LidThemeComplexScript>X-NONE</w:LidThemeComplexScript>
<w:Compatibility>
<w:BreakWrappedTables/>
<w:SnapToGridInCell/>
<w:WrapTextWithPunct/>
<w:UseAsianBreakRules/>
<w:DontGrowAutofit/>
<w:SplitPgBreakAndParaMark/>
<w:DontVertAlignCellWithSp/>
<w:DontBreakConstrainedForcedTables/>
<w:DontVertAlignInTxbx/>
<w:Word11KerningPairs/>
<w:CachedColBalance/>
</w:Compatibility>
<w:BrowserLevel>MicrosoftInternetExplorer4</w:BrowserLevel>
<m:mathPr>
<m:mathFont m:val="Cambria Math"/>
<m:brkBin m:val="before"/>
<m:brkBinSub m:val="--"/>
<m:smallFrac m:val="off"/>
<m:dispDef/>
<m:lMargin m:val="0"/>
<m:rMargin m:val="0"/>
<m:defJc m:val="centerGroup"/>
<m:wrapIndent m:val="1440"/>
<m:intLim m:val="subSup"/>
<m:naryLim m:val="undOvr"/>
</m:mathPr></w:WordDocument>
</xml><![endif]--><br />
<!--[if gte mso 9]><xml>
<w:LatentStyles DefLockedState="false" DefUnhideWhenUsed="true"
DefSemiHidden="true" DefQFormat="false" DefPriority="99"
LatentStyleCount="267">
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Normal"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="heading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="9" QFormat="true" Name="heading 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 7"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 8"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" Name="toc 9"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" Name="footer"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="35" QFormat="true" Name="caption"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" Name="page number"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="10" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" Name="Default Paragraph Font"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="0" Name="Body Text"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="11" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtitle"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="22" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Strong"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="20" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="59" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Table Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Placeholder Text"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="1" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="No Spacing"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" UnhideWhenUsed="false" Name="Revision"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="34" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="List Paragraph"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="29" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="30" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Quote"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 1"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 2"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 3"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 4"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 5"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="60" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="61" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="62" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Light Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="63" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="64" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Shading 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="65" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="66" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium List 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="67" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 1 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="68" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 2 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="69" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Medium Grid 3 Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="70" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Dark List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="71" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Shading Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="72" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful List Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="73" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" Name="Colorful Grid Accent 6"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="19" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="21" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Emphasis"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="31" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Subtle Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="32" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Intense Reference"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="33" SemiHidden="false"
UnhideWhenUsed="false" QFormat="true" Name="Book Title"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="37" Name="Bibliography"/>
<w:LsdException Locked="false" Priority="39" QFormat="true" Name="TOC Heading"/>
</w:LatentStyles>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 10]>
<style>
/* Style Definitions */
table.MsoNormalTable
{mso-style-name:"Table Normal";
mso-tstyle-rowband-size:0;
mso-tstyle-colband-size:0;
mso-style-noshow:yes;
mso-style-priority:99;
mso-style-qformat:yes;
mso-style-parent:"";
mso-padding-alt:0in 5.4pt 0in 5.4pt;
mso-para-margin:0in;
mso-para-margin-bottom:.0001pt;
mso-pagination:widow-orphan;
font-size:10.0pt;
font-family:"Times New Roman","serif";}
</style>
<![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapedefaults v:ext="edit" spidmax="2049"/>
</xml><![endif]--><!--[if gte mso 9]><xml>
<o:shapelayout v:ext="edit">
<o:idmap v:ext="edit" data="1"/>
</o:shapelayout></xml><![endif]-->
<br />
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">UHAKIKI WA KITABU: HAKI ZA MADEREVA, ABIRIA
NA POLISI BARABARANI.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="margin-left: .5in; mso-list: l0 level1 lfo1; tab-stops: list .5in; text-align: justify; text-indent: -.25in;">
<b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;"><span style="mso-list: Ignore;">1.<span style="font: 7.0pt "Times New Roman";">
</span></span></span></b><b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Rekodi za Kibibliografia.</span></b></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Jina la kitabu
kinachohahikiwa hapa ni Haki za Madereva, Abiria na Polisi Barabarani. ,
Kimeandikwa na Al-Muswadiku K.Chamani . Mchapishaji wa kitabu hiki ni Tanzania
Educational Publishera LTD(TEPU) na amekipatia namba ifuatayo katika sekwensia
ya vitabu duniani (ISBN): 978 9987 07 048 0 Kitabu kina kurasa 85 . Na
anayekihakiki sasa hivi katika safu hii ni mimi Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">II. <b>Utanguliz</b>i</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;"><span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Jina refu la kitabu hiki linastahili liwe “
Haki na Wajibu wa Madereva, Abiria na Polisi Barabarani kwa mujibu wa sheria na
kanuni”. Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu iliyochapishwa na Oxford
University Press, maana ya neno dereva ni mwendeshaji wa vyombo vinavyosafiri
nchi kavu, kama vile trekta, treni, motokaa, pikipiki na baiskeli; neno abiria
lina maana ya mtu anayesafiri kwa chombo chochote cha usafiri na neno polisi
lina maana ya askari mwenye dhamana ya kuona kuwa sheria na usalama wa nchi
hauvunjwi. Kwa upande mwingine, hakuna mtu mzima ambaye hajawahi kuwa abiria au
anayeweza kusema kuwa hatakuwa abiria maishani mwake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Ili shughuli za usafiri
na usafirishaji ziendeshwe kwa usalama, sheria kadhaa zimetungwa kuongoza
wadau, na makundi matatu, yaani Madereva, Abiria na Polisi hayaepukiki
kukutana. Wajibu wa polisi ni kuhakikisha kuwa sheria hizo zinazingatiwa kwa
usalama wa abiria na wadau wengine na wajibu wa madereva ni kuzizingatia.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Katika kufanya kazi hii,
baadhi ya polisi wa barabarani na wakubwa wao, hawana sifa nzuri. Wanatuhumiwa
na madereva kuwa hudai na kupokea rusha. Lakini, si polisi wote wanabebeshwa
tuhuma hii. Hata hivyo, mara nyingi madereva au/na vyombo vyao kweli huwa na
makosa. Lakini ni si wote huyakubali. Wao wanadai wameonewa, hata makosa
yanapokuwa dhahiri.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Lakini, sheria za
usalama barabarani zinasema nini katika kulinda usalama wa madereva, abiria na watumiaji
wengine wa barabara? Je, kwa mujibu wa sheria hizo, haki na wajibu wa Madereva,
Abiria na Polisi ni upi? Katika kitabu hiki, mwandishi, anayajibu maswali hayo
kwa utaalamu na umakini. Katika kurasa zinazofuata nitafanya uhakiki wa kitabu
hiki baada ya kukaangalia mazingira yanayokizunguka.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">III. <b>Mazingira
yanayokizunguka kitabu</b></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Tanzania, tuna tatizo
kubwa kutofuata sheria. Kwa maneno mengine hatupendi kufuata utaratibu. Unaweza
kutaja mambo mengi ambayo mara nyingi watanzania wanapenda njia za mkato. Na
kufuata njia za mkato ni chanzo cha rushwa katika taifa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Lakini kwa hoja iliyo
mbele yetu, njia za mkato zinasababisha vifo. Ajali nyingi za vyombo vya
usafiri na hasa vyombo vya abiria ni matokeo ya utamaduni wa kutofuata sheria.
Vifo vinavyobabishwa na vyombo vya usafiri vinaongezeka siku hadi siku. Wakati
polisi wanalaumiwa kuwanyanyasa madereva, kwa upande wao wanajitetea kuzingatia
sheria. Bila kuwapendelea polisi, ambao nao kwa upande wao kuna ambao
wanatanguliza rushwa na maslahi binafsi kabla ya sheria, kwa kiasi kikubwa
madereva wanachochea utamaduni wa rushwa kwa kutaka kukwepa usumbufu wa
kusimamishwa muda mrefu na maswali mengi.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Pamoja na ukweli kwamba
Tanzania, ina baadhi ya sheria ambazo ni nzuri, lakini watu hawazifuati na
kuzitekeleza. Ni wazi kuna baadhi ya sheria ambazo ni kandamizi na zilitungwa
wakati wa ukoloni na zinaendelea kuwepo kwa vile zinawalinda viongozi wanaokuwa
madarakani, kwa vyovyote vile ili maisha yaende vizuri ni vyema kufuata sheria.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Serikali, mashirika
yasiyokuwa ya kiserikali na watu wengine wenye mapenzi mema wamekuwa
wakijitahidi kuhimiza utawala wa sheria na watu kufuata sheria. Mwandishi wa
kitabu hiki Bwana Al-Muswadiku K Chamani, ni mmoja wao. Ameandika vitabu vingi
juu ya sheria mbali mbali katika taifa letu, baadhi ya vitabu hivyo ni: </span><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW;">Ufafanuzi wa Sheria ya
Kumiliki ardhi vijijini Tanzania, Mwalimu katika Sheria Tanzania, Fahamu kisheria
afisa mtendaji wa kata nchini Tanzania, Sheria ya ardhi: Umilikaji na matumizi
ya ardhi mkoani Kagera, Haki zangu mbele ya polisi, Haki za mwalimu Tanzania, Ufafanuzi
wa sheria ya kumiliki ardhi vijijini Tanzania. Na sasa kitabu hiki cha Haki za
Madereva, Abiria na Polisi Barabarani kinaongezeka kwenye orodha ya mwandishi
huyu.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW;">Wakati sote tunalalamika kwamba watu hawafuati
sheria, na wakati mwingine hata wale wanaofanya kazi serikalini hawafuati
sheria, mwandishi amevunja utamaduni huu wa kulalamika, na kuhakikisha anatumia
elimu yake ya sheria, kuwafahamisha watu sheria mbali mbali na kuzieleza katika
lugha nyepesi, ili kila mtu azifahamu.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW;">Mfano, alipoandika kitabu juu ya Watendaji wa
vijiji, watu wengi walifurahi kufahamu wajibu wa watendaji wa vijiji na mipaka
yao. Tabia ya watendaji wa vijiji kujifanya Miungu watu, kuwapiga watu na
kuwaweka ndani ilipungua sehemu ambazo vitabu hivi vilisambazwa. Ni wazi
watendaji ambao walitumia nafasi yao kujipatia fedha na mali kwa kuwanyanyasa
na kuwatesa wananchi, hawakukipenda kitabu cha Chamani, hata hivyo ukweli
unabaki pale pale kwamba tunahitaji utawala wa sheria.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW;">Huyu ni miongoni mwa watu wachache wanaotumia
elimu yao kuwaelimisha watu wengine na hasa kwa kuandika vitabu. Mzee Pius
Ngeze, amefanya hivyo kwenye kilimo na kuandika vitabu vingi vya kilimo katika
lugha nyepesi. Sasa na Chamani, anafanya hivyo upande wa sheria. Watanzania
wakijijengea utamaduni wa kusoma, na kuvisoma vitabu hivi, ni lazima maendeleo
ya taifa letu yatakwenda kwa kasi kubwa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Mwandishi wa kitabu hiki
ni wakili wa kujitegemea, aliyezaliwa wilayani Karagwe, mkoani Kagera, mwaka wa
1952. Al-Muswadiku K Chamani, maarufu kwa jina la “Kaka Alli”, alimaliza elimu
ya msingi katika shule ya Msingi Katembe iliyoko wilayani Karagwe, mwaka wa
1967 na kujinga na Shule ya Sekondari ya Nyakato, wilayani Bukoba, kuanzia
mwaka wa 1968 hadi 1971.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Baada ya hapo, alijiunga
na kozi ya ualimu katika Chuo cha Ualimu cha Tabora,mwaka 1972 hadi 1973. Kaka
Alli alianza kufundisha mkoani Mara katika shule ya Msingi Kanyega, wilayani
Musoma, mwaka 1974 hadi 1977. Alifanya mtihani wa kidato cha sita mwaka 1975 na
akafaulu kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam, kuanzia 1977 hadi 1980
alipotunukiwa shahada ya B.A. (Hons).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Aliteuliwa kuwa Mkuu wa
Chuo cha Maendeleo ya Wananchi wilayani Ngara mwaka 1981 na baadaye kuhamishiwa
wilayani Biharamulo mwaka 1982. Alijiunga tena na masomo ya Stashahada ya Juu
ya Sheria kuanzia mwaka 1983 hadi 1984, katika Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, akafaulu kupata shahada ya
Sheria (LLB- Hons) mwaka 2004.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Sasa hivi ni wakili wa
kujitegemea kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa akiwa katika kampuni ya Mawakili ya
Chamani And Company Advocates, makao makuu yakiwa ndani ya Manispaa ya Bukoba,
Kagera.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">IV. <b>Muhtasari wa
Kitabu</b></span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Kitabu kimegawanywa kwenye vipengele 50. Vipengele 1 – 8 vinaongelea;</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Wajibu wa raia katika kulinda sheria za nchi, wajibu wa Mwanasheria wa
Serikali na Kamanda wa Takukuru katika kuhakikisha sheria zinalindwa,</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Sheria zinazohusiana na usalama wa magari barabarani, Adhabu bila
kushatakiwa,, Kumkamata mtu aliyetenda kosa, Makosa ya taarifa na kuwekwa chini
ya ulinzi kwa makosa yasiyoorodheshwa katika kanuni ya taarifa ya makosa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">“</span></b><span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania,(Sura ya 2 R.E.2002) inampa raia wajibu wa kuhakikisha hifadhi ya
Katiba na Sheria za nchi” (Uk 1).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mteule wa Rais, madaraka yake
yanaonyeshwa katika Ibara ya 59 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
kuwa ni mshauri wa serikali juu ya mambo ya sheria na kutekeleza shughuli
zozote zenye asili au zinazohusiana na sheria zitakazopelekwa ofisini kwake au
atakapoagizwa na Rais kuzitekeleza na kutekeleza shughuli nyingine
zilizokabidhiwa kwake na Katiba hii au sheria yoyote” (Uk2)</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“Sheria zinazohusu usalama barabarani ambazo ni muhimu zaidi ni ni: Sheria
ya Mwenendo wa Makosa ya jinai,<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Sheria
ya Usalama Barabarani (sura ya 168 R.E. 2002), Sheria ya Leseni za Usafirishaji
(Sura ya 317 R.E. 2002), Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria ya
Moto na Jeshi la Uokoaji ( Sheria namba 14 ya mwaka 2007) na Sheria ya Mamlaka
ya usafirishaji wa Nchi kavu na majini (Sura ya 413 R.E. 2002)” (Uk 4).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“Fungu la 110 la Sheria ya Usalama Barabarani (Sura ya 168 R.E. 2002)
limeonyesha kosa ambalo likitendeka, basi, Ofisa wa Polisi atakuwa na madaraka
ya kumkamata mtuhumiwa” (Uk 11).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Vipengele kuanzia cha 9 hadi 25, vinajadili juu ya; Madaraka ya<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>polisi kusimamisha gari, kupekua na kuzuia
gari, Umuhimu wa Ofisa wa Polisi kufuata sheria, Tafsiri ya “Sababu za maana”,
Watoza ushuru wa maegesho kukamata gari na kuyafunga minyororo, Utaratibu wa
kupinga Sheria ndogo inayokinzana na Sheria andishi, Kuwa na leseni wakati wa kuendesha
gari, Mtuhumiwa kutoroka, Bima ya gari, Stika ya Wiki ya Nenda kwa Usalama
Barabarani, Leseni ya barabara na Stika ya Zimamoto, Kutoa kibao cha usajili wa
gari na kunyang’anywa leseni, Muda wa kulipa faini baada ya ilani ya kosa
kutolewa, Matumizi ya pikipiki kibiashara, Utaratibu wa kufuta leseni, Makosa
ya pikipiki ya biashara, Nani hulipisha faini za pikipiki za biashara, Muda na
kiwango cha kulipa faini ya pikipiki ya biashara, Nauli ya abiria na Kuweka
petroli wakati gari lina abiria.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“ Madaraka ya Polisi kusimamisha, kupekua na kuzuia gari lisiendelee na
shughuli zake yapo katika fungu la 25 la sheria<span style="mso-spacerun: yes;">
</span>ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (Sura ya 20 R.E. 2002)” (Uk 14).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“Mtu yeyote kwa makusudi anayetumia vibaya nafasi yake katika kufanya au
kushindwa kufanya tendo kwa kukiuka sheria, wakati akitekeleza wajibu, atakuwa
ametenda kosa..” (Uk 23).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“Iwapo itaonekana ( kuwa mtu huyo) hakuamini kuwa<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>(Mtu aliyetuhumiwa) alikuwa katenda kosa,
basi, hakuna “sababu ya maana” kwa upande wake na hawezi kusikilizwa kwa kusema
hali halisi ambayo ilikuwa haifahamiki kwake ingeweza kumfanya mtuhumiwa kuwa
na kosa” (Uk 24).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Juu ya matumizi ya Pikipiki kibiashara tunaambiwa na mwandishi kwamba:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">“ Kanuni za Lezeni za Usafirishaji (Pikipiki na Pikipiki yenye magurudumu
matatu) za mwaka 2010, zilizotolewa katika Gazeti la Serikali 144 ya mwaka
2010, imeruhusu pikipiki kutumiwa katika shughuli ya biashara ya kusafirisha
abiria kwa mashati yafuatayo:</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">- Kuwa na leseni halali ya huduma ya barabara inayotolewa na mamlaka ya
serikali za Mitaa inayohusika, vinginevyo ukiendesha pikipiki bila leseni hii
utakuwa umetenda kosa na ukitiwa hatiani utatozwa faini isiyopungua shilingi
elfu hamsini au kifungo kisichopungua miezi sita wala kuzidi mwaka mmoja au
vyote kwa pamoja.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">- Leseni hii, itatolewa kwa mwombaji mwenye pikipiki inayofaa kufanyiwa
biashara hii.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">- Mwombaji awe na umri zaidi ya miaka kumi na nane</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">- Mwombaji atapaswa kulipa ada, faini na gharama nyinginezo kwa SUMATRA
kupitia mamlaka ya Serikali za Mitaa ili kuweza kupata leseni hiyo” ( UK39)</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Juu ya<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>utaratibu wa kufuta leseni,
tunaambiwa kwamba: “Kanuni ya 19 ya Kanuni za Leseni za Usafirishaji (Pikipiki
na Pikipiki za Magurudumu matatu) za mwaka 2010 inaonyesha utaratibu
utakaotumiwa katika kufuta leseni hiyo iwapo atakiuka masharti yaliyotolewa” (
Uk 41).</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Vipengele vya 26 mpaka 40, vinajadili juu ya: Taarifa ya kito cha
kushukia, Gari likiharibika, abiria hurudishiwa nauli?, Ukaguzi wa gari kwa
kuwekwa chini ya ulinzi, Madaraka ya Ofisa wa Polisi Mkaguzi kukagua gari la
abiria, Wafanyakazi wa gari la abiria, Wajibu wa abiria, Uzito wa mizigo ya
abiria, Kulipia tiketi mapema na kusitisha safari, Nauli ya mtoto na
mwanafunzi, Kiwango cha nauli, Kutotoa huduma ya usafiri kwa muda uliopangwa,
Kosa la kutotoa tiketi ya nauli, Abiria kushindwa kulipa nauli nakuteremshwa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Juu ya taarifa ya kituo cha kushukia, tunasikia kwamba: “ Anayefanya
huduma ya gari ya kusafirisha abiria atapaswa ahakikishe anawatangazia kituo
kinachofuata” (Uk 48) na hii ni kwa mujibu wa “ Kanuni ya 103 ya Kanuni za
SUMATRA (Usalama wa Kiufundi na kiwango cha huduma (Magari ya abiria) za mwaka
2008. Hivyo ni lazima kituo cha kushukia kitangazwe, ingawa mara nyingi hawafanyi
hivyo, ni vizuri kupitia kitabu hiki abiria wakatambua haki zao ambazo mara
nyingi zinakiukwa.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Je Gari likiharibika, abiria hurudishiwa na nauli? Kanu ya 11 ya Kanuni
za SUMATRA(Usalama wa Kiufundi na Kiwango cha huduma) (Magari ya abiria) za
mwaka 2008, inaonyesha kuwa; “ Iwapo gari lililoharibika linafanya shughuli
zake katika maneno ya mji, basi, mwenye gari atapaswa atoe usafiri mwingine
ndani ya dakika kuma na tano au arudishe kiasi cha nauli ambacho kitamalizia
sehemu ya safari iliyobakia kwa kila abiria. Kama gari hilo linafanya safari za
nje ya mji, basi mwenye gari atapaswa alitengeneze <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>na kuendelea na safari ndani ya muda wa saa
mbili au atoe usafiri mwingine ndani ya saa mbili...... Kutokana na msimamo wa
kisheria ni kuwa, iwapo gari la abiria limeharibika, basi, unazo haki zako na
utapaswa utendewe kwa mujibu wa sheria” ( Uk 49)</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Ni abiria wangapi wanatendewa hivyo? Au ni abiria wangapi wanafahamu
kwamba sheria inawalinda na gari likiharibika ni lazima sheria ifuate mkondo
wake?</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Vipengele vya 41 mpaka 50, vinajadili juu ya: Vizuizi barabarani, Vizuizi
kwa ajili ya kutoza ushuru, Kuzuia polisi kufanya wajibu wake, Polisi
kufunguliwa madai akiwa kazini, Kutovaa helmeti ni kosa? Kukamatwa, kushtakiwa
na udhamini wa mahakamani, Pikipiki za polisi barabarani, Majedwali, marejeo na
mwisho kabisa ni wasifu wa mwandishi wa kitabu hiki.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Kwa kifupi kitabu hiki kinalenga kusaidia kupunguza ufa wa ushirikiano
uliopo kati ya madereva na wa vyombo vya usafiri vinavyotumia barabara, abiria
na Jeshi la polisi. Wananchi wakifahamu madaraka na wajibu wa polisi inakuwa
rahisi kushirikiana nao badala ya kuwaona kama maadui wake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-ansi-language: SW; mso-bidi-font-size: 12.0pt; mso-bidi-font-weight: bold;">Mada zilizogusiwa humu zinahusu zaidi Haki na Wajibu wa madereva wa
polisi wakiwa barabarani; utaratibu wa kumaliza makosa yaliyotendwa na dereva
wa chombo<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>cha usafiri; ukamataji wa
dereva na chombo chake; amri ya kulipeleka Kituo cha Polisi na magari ya
abiria, pikipiki za biashara, baiskeli na masharti yake.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">V. <b>Tathmini ya Kitabu</b></span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Baada ya kuona muhtasari huu sasa tufanye
tathimini ya kazi hii aliyoifanya Bwana Al-Muswadiku K Chamani. </span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Awali ya yote lazima niseme kwamba, kwa
kuangalia hadhira anayoikusudia mwandishi, kitabu kinasisimua, kinafundisha na
kinafikirisha kutokana na mtindo alioutumia mwandishi. <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Ametumia mtindo wa Maswali na Majibu
kuwasilisha ujumbe kwa msomaji, huku akinukuu vifungu vya sheria kwa makusudi
ya kuweka msisitizo na kufanya wepesi wa marejeo kwani sheria zilizo nyingi
hazipatikani kwa wadau.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Pili, <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>mwandishi kwa kutumia vitabu vyake hivi vya
sheria mbali mbali katika jamii yetu anatufumbua macho na kutuaminisha kwamba
utawala wa sheria unapofuatwa, basi, haki na amani vitakuwapo kwa manufaa ya
maendeleo.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Tatu, kama nilivyodokeza kwenye utangulizi,
mwandishi huyu anajiunga na waandishi wengine ambao baada ya kusoma kuihitimu
wanaitumia elimu yao kuwaelimisha wengine ambao hawakupata bahati ya kufikia
hatua hiyo ya elimu. Si kila Mtanzania anapata nafasi kusomea Sheria, hivyo kwa
kutumia kitabu hiki, hata yule ambaye hakusomea sheria anaweza kutetea haki
zake.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Nne, kitabu hiki kinakuja wakati wake, ambapo
magari yakiharibika abiria wanajijua. Ni wachache wanaofahamu haki zao. Sasa
wakisoma kitabu hiki, na kufahamu haki zao, kufahamu kwamba Gari, likiharibika
ni lazima mwenye Gari kuhakikisha abiria hao wanaendelea na safari wenye vyombo
vya usafiri wa abiria wataacha kiburi chao na vitendo vya kuwanyanyasa abiria.
Tunaweza kuanza kushuhudia mabadiliko makubwa katika usafirishaji wa abiria.
Uzuri wa kitabu hiki kinaelezea vizuri haki na wajibu wa kila mdau. Ni kwamba
kinasisitiza kufuata sheria ili mahusiano ya polisi, madereva na abiria yawe
mazuri.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Tano, kitabu hiki ni msaada kwa wadau wote,
madereva, abiria na polisi. Kuna wakati polisi anawakamata madereva, kwa uonevu
tu au kwa utamaduni wa kutaka rushwa na hasa sikukuu kubwa za kidini na kufunga
na kufungua mwaka zinapokaribia, lakini kwa vile madereva hawafahamu haki zao,
wanakubali kunyanyaswa na kutoa fedha. Hivyo madereva wakisoma kitabu hiki
watafumbuka macho na kuanza kuzitetea haki zao.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Sita, kwa upande wa mijini<span style="mso-spacerun: yes;"> </span>na hasa mikubwa kama vile Dar-es-Salaam,
Mwanza, Arusha, Mbeya na mingine, ambako karibia kila siku ya Mungu, kila mtu
anapanda magari ya abiria, kitabu hiki kitakuwa msaada mkubwa.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Saba, kwa vile sasa hivi tuko kwenye siasa za
vyama vingi, ufahamu wa sheria ni muhimu sana. Ule upendeleo wa wazi, kwa watu
wanaokiunga mkono chama tawala, kiasi hata cha kuvunja sheria zote hata na zile
za barabarani utakwisha! Sheria haina vyama, sheria haina dini na sheria haina
kabila. Hivyo kitabu hiki kitawasaidia wengi na uonevu wa ovyo utapungua.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">VI. <b>Hitimisho</b></span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Kwa kuhitimisha, nawaomba watanzania
kukitafuta kitabu hiki na kukisoma. <span style="mso-spacerun: yes;"> </span>Kusema kweli ni kitabu cha msaada kwa wale
wanaosafiri mara nyingi na vyombo vya abiria. Pia ni muhimu kwa polisi nao
kukisoma kitabu hiki ili kupunguza mapambano yasiyokuwa ya lazima katika ya
polisi na madereva.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Lakini pia ni muhimu kuvitafuta vitabu
vingine vya Al- Muswadiku Chamani na kuvisoma, maana vyote vinaelezea utawala
wa sheria.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Mwisho kabisa, nampongeza Bwana Al-Muswadiku
Chamani kwa kujitoa kuandika vitabu vya sheria ili kuwasaidia watu wengi ambao wananyanyaswa
na kupokwa haki zao kwa vile hawana utaalamu wa sheria. Vitabu vyake vimekuwa
msaada mkubwa kwa watu wa vijijini na hasa vitabu vyake vinavyohusu sheria za
Ardhi na watendaji wa vijiji.</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<br /></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Na,</span></div>
<div class="MsoBodyText" style="text-align: justify;">
<span lang="SW" style="font-size: 14.0pt; mso-bidi-font-size: 12.0pt;">Padri Privatus Karugendo.</span></div>
<div class="MsoNormal" style="text-align: justify;">
<br /></div>
pkarugendohttp://www.blogger.com/profile/03555493916102075228noreply@blogger.com0